Baba wa watoto wangu watatu (kila mmoja na babake) wote wanataka kufunga ndoa na mimi

Baba wa watoto wangu watatu (kila mmoja na babake) wote wanataka kufunga ndoa na mimi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mtoto wa kwanza nilimzaa na class mate wangu. Wakati huo wote tukiwa hatuna ajira. Wazazi wote walitusaidia. Ikifika wakati kaka yake alimuita Gabon akamsaidie biashara. Aliniacha na mtoto wa miaka miwili. Tulipoteza mawasiliano.

Mtoto wa pili nilimzaa na aliyekuwa boss wangu. Alikuwa msaada mkubwa kwangu. Alisaidia hata ada ya shule ya mtoto mkubwa. Huyu bwana alipata matatizo kazini na alifungwa.

Mtoto wa tatu nimemzaa na jirani yangu. Huyu kaka ndiyo kwanza alikuwa amehamia mkoa huu. Mimi nikiwa mtu wa karibu nilimsikiliza chakula na kumfahamisha mji. Nilipopata ujauzito aliamua kunifahamisha kwa ndugu zake.

Baba Tatu anataka kunioa na mipango ya mahari imekamilika. Baba Mosi na baba Pili wote wamerudi na kila mtu anataka kuanzisha familia na mimi.
 
Hakuna haja ya ndoa, vunja mifupa angali meno bado ipo.
 
Ndio maana huwa unahasira na chichiem kumbe mambo yameanzia mbali hivi..😂😅
 
Usikilize moyo wako unakutuma wapi ila usisahau pesa pia ndo kila kitu
 
Haiwezekani uwe na upendo sawa kwa wote, angalia pale moyo umelala zaidi bt kama unawaonea huruma wote kisa umezaa nao basi ndoa ya threesome ihusike nadhani nimekushauri vyema sana kuliko wananchi wote
 
Back
Top Bottom