Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano na maridhiano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional bila masharti yoyote, Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, wala haibembelezewi kwa vikao vya maridhiano, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, kwa kuweka mashinikizi ya mikutano na maandamano ya kudai haki hizo na sio kuziomba, na hapa ni pale tuu inapobidi, baada ya njia nyingine zote kushindikana ni katika kuipigania huku kuna wakati machozi, jasho na damu huweza kumwagika, katika kupigania haki.