Baadhi ya fani zenye ajira kubwa Duniani: Wazazi somesheni watoto nje Degree za Cyber Security na Aeronautical Engineering

Ah ah
Dah mkuu unatu motivation speaker au ya kweli haya.

Yaani utaamjniwa vipi bila cheti sasa??
Hebu tufafanulie kabla hatujaenda darasani.
Me nilisoma ICT(informational communication technology)
Mzee nawe unauza kava nini...yote maisha kweli
 
Kwa ajira mkuu hapo ni tatizo. Nadhani mimi na wewe tunahusika pia ktk kutengeneza ajira kwa vijana.
Ni sawa kweli tunapaswa kuzitengeneza ajira kwa vijana wenzetu ila mazingira yanayotuzunguka na hata selkali ilipaswa angalau hata kwa miaka 5 hii tatizo la ajira lingepungua kwa namna moja ama nyingine ila tukiangalia ajira za selkali sidhani kama ni nyingi kipindi hiki kama miaka ya nyuma
 
Waombe jeshini
 
Hongera kwa hiyo hatua.Nakuombea ufanikiwe ili tuongeze wataalamu wa cyber nchini wenye soko hadi kimataifa.
 
Mkuu naomba mwongozo nina dogo anamaliza olevel mwaka huu anapenda sana haya mambo, naomba nishauri apige course/certification zipi kwa kuanzia hataki kwenda advance yeye pia ni mtundu wa computer. Physics na number ni mzima pia. Nashukuru
 
Mie ni Cyber Security ( Penetration tester)... kwa hapa bongo bado maluwe luwe tu, labda wasome huko na wabaki huko huko ulaya.. ila sio hapa bongo
 
Kuna kozi nje ni hot cake ila ukirudi huku utasugua benchi vizuri.

Hiyo Aeronautical Engineering kuna jamaa yangu nilisoma nae A'Level akabahatika kwenda nje kusoma karudi saizi mwaka wa 3 yupo anaendelea kubeba bahasha ya kaki mtaani.

Huwa nikikutana nae mtaani naona ana stress haamini, huwa namwambia mzee baba vyeti tuviweke ukumbusho ndani. Tuendelee kupambana na harakati nyingine za maisha.
 
Kiherehere kilimponza huyooo!
 
Mkuu sio general. Mie by Pro.. ni Mechanical Eng, nina Bacheraol ya IT na nina PGD ya Electrical.. na ni certified Penetration Tester.. programing nilikuwa najua zaidi hata ya ma programer. Kwenye field ya Security nilikuwa nawalaza na ukija kwenye programing na kulaza.. sema now days nimeacha vyote niliona upumbavu nanufaisha watu
 
Huyo ameongelea General.. ila mie programing nilikuwa mwiba na security nilikuwa fimbo.. nili balance.. but tanzania ilinivunja moyo nimeacha kabisa.. haya makitu.. nalima tu sasw hivi
 
Ninapo ona comment kama hii humu na pata nguvu ya kuendelea kujifunza programming.
 
Huyo ameongelea General.. ila mie programing nilikuwa mwiba na security nilikuwa fimbo.. nili balance.. but tanzania ilinivunja moyo nimeacha kabisa.. haya makitu.. nalima tu sasw hivi
Mkuu unalima nini?
Ni vitu vya kusikitisha.

Kuna rafiki yangu wa karibu sana anaishi Marekani, yeye yupo upande wa IT huwa ananiambia kazi za field yako na yake yeye nje nje huko.
 
Ili uje kuajiriwa SENTERO uwe unafatilia IMEI ,IP na MAC Adress za watu?
 
Mkuu unalima nini?
Ni vitu vya kusikitisha.

Kuna rafiki yangu wa karibu sana anaishi Marekani, yeye yupo upande wa IT huwa ananiambia kazi za field yako na yake yeye nje nje huko.
Mahindi, viazi vitamu na vitunguu.
Kwa nje ni kweli wanalipa vizuri field za cyber security hata hapa tanzania kwa baadhi ya maeneo ila ni nadra kuyapata.. watu mnakuwa 20 position moja, inakuwa kama tani vile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…