Azam TV badilisheni Tamthilia zenye mlengo wa itikadi za kidini

Azam TV badilisheni Tamthilia zenye mlengo wa itikadi za kidini

Halafu wa mlengo mwingine ndio wanafeli na kuonekana wadhalimu na dhaifu sana... yaani hata kubalance hizo filamu zao wanashindwa.🤣🤣🤣
Tena na misalaba yao kifuani😂
 
Kwanini usidili na wale wako chini ya mamlaka yako. Kama unaona ina maudhui ya upande mmoja, suluhisho ni kutokuwa mteja wao ila ukisema uwapangie cha kuonyesha utakuwa hujawatendea haki pia.
Wikendi nabadili kisimbuzi
 
Unakuta mgalatia nae anakenua mdomo na kukodoa macho from saa nne mpaka saa tano..nilishawakataza wanangu kuangalia hizo tamthilia zao za mapanga shwaaa..na za kidini hazimfundishi mtt wa kikristu lolote...
 
wakati mwingine njia bora ya kumwepuka mtu mjinga ni kukaa mbali naye.

binafsi huwa sioni mantiki ya kuingia ndani ya nyumba ya mtu halafu kuanza kupambana na ujinga uliopo ndani ya nyumba yake,mwache nao angalia mitikasi yako.

sio azam tu peke yake,ndugu zetu ktk imani huwa hawana utamaduni wa kutambua au kuheshimu imani nyingine,labd andivyo walivyofundishwa,suluhisho ni kutotumia bidhaa zao kabisa.sio kugome,hapana ni kujiepusha na makasiriko madogo madogo.
 
Jana nimerudi nimechoka nikafikia kujitupa tu kwenye kiti hakukuwa na mtu sebuleni ila TV ilikuwa inaonesha chaneli ya Azam 2

Macho yangu yakaona kipande kimoja kwenye tamthilia ya kituruki bila shaka inaitwa Alpasalani nadhani, Sasa Kuna Binti alikuwa Yuko kwenye mtego na viongozi wa utawala mwingine inaonesha huo utawala una Ukristu maana askari wake wana misalaba kwenye mavazi yao.

Sasa hawa askari aisee ni midebwedo vibaya mno yaani mwanamke moja anaua infidels (humo wanaita wadhalimu) zaidi ya 20 mbele ya kiongozi wao halafu Yuko pekeake na bado anaendelea kusurvive!? Duuuh ina maana hao ni wanyonge kiasi hiko? Halafu mule inaonesha waislamu ni watu wema sana na wakristu ni watu wenye Roho mbaya mno na hii chanel secular ila inabagua Imani moja na kuipendelea ingine.

Ututuki ni nchi ambayo raia wake wengi ni waislamu hivyo ni sawa kuwa na maudhui kama Yale, Sasa Tanzania hii ni multi religion county huwezi kuwa na maudhui hayo hayo tu kila siku ya kukandamiza Imani moja na kuipendelea ingine kulikuwa na;
  • Ertugrul
  • Ottoman
  • Barbarossa na Sasa ni hii
  • Alpasalani
Zote hizi maudhui ni yaleyale.

Azam tv badilikeni, hela tunalipa sisi lakini mnatutibua nyingi makusudi kabisa.

Na huu mwezi nitaacha kulipia hiki kisimbuzi kama ni ligi kuu nitaangalia bandani na kisimbuzi nitanunua cha startimes.

Azam tv mjifunze kwa wenzenu, mbona wao wanajua mipaka yao.

Mnakera bwana aah!
Achana na tamthilia tazama vipindi vingine
Usiwapangie watu , huwezi nunua Star times
 
Shida sio kuwa na maudhui ya kidini naomba unielewe ndugu yangu katika Imani
Shida ni kupambanisha Imani za watu, moja kuichora kama Imani safi na nyingine kuwaita wadhalimu hii si sawa, na tena wanatumia hadi nyenzo takatifu za Imani nyingine kudhihaki

Mbona bongo movie zipo movie nyingi tu ambazo huegemea desturi za kiislamu lakini bila kukashifi Imani ingine? Movie za madebe na hata Mohamed nurdin nyingi tu ziko hivyo
Unamaanisha crusaders sio? Waliua pia wakristo, na ile ni historia ya kweli, crusader ni kama unavyoona Nazi, Fascists ama Zionism ni movement tu za watu weupe ambao walikua wakijiona superior na wana haki ya kutawala dunia, na wengine si viumbe vikamilifu.
 
wagalatia bana, kwahio mkuu umeona dada wa kiislmau kashika panga anakata vichwa wagalatia wenzio umehuzunika sana
 
Hakuna maudhui yeyote ya Kiislamu kwenye tamthilia za kituruki,kama kweli unauelewa uislamu
 
Back
Top Bottom