Baada ya kutangaza kugombea u/kiti CDM, ni kosa TAL kuendelea kuwepo nchini. Wakati sahihi kuwepo ni siku ya uchaguzi wenyewe. Sababu hizi hapa.

Baada ya kutangaza kugombea u/kiti CDM, ni kosa TAL kuendelea kuwepo nchini. Wakati sahihi kuwepo ni siku ya uchaguzi wenyewe. Sababu hizi hapa.

Ana maadui wengi, Kwa hiyo hawezi kujulikana yupi kamudhuru.
1. Adui walioko ndani ya chama chake wakihusika watasema ni watawala.
2. Watawala wakihusika watasema ni maadui ndani ya chama chake.
3. Vyama vingine vya upinzani vikinusika vitasema ni watawala au wenzake ndani ya chama chake.
Kwanini kati ya hao watatu mmoja wao anaweza kuhusika na asihisiwe ni yeye na kwa nini ahusike. Nikianzia mwisho.
1. Vyama vingine vya upinzani; kama TAL atapata uenyekiti anaweza kukiimarisha chama hicho na kuzidi kuvifanya vikose nguvu na kukimbiwa zaidi na wanachamq wake. Kwa kuhusika kumudhuru TAL vinaweza kunufaika kupata wafuasi wa TAL wataokimbia CDM kwa hasira.
2. Kwa chama tawala; kwanza kina hofu na msimamo ya TAL, kina amini utulivu utaondoka nchini kama hakitatawala kwa haki. Na kwa walivyo wazuri kutengeneza propaganda hata wakihusika itaonekana ni Mbowe na chawa wake kama alivyowaita leo kwenye press. Makosa ya tweet kama Ex Mayor wa Ubungo kuita uamuzi wa TAL kugombea ni vita. Kunaweza kuhalarisha uhusika wa maadui ndani ya chama chake.
3. Uhusika wa CDM; kinaweza husika hasa kundi la wale wasiomuunga mkono na kujisafisha kuwa ni watawala wahusika wa hilo.
Kwa mtazamo wangu TAL anapaswa kuondoka hata Leo nchini, ili arudi siku ya uchaguzi ndani ya chama chake. Anaweza ratibu kampeni yake akiwa hata Kenya kwani hata mwilini mwake ana damu ya wakenya. Nahitaji kupiga kampeni sana, na alivyo na uwezo kujieleza anaweza shida kwa kujieleza ndani ya dk 5 tu siku ya kupiga kura.
Hapa sasa ndio maana ya uhuru,haki,uadilifu na uwajibikaji unapopata maana halisi.Ila kwakuwa taifa limeamua kuchukua mkondo ambao wasio taka haki,uhuru,uwajibikaji basi kila mmoja atayatafuta maslahi yake.Kwa namna ipi?Itajulikana huko tuendapo,hii sii jambo lenye afya kwa taifa na watu wake.Tafsiri ni nini,wapo tulio waamini kuhakikisha hatufiki huku ila wamethibitisha kushindwa majukumu hayo.
 
Back
Top Bottom