ATCL, Reli ya Kati, TAZARA na SGR tuwape wanaoweza kuendesha kwa ufanisi mapema kabla ya kuumizwa

Naunga mkono hoja. Watanzania ni wezi, wavivu na watu wa kuendekeza starehe.

Nyerere alianzisha mashirika 400 lakini yote yalkuwa dhoofu hali by 1995
Hakuna mtu anazaliwa mwizi au mvivu, utaratibu mbovu wa kupata wenye sifa na uwezo kwa kazi husika ndio umefanya watu wawe wezi na wavivu!
 
Toka tupate uhuru hakuna shirika la umma linaloendeshwa na Watanzania likawa na mafanikio, tu wajinga wa hali ya juu.
 
Toka tupate uhuru hakuna shirika la umma linaloendeshwa na Watanzania likawa na mafanikio, tu wajinga wa hali ya juu.

Tatizo letu lina sehemu kuu moja, uongozi. Kwa miaka 60 hakuna akili mpya zaidi ya ile ya kulindana

Mwaka jana Mh Rais alipewa taarifa ya CAG, akawashughulikia wezi kwa kuwaambia '' Stupid'
Mwaka huu kapewa madudu yale yale tena yakijuridia kwa kasi, Rais atawashughulikia kwa neno ' Foolish'

Wizi unatoke tuna kila aina ya chombo na viongozi. Maana yake ni moja, hakuna anayejua tuna deal na nini na hakuna mwenye mbinu mpya. Inawezekana pia ni utamaduni wa kulindana siku ziende.

Hatuhitaji kuuza mashirika. Tunahitaji mashirika hayo yawe chini ya CEO , CFO, Operation Officer na Chief security Office kutoka Ulaya au America au Asia

Futa upuuzi wa bodi za mashirika. Waziri apokee taarifa tu asijihusishe na shughuli za mashirika
 
TAZARA inashindwa kutumia electronic payment ticket inasababisha kupoteza fedha nyingi mnoo,inashindwa na TRC wao Wana mfumo wa electronic
 
Hakuna mtu anazaliwa mwizi au mvivu, utaratibu mbovu wa kupata wenye sifa na uwezo kwa kazi husika ndio umefanya watu wawe wezi na wavivu!
Nyerere aliambiwa hakutaka kusikia. Aliambiwa kusema vbitu ni mali ya umma ni kosa kubwa sana kiuchumi, hakuelewa.

Kiko wapi?
 
..........ni kweli kabisa

Hata maisha yetu tuwape wanajua kuendesha maisha mazuri.
 
Hivi mashrika yanaoingiza pesa nyinyi yanakufaje?
 
Apewe kaka Yako Rosta
 
Hivi hata wewe unawalalamikia maccm wenzako??
Je, huko kwenye pindo na korido zenu za uchawa nako hamsikilizwi??
Au ndo mmetumwa kupima upepo kama kipindi kile cha DPW?
 
Lugha kali lakini ujumbe una mashiko. Ni bora wakabidhiwe akina "ROSTAM, MENGI, MO DEWJI, BAKHRESSA, SHIGONGO", n.k., lakini siyo watumishi wa Serikali!
 
Shida ya watu ambao wapo kwenye mfumo wanamawazo kama yako.

Niambie wewe kwanini tusijitegemee. Yani kila kitu tushikiwe kwani shule tulienda kufanya nini?

Kama kunawatanzania wanaweza kuendesha kwanini tusiwaachie? Matokeo yake tunakuja kuanza kulalamika kuwa Ajira hamna wakati wanapewa wageni🙌
 
Tulianza kujitegemea kuanzia wakati wa Nyerere mpaka leo tunashindwa. Kila tunachokianzisha au tulichokikuta tukikifanya kwa "kujitegemea" kinashindwa.

Misingi na dhana ya kujitegemea iliwekwa mibovu.

Tumuombe Mwenyezi Mungu, mama Samia aibomowe yote aijenge upya (Rebuild).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…