Bado najiuliza: Nini hasa chanzo cha Lowassa kuwa na ushawishi kwa watu?

Kwenye pesa hapo si kweli, wangapi walijua kua mzee ana ukwasi??

Kilichompa kiki ni ile kujivua gamba, akaonesha weredi pale, akaja kupata booster kwenye chama chake kwenye ule uchaguzi, ni nani alikua mkubwa zaidi yale pale.??

Chadema nao wakaja kumpaisha zaidi.
Japo pesa zilihusika ila kua na pesa hakukupi ushawishi direct.
 
Nilisoma naye Arusha Secondary School akinitangulia miaka miwili, niseme tuu sisi tuliotokea Arusha mjini tulizidiwa na Masai toka Monduli akawa Parade band leader, Head Prefect na best Basketballer
Alikuwa na nyota na haiba ya kupendwa.
Shkamoo mzee. Hivi nasikia wakati sheikh Amri Abeid stadium inajengwa wanafunzi walikuwa wanapigishwa kazi. Unaweza tupa stori kidogo?
 
Pengine Mimi sijakuelewa. Unahoji nguvu ya mtu ambae katumikia nyazifa mbalimbali za juu zinazo muunganisha na watu moja kwa moja katika maisha yao.
Hiyo ni kawaida kabisa kwa mjibu wq nyazifa mhimu alizozipitia

Mkuu, nafikiri hujui ushawishi wa Lowasa kwenye hii nchi.
Hizo nafasi wapo waliozitumikia tena wengine mpaka kuwa Marais lakini hawana huo ushawishi.
 
Marehemu alikua mtu wa misimamo.

Watu wanakuheshimu automatically kama una tabia ya kujisimamia.

Anyway, hadi leo ile picha ya wengi wa wana-ccm wakiimba "Tuna imani na Lowassa" kwenye mkutano wa NEC 2015 kpnd cha mchujo haijanitoka akilini.

R.I.P Lowassa
 
Anhaa
A
Ngoja wajuvi wa mambo waje.
 

Tukio lile lilikuwa la kusisimua.
Wengine tulifikiri mchezo ulikuwa umeishia pale lakini kilichotokea Mungu kweli ndiye mpangaji
 
Ni pesa tu huyu mzee alijua kuzitega pesa na zikategeka..
yeye ndio amesababisha ccm kutumia matajiri kwenye siasa huko nyuma haikuwa hivyo kabisa sasa mzee EL alikuwa very strategic aliweza kuwashawishi best businessman wa hii nchi wansapport yy na kundi lke ndani ya ccm.

Ndio maana wanaccm walimuona kichwa maan pesa zilimiminika vibaya mno kupitia kwa lowasa. Aliwasaidia wanasiasa wengi sana kwenye kampeni zao pesa alikuwa akiwapa yeye malipo ilikuwa ni kumsuport yeye na genge lake na wewe automatuc unakuwa genge lake.

Kusema na ukweli mwaka 2015 ccm ndio ilikuwa mwisho kutawala hii nchi ni bahati mbaya sana huyu mzee alihamia upinzani ungali dhaifu sanaa nchini..uwezi kuachia dola kwa upinzani dhaifu km kina lisu , mbowe na the like utabomoa nchi iliyojengwa kwa shida kwa miaka ndani ya muda mfupi tu.
 
💰 💴 💵 hela, fedha, ukwasi, etc. Alihakikisha anasemwa vizuri. Ila hapa wazee koti zile za rangi ya muafrica nawakubali, si unaona walivyogeuza na kumfanya Dkt Samia aonekane anaweza kushinda uchaguzi hahahaha yaani Makonda hakika kaupiga mwingi
 
Pesa ni sabuni ya roho.
 
Umenena vema
 
Licha ya kuwa mwanasiasa mkubwa tu enzi zake, pia alikuwa bonge la don, mtu mwenye mishe nyingi na fedha za kutosha. Umaarufu wa Lowassa vilevile upo zaidi Arusha. Pale anabiashara nyingi na pia ni Laigwanani katika kabila la Wamasai, mtu mkubwa zaidi kwa Wamasai. Nadhani Wamasai watalia sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…