Baada ya mahojiano ya Chief Odemba na Tundu Lissu leo nimeelewa kwa nini dereva yuko Ubeligiji

Baada ya mahojiano ya Chief Odemba na Tundu Lissu leo nimeelewa kwa nini dereva yuko Ubeligiji

Hivi Lissu mwenyewe hawezi kufungua mashtaka ya jaribio la kutaka kuuliwa? Inaonekana anaushahidi mwingi sana.
 
Mtailalamikia polisi mpaka Yesu arudi.
Usitegemee polisi watende haki kwa wapinzani ikiwa hakuna katiba mpya.

Hii katiba imelilink moja kwa moja jeshi la polisi na wanasiasa, CPF (IGP) anateuliwa na mwanasiasa, CPF anawateua ma-RPC, upandaji vyeo wa jeshi la polisi unategemea mwanasiasa huyo huyo mteuzi (kuanzia ngazi ya ACP kupanda juu) hawa ma-ACP ndo ma-RPC, unategemea nini kama sio kufuata maelekezo na matakwa ya mwanasiasa ili wapande cheo?

Rejea sheria ya jeshi la polisi na polisi wasaidizi, waziri anatoa maelekezo kwa polisi kwa mujibu wa hiyo sheria, polisi wataenda kinyume?

Katiba mpya kwanza, jeshi liwe huru ili wasiingiliwe na wanasiasa
Hakuna haja ya katiba Mpya na Polisi kutenda haki!!

Polisi wafuate PGO na kutenda haki!!

Wafanye kazi kwa miongozo na ethic's zao over
 
Unamkumbuka Ulimboka? Mo je? Basi huenda alipewa vitisho vikali na sehemu ya kutoa taarifa ni kwa hao hao watekaji!

Bila shaka + udhalilishwaji nyuma ya camera vinginevyo kila mtu atajua yaliyomsibu mtu na heshima zake.
 
Jaribu kuishirikisha akili yako vyema kabla uandike huu upuuzi wako hapa! Kama kwenye chama Chao Kuna muuaji kwanini basi polisi isichunguze na kuwabaini? Au nao wapo juu ya Sheria? Unaichafua polisi kimtindo siyo? Yaani muuaji awe cdm halafu hao policcm wamwache tu badala ya kuchukua ujiko ili wapande vyeo! Na zile cctv camera kwenye nyumba aliyokuwa akiishi kalemani zilinyofolewa na cdm?
Kama mliweza kumnyofoa uhai chacha Wangwe mtashindwa nini' kwa lissu?!!! Kama mliweza kumnyofoa jicho na meno kibanda siku Moja tu baada ya kuandika jambo la kumsifia jk kwa jambo flani mtashindwa kumshughulikia lissu na wengine?!!!! Kawadanganyeni mapoyoyo, mi Niko makini sana!
 
Polisi ni chombo cha wanasiasa waliopo madarakani..... uwezo wao wa kufanya upelelezi ni mkubwa sana, ila kama wanasiasa hawajaamua, unaweza kuua mtu mbele ya kamera na wakasema hatumjui mtu huyu
 
Itakumbukwa kuwa IGP Simon Siro alisema polisi wameshindwa kuendelea na uchunguzi wa kisa cha Tundu Lissu kupigwa risasi kwa sababu hakuwepo Tanzania. Lakini hata baada ya Lissu kurejea nchini bado polisi walisema hawawezi kuendelea na uchunguzi hadi dereva wake naye arejee kwa sababu ndiye aliyeshuhudia risasi zikipigwa. Lakini pia hadi leo polisi hawajafungua jalada la uchunguzi wa tukio hilo la kijinai na kigaidi.

Katika mahojiano hayo Lissu amesema anaishtaki kampuni ya Tigo kwa kuhusika kwake kutoa taarifa zilizofanikisha Makonda na genge lake kumpiga risasi.

Kwa sasa Tundu Lissu amekamilisha maadalizi ya kufungua kesi hiyo na miongoni mwa watu watakaoitwa kutoa ushahidi ni polisi, Makonda na dereva. Kwa sababu hiyo ni wazi dereva ni mtu muhimu sana katika kesi hiyo na kuja kwake nchini kunaweza kusababisha ushahidi wake kupotea au kupotezwa. Nadhani imeeleweka " kupotea au kupotezwa"!
Tafuta story yenye mashiko basi Tundu Lisu mwenyewe anasapoti ushoga na yupo huru, eti dereva wake atapotezwa, mfyyyyyuuuu!
 
Back
Top Bottom