Baba wa Manabii na Mitume wote Ibrahimu au Abrahamu alikuwa Dini gani?

Baba wa Manabii na Mitume wote Ibrahimu au Abrahamu alikuwa Dini gani?

Uislama,ukristo,uyahudi,ubudha,Hinduism hizi zote ni imani za watu wengine.
Waafrika fuateni imani za mababu zenu,achaneni na utahira wa kufuata imani za watu wengine, ndio maana mnakosa majibu maaana imani zenu ni za mapokeo.
 
Uislamu na ukristo zote ni imani za kitapeli
Uislamu ndio utapeli mkuu maana hadithi za ibrahimu , Yesu nk ukiacha za muhamad wao wamekuja kuziandika ilihali wenzao wayahudi, wakristo walishaziandika kwao, ndio maana ibrahimu amekuja kuwa muislam wakati wa ukristo na uyahudi kama aya yao hiyo ya quran
 
Uislamu ndio utapeli mkuu maana hadithi za ibrahimu , Yesu nk ukiacha za muhamad wao wamekuja kuziandika ilihali wenzao wayahudi, wakristo walishaziandika kwao, ndio maana ibrahimu amekuja kuwa muislam wakati wa ukristo na uyahudi kama aya yao hiyo ya quran
Utapeli ni ule mnaofanyiwa nyinyi kila mkienda huko kanisani kwa kumtajirisha mtu ety sadaka ya Mungu

Aisee ivi nyinyi akili zenu ziko wapi?
 
Sasa utakuwepo vipi wakati unamrefer mtu ambaye hakuwepo? Mbona mnakuwa wajinga sana nyie watu?
Sasa wote hatuja kuwepo , wewe unacho kataa kipi kuwa uislamu ulikuwepo toka mwanzo? wakati hata Yesu unae muamini pia hujamuona umehadithiwa tu kama wengine
 
Sasa mkuu kwani ushasikia wakristo wanasema ukristo umekuwepo kabla ya yesu?
Au ushasikia wanasema kina Musa na Ibrahim walikuwa wakristo?
Sasa wewe usichoelewa ni nini? Kwamba hujui kama Wakristo wanaamini kwamba imani ya Ibrahim kwa Mungu ndio imani ya Wakristo, wanaamini waliotangulia wote ilikuwa ni mpango wa Mungu kufikisha ujumbe kwa mwanadamu. Hata Waislam wanaposema Ibrahimu alikuwa Muislam ni kwasababu wanaamini ibrahimu alikuwa ni mwenye kuamini katika Mungu. Ukristo sio jina tu bali imani(kufuata yale yaliyoelekezwa)
 
Mkuu wakati huo hakukuwepo na Dini. Ila kilichokuepo ni Imani Aidha imani kwa Mungu au kwa Miungu.

Kwa hiyo wakati huo wa Ibrahimu dini haikuepo maana hata yeye kabla ya hapo hakujua Mungu ila alikua akienenda kwa haki na ndio maana Mungu akamtokea na akabarikiwa kwa sababu ya nini? HAKI NA IMANI.
Mungu alimtokea wapi?
 
Qurani ni janja janja tu, hivi huyo Ibrahimu Mwislamu wa kwenye Qurani ni mtoto wa nani ?
Yaani Baba wa huyo Ibrahimu anaitwa nani kwa mujibu wa Qurani ?

Kumtaja tu hakumaanishi ni Mhusika mwenyewe.
Babu yako wa Tano anaitwa nani?
 
Utapeli ni ule mnaofanyiwa nyinyi kila mkienda huko kanisani kwa kumtajirisha mtu ety sadaka ya Mungu

Aisee ivi nyinyi akili zenu ziko wapi?
Hivi kujengewa misikiti nayo unaona ni akili? Hao wanaojenga hizo pesa wanaokota? siyo sadaka zinazotolewa na waislamu wenye dini yao Uarabuni.
 
Wanasema ni dini iliyokamilika tangu imekuja lakini.

Mud ndio laleta nguzo 5 hivyo kabla kama ilikuwepo wakati wa Ibrahim zilikuwepo nguzo ngapi.

Sasa hivi wakokunasa ili ujiunge nao Wana shahada sijui ni ya sheria au ya udaktari wanakuambia utamke, Sasa kama hicho kitabu hakikuwepo na huyo mud hakuwepo hiyo shahada enzi hizo ilikuwa inatamkwaje au mshkaji aliichomekea ili awe anatakiwa tajwa?
Unahitaji elimu kidogo tu uelewe
 
Mimi kwa mtazamo wangu haijatajwa Nabii Ibrahimu (as) ana dini gani, kilichotajwa ndani ya Qur'an ni kwamba Nabii Ibrahimu alikuwa mnyenyekevu/aliyejitupa kwa Allah na hii unaweza kupata katika Qur'an 2:127-128, ambapo amemuomba Allah amfanye awe mnyenyekevu, neno unyenyekevu ndio "Islam" na mtu mnyenyekevu anaitwa "muslim" kwa kiarabu, hivyo popote nabii Ibrahimu anapotajwa ndani ya Qur'an kwa jina la la "Muslim" maana yake ni hiyo kwamba yeye ni mnyenyekevu na hata manabii wote wanabeba sifa hiyo ya kuitwa "Muslimina" yaani wanyenyekevu mbele ya Allah.

Kitu kinacho wachanganya watu ni kuona manabii wameitwa Muslimina na hivyo kusema kwamba wao ni Waisilamu waliofuata dini ya Kiisilamu dini hii iliyoanzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw)-- kitu ambacho sio sahihi kwani Dini hii ya kiisilamu imejengwa katika nguzo 5 na nguzo ya kwanza (shahadatein) ambayo ili uwe muisilamu lazima uitamke katika kila swala (katika kikao cha attahiyyatu) nk, je kama nabii Ibrahimu alikuwa mfuasi wa dini hii (hata kabla haijaanzishwa) alikuwa akitoa hii shahada hii?? je alifunga swaumu hii ya Ramafhani??, kuna maswali mengi kwa wale wanaoshindwa kujua Nabii Ibrahimu anapoitwa Muslim ina maana gani!!.

Hivyo nabi Ibrahimu (as) ni Muslim kwa maana ya unyenyekevu na sio Muslim kwa maana kwamba yeye ni mfuasi wa dini hii ya Kiisilamu dini iliyoanzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw) ambayo imejengwa katika nguzo tano, na manabii wote wameitwa Muslim kwa maana hiyo ya kuwa wao ni wanyenyekevu mbele ya Allah.
Naona unapambana kufa kupona ili tu Ibrahim asiwe muislam
 
Naona unapambana kufa kupona ili tu Ibrahim asiwe muislam


Hizo ni shutuma nzito dhidi yangu.

Wapi Nimesema Ibrahimu hakuwa Muisilamu??, Qur'an inasema yeye ni alikuwa Muisilamu sasa kwanini nipinge??!!.

Ninachosema mimi Ibrahimu hakuwa mfuasi wa Mtukufu mtume (saw) hivyo hakuwa anatekekeza nguzo 5 za Uisilamu huu wa Mtume (saw) kwani Uisilamu huu licha ya mtu kuwa mnyenyekevu kwa Allah ni lazima ufuate na kutii nguzo 5 na hapo ndipo unakuwa Muisilamu mfuasi wa mtume (saw).

Sasa kwanini Allah kamwita Ibrahim Muisilamu??, kamuita Muisilamu kwa maana ya UNYENYEKEVU/KUJITUPA kwa Allah na manabii wote wameitwa Waisilamu kwa maana hiyo tu kwamba Wao walikuwa Wanyenyekevu waliojitupa na kujisalimisha kwa dhati kubwa mbele ya Allah, hiyo ndio maana ya neno Islamu kwa hao manabii wengine.

Watu wanashindwa kueleza jambo hilo na ndio maana Wakristo wanashangaa na kuuliza inakuaje ibrahim (as) awe Muisilamu wakati dini ya kiisilamu imekuja karibu miaka 5000 baada ya nabii Ibrahim (as)??, wanahitaji majibu yanayoingia akilini.
 
Kuna umuhimu gani wa kujua ni mtoto wa nani kwa mujibu wa Quran!?..hata Muhammad haikusema ni mtoto wa nani...uwe unatoa hoja za maana
Sasa tutajuaje ni Ibrahimu mtoto wa Tera ?
Baba wa Muhammadi kaandikwa kwenye hadithi za Mtume Muhammadi au husomi kijana ?
 
Back
Top Bottom