Azzan Zungu ataka mazungumzo Bandari ya Bagamoyo kunusuru tatizo la ajira

Azzan Zungu ataka mazungumzo Bandari ya Bagamoyo kunusuru tatizo la ajira

Tanga na Mtwara mbona zinapanuliwa kitambo tu lakini ujenzi unaenda taratibu sana sababu bajeti ipo stretched sana.

Sababu kubwa ya Bagamoyo ni muwekezaji ndio ameonyesha opportunity hapo sio kwamba pesa ni yetu tunaweza amua wapi iwekwe. But maadam ni Tanzania hakuna hasara yoyote hta Gesi ipo mtwara but inachakatwa Dar!!

Bagamoyo kwa maoni yangu ipo karibu na social amenities nyingi kwa uwepo wa Dar tu mfano SGR, Airport kubwa, service sector karibu yote imejikita Dar (Bima,logistics etc) so Bagamoyo itakua kma extension tu ya jiji la Dar but kwa Mtwara inabidi mpka lami zijengwe, Airport zitanuliwe, mfumo wa Reli na vitu kibao vianze kujengwa upya so inakuwa disadvantage kwa uwekezaji mkubwa kama huo.
Kwa maoni yako "Mwenye aliye nacho aongezewe zaidi"?

Bagamoyo ni sehemu nzuri ya kuwepo kwa bandari ya nguvu; lakini kwa sababu tunataka maendeleo yaenee nchi nzima, ni bora tuweke jitihada za ziada kuwekeza na huko kwingine, ili nako mchango wao kwa taifa uonekane.

Ukiangalia tu hata ramani, pakiwepo bandari yenye uwezo mzuri Tanga, na miundombinu (iliyopo) kama reli na barabara ikaimarishwa, bandari hii itakuwa na umuhimu wa kipekee sana kwenye eneo lote la kaskazini hadi kuelekea kwenye ukanda wa Ziwa, hadi Uganda, DRC na kwingineko.
Hii itakuwa ni bandari muhimu inayofanya kazi kwa pamoja na hii ya Dar.

Tukiimarisha bandari hiyo, sehemu hizo zinazonyemelewa sana sana sasa hivi na bandari ya Mombasa, hawatakuwa na usumbufu tena wa kusubiri mizigo toka Dar.
Usafiri wa ndani ya Ziwa Victoria utawafanya waganda wengi kutegemea bandari hii. Kifupi ni kuwa itaweka ushindani mzuri sana kwa Mombasa.

Sasa hivi Mombasa wanategemea kushika sehemu zote hizo bila ushindani - Kilimanjaro, Arusha, Manyara, na hata sehemu za ukanda wa ziwa, maeneo haya hatimaye yatashikwa na Mombasa, na hakuna atakayezuia hilo lisitokee.
 
kwanini hao wanaoitaka sana hii bandari wasituwekee mkataba tuuone tujiridhishishe nini nchi yetu itapata ili huo ujenzi uendelee
giphy (2).gif
 
Bandari tunazungumzia sekta binafsi kuwekeza kwenye taasisi za uma mahali ambapo Serikali haina uwezo wa kuwekeza
Hapana kwani PPP inafanyeje kazi? Kuna hospitali za Rufaa zinamilikiwa na taasisi binafsi kwa ushirikiano na serikali. Hata kuna shule ya serikali ya viziwi ila inaendeshwa na benki fulani!! Yaani wao wanaweka majengo serikali inatafuta walimu n.k

Kwenye karne ya 21 biashara zinafunguka zaidi so ushiriki wa serikali unabaki kwenye udhibiti tu sio mpaka ishiriki moja kwa moja kwenye kuendeleza bandari/viwanda n.k

Ndio maana kuna kampuni za ulinzi ilihali kuna polisi, kuna private investigators ilihali kuna TISS n.k so sio vibaya serikali ika focus kwenye kuweka mazingira wezeshi kma miundombinu alafu ikaachia mambo mengine sekta binafsi yenyewe isubiri kodi tu na mapato ya wananchi wake wanaopata ajira.
 
Sasa hapo upigaji wake uko wapi?

Umasikini ni mbaya sana
NSSF wangewalipa Wananchi wenye maene yao vizuri, sema Manji akaja akawanyanganya Tonge la mdomoni kwa ujanjajanja, halafu yeye Manji akavuta Mkwanja mrefu sana kutoka NSSF!! Hapo huoni Kama Muhindi kawapiga Watanzania wenzako wasiokuwa na uelewa wa Mambo yanavyokwenda huko ndani!? Wewe unadhani Kama kweli Wananchi wangeambiwa mapema kuna mradi unakuja na watalipwa, unadhani wangekubali kumuuzia Manji maeneo yao!?

Tujifunze kuwapa Wanyonge haki zao hata Kama tunaona akili zao zimelala na wala hata hawajui kuwa wana haki zao!! Manji aliwapiga kwa kuwa hawana information za kutosha!! Au wewe unadhani bila huo Mradi Manji angethubuti kununua hayo maeneo kwa wakati huo!? Viongozi ndiyo walitakiwa wawape information raia wao, lakini information wamempelekea Manji kimyakimya!!
 
Bandari hii ni muhimu sana lakini tu alimradi usiingilie utendaji kazi wa bandari zingine wala mamlaka zetu za mapato zisiwekewe vikwazo za ukusanyaji mapato katika bandari hii mpya ya Bagamoyo aidha ni bora tukaziuza ndege zote tukabaki na mbili tu na fedha zote zikaingizwa katika mradi wa BAGAMOYO.
Hiyo hela haitatosha
Pale inatakiwa zaidi ya trillion 20
 
Uchumi wa Singapore na Malaysia wanategemea bandari mkuu,kwa hiyo bandari ni mojawapo ya vyanzo vya mapato kwa asilimia kubwa vyenye uhakika kwa mwaka
Sawa kwan hizi zilizopo hatuwez kuboresha ili kuongeza mapato??

Acheni kuuza nchi wajukuu wenu watakuja kuwalaani
 
NSSF wangewalipa Wananchi wenye maene yao vizuri,sema Manji akaja akawanyanganya Tonge la mdomoni kwa ujanjajanja,alafu yeye Manji akavuta Mkwanja mrefu sana kutoka NSSF!! Hapo huwoni Kama Muhindi kawapiga Watanzania wenzako wasiokua na uwelewa wa Mambo yanavyokwenda huko ndani!? Wwe unazani Kama kweli Wananchi wangeaambiwa mapema kuna mradi unakuja na watalipwa,unadhani wangekubali kumuuzia Manji maeneo yao!? Tujifunze kuwapa Wanyonge haki zao hata Kama tunaona akili zao zimelala,na wala hata hawajui kuwa wana haki zao!! Manji aliwapiga kwa kuwa hawana information za kutosha!! Au wwe unazani bila huo Mradi Manji angethubuti kununua hayo maeneo kwa wakati huo!? Viongozi ndiyo walitakiwa wawape information raia wao,lakini information wamempelekea Manji kimyakimya!!
Manji ni mfanya biashara. Angewatapeli hayo maeneo bila kuwalipa, ningekuunga mkono kuwa aliwapiga. Lakini waliuza kaa hiari yao wenyewe.

Tuache hizi mambo za kutaka kuonewa huruma kwenye ulimwengu wa ukweli
 
Mchezo Kama huo aliuufanya pia Manji huko Kigamboni, baada ya kustuliwa na watu wa ndani kuhusu Ujenzi wa Daraja la Kigamboni kupita,yeye Manji akawafuata Wakazi wa pale kwenye mradi na kuwarubuni kununua Viwanja vyao kwa M7 kwa kila mwenye kipande chake Cha Aridhi na kweli wengi walimuuzia maana walikuwa hawajui kuwa mradi tayari unakuja, na wale wachache waliojuwa walitishwa kuwa watanyanganywa Aridhi yao na Serekali,basi kwa haraka haraka nao wakakubali kumuuzia manji, japokua kuna wachache sana wao walichukua pesa kwa Manji na bado wakamkatalia, hao wengi wao walikua Wanajeshi wastaafu,

Sasa Mradi ulivyo kuja tu,ukakuta tajiri Manji ndiyo mmiliki wa eneo lile, Sasa ndiyo ikabidi wakae na Manji awauzie,Sasa hizo bei zilizopigwa hapo! Manji alipiga pesa ndefu sana,na ndiyo maana itachukua muda mrefu sana lile Daraja la Kigamboni kurudisha pesa zote za Mradi!! Matajiri wengi ni Wapigaji!!
Duuuh kumbe Hawa watu ni wahuni hivi?? Daaah
 
Uchumi wa Singapore na Malaysia wanategemea bandari mkuu,kwa hiyo bandari ni mojawapo ya vyanzo vya mapato kwa asilimia kubwa vyenye uhakika kwa mwaka
Unaweza kulinganisha akili ya Malaysia na Singapore na akili ya Bongo ya hivi karibuni? Hatuwezi kuiga ujenzi wa bandari Singapore peke yake bila kuyawwza mwngine madogo tu, kwa mfano; kuchaguana na kupeana madaraka kwa misingi ya sifa zinazofaa! Tunashindwa!
 
Mbunge wa Ilala ameomba muongozo leo Bungeni Dodoma kuhusu mpango wa Serikali kuanzisha mazungumzo tena ya bandari ya Bagamoyo kutokana bandari ya Dar es Salaam kuzidiwa na kutokuwa na uwezo wa kuingiza meli kubwa. Zungu amesema bandari ya Bagamoyo itapelekea kuanzisha viwanda, kuleta ajira na gateway kwa Bagamoyo.

Zungu amesema ulikuwa mpango wa Serikali kuanzisha Industrial Park Bagamoyo lakini wakapata mgogoro wa kimkataba.

Ni kweli mwenda zake baadhi ya mambo yake yalikuwa ya kuumiza watu, ila kwa swala bandari ya Bagamoyo mkataba ule ni ng'ombe pekee anayeweza kuukubali sababu hana utashi wa kujua jema au baya, sasa baadhi ya wabunge wanaibuka wakati huu bila kufiria hata jinsi ya kurekebisha mkataba wenyewe 10% inawabana kama kuku anayetafuta pa kutagia.
 
zungu hafai hata kuwa mwenyekiti wa mtaa ni waovyoo sana ilala haina barabara za maana magufuli alimchagua kuwa waziri wa mifuko ya nailoni rais alijuta kupa uwaziri
 
Mradi wa bandari ya bagamoyo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa nchi yetu na utaleta ongezeko kubwa la ajira na uzalishaji wa bidhaa kutokana na eneo mwambata la industrial area.Unafaida nyingi huu mradi kuliko hasara nashauri serikali isaini utejelezaji wa mradi kwa kuzingatia win-win situation #mh Rais na watendaji wako tafadhalini tumewapa dhamana msisite kufanya maamuzi magumu yenye tija.Mradi wa ges Lindi tafadhali harakisheni utekelezaji wake nchi inufaike na rasilimali hizi
 
Angalau jana niliona Wakenya wanaandamana kutaka mikataba ya ujenzi wa SGR iwekwe wazi...japo wameishachelewa,
" ...akili zangu ndogo huwa zinajikita kwenye uadirifu wa hawa wanaochombeza kuhusu huu mradi, kwanini wote ni watu wenye rekodi zenye utata kwenye utumishi wao?..."

..Je, watanzania tunajua kilichomo ktk mikataba ya ujenzi wa sgr au stieglers gorge?
 
Wabunge wetu ni mbumbu, how we vote for imbeciles, I just can’t understand. Funga bunge na Pima akili zao, 99% ni vichaa, they have serious mental issues!
Hapana siyo vichaa, wanajuwa watakacho, its all about 10% in dollars...
 
Bandari hii ni muhimu sana lakini tu alimradi usiingilie utendaji kazi wa bandari zingine wala mamlaka zetu za mapato zisiwekewe vikwazo za ukusanyaji mapato katika bandari hii mpya ya Bagamoyo aidha ni bora tukaziuza ndege zote tukabaki na mbili tu na fedha zote zikaingizwa katika mradi wa BAGAMOYO.
Bandari ya Bagamoyo haiwezi kujengwa pasipo kuzuia utendaji wa bandari zingine, ni sharti la lazima linasemwa kuwepo ndani ya mkataba. Huwezi kupata vyote.
 
Umuhimu wa bandari sio tatizo, tatizo ni mapato yatokanayo na bandari yanamnufaisha nani? Hata hiyo Dar Port, container terminal kwa undani anaefaidika ni TICTS siyo TPA sababu ya mikataba mibovu.

Iwe kupanua bandari za Mtwara, Dar na Tanga au Kujenga bandari upya kama Bagamoyo, Kilwa n.k, tusiwabebeshe wananchi mzigo mzito wa madeni wakati mfaidika au wafaidika ni watu wachache.

Mkataba wa ujenzi wa Bagamoyo uwekwe wazi ili umma ujue mazuri na mabaya yaliomo.
 
Back
Top Bottom