Bado najiuliza: Nini hasa chanzo cha Lowassa kuwa na ushawishi kwa watu?

Bado najiuliza: Nini hasa chanzo cha Lowassa kuwa na ushawishi kwa watu?

Nimeishia kusoma uliposema JPM mchapakazi. Umechanganya propaganda na chapakazi
Kama hujaona hata chembe ya uchapakazi wa JPM pamoja na kwamba naye alikuwa na mapungufu yake na nahitimisha kwa kusema "CHUKI HUMUUA MTU MPUMBAVU".
 
Hakuna cha uchawi,nyota, ushawishi wala nini, bali [emoji117]kipindi lowasa anagombea urais nchi ilikuwa imetoka ktk uongozi wa hovyo(CCM) ambao wanachi walishauchoka, hivyo kuamua liwalo na liwe bora kumchagua yeyote ambaye yuko kinyume na uongozi wa CCM.

Karibu kila mtu kipindi hicho alikuwa kinyume na utawala wa kikwete pamoja uongozi wake, kuchokwa kwa utawala huo ndio jambo lililofanya wengi wahamie upande wa kusapoti upinzani, the same way kama ilivyokuwa 2010 kwa Dr Slaa alivyopita na nyomi la wafuasi wengi waliochoshwa na utawala wa CCM, hapo hakuna cha uchawi,dawa wala mvuto bali uhalisia wa maisha unaowafanya watu kuchoshwa na aina ya mfumo na kuamua kuhamia/kutamani mfumo wa upande wa pili(upinzani).

Ndiomaana baada ya lowasa kushindwa, matumaini ya walioupinga mfumo wa ccm yalirudi baada ya kuona kumbe kuna matumaini hata huko CCM pale Magufuri alipobadili mfumo mzima wa kipuuzi huko CCM, hapo ndipo hata baadhi ya wapinzani walianza kumsapoti na hata wale waliokuwa wamechoshwa na utawala wa CCM kabla ya 2015 walirudisha matumaini.

Sio hadithi, sio stories, haya mliyashuhudia wenyewe baada ya magufuri kuapishwa tu alipoanza ziara za kushitukiza, kutumbua wazembe/wala rushwa, kuinua maisha ya walala hoi, kupambana na wakwepa kodi, haya aliyafanya ndani ya muda mfupi jambo lililorudisha matumaini kwa Watanzania.

Suala la Lowasa kuwa na wafuasi wengi lilitokana na Raia kuchoshwa na utawala wa kihuni wa CCM ndiomaana wakatamani na kushawishika na upande wa Upinzan wakifikili kutakuwa na unafuu au kutaman Uongozi mpya nje ya CCM.

Simple hakuna uchawi hapo ni suala tu la mifumo kupoteza direction.

Hata wewe hapo leo hii ukipata pesa hata kama ni domo zege utashangaa sana utakavyokuwa chambo/asali ya warembo na utajiuliza haya mambo kwanini hayakuwepo kipindi hauna hela? Jibu ni kuwa watu wanafuata kitu ambacho ni bora, kitu ambacho kwa wengine hakipo.
Alikuwa na ushawishi zaidi alivyokuwa CCM kuliko upinzani 2015 ndio mara ya Kwanza mgombea wa CCM analalamika kuwa Kuna watu mchana ni CCM usiku ni chadema
 
Kama hujaona hata chembe ya uchapakazi wa JPM pamoja na kwamba naye alikuwa na mapungufu yake na nahitimisha kwa kusema "CHUKI HUMUUA MTU MPUMBAVU".
Wapi imezungumzwa chembe ya uchapakazi? Anzisha uzi wa chembe ili nikuunge mkono. Tofautisha mchapakazi na mwenye chembe ya uchapakazim
 
MONEY + POWER + RESPECT jamaa anavyo vyote hivyo

Edward Lowasa pesa anayo, power ( Chi power - nguvu ya ndani kabisa), pia na anaheshimika.

Mfanano wa kaliba ya Edward Lowasa ni sawa na wa Edward Moringe Sokoine, ingwa Sokoine hakuwa na ukwasi mwingi kama wa Lowasa ila alikuwa na Power.

Wanasiasa wengine ni masikini wenye vipato na uhakika wa pesa kupitia madaraka yao, hawana nguvu ya ndani ila nguvu ya soda/nguvu ya dola pia hawana heshima katika jamii bali wanaogopeka kupitia mamlaka yao.
 
Anhaa!
Unajua tangu nipate akili sidhani kama kuna mwanasiasa tangu nchi ipate uhuru alikuwa na ushawishi kama Lowasa.
Wengi wanakuwa na ushawishi wakiwa ndani ya mfumo iwe wa ccm au serikali. Wakitoka wanakwama
Mmh kwamba alimzidi hata Nyerere kiushawishi?unajua Nyerere alikuwa na uwezo wa kumkosoa aliyeko madarakani na akafyata?
 
Nyerere bila Tanu na CCM hana nguvu hiyo.
Uwezo wake wa kukosoa ulitokana na kuwa yeye ndiye Baba wa taifa
Baba wa taifa ni cheo cha mdomoni tu,kile ni kipawa ambacho mtu anakuwa nacho kwani wengine hawakutokea tanu na ccm?Lowasa huwezi mfananisha na Nyerere labda na akina makamba,Jk ...Yule alikuwa na hamasa hadi nje ya mipaka ya Tanzania.
 
Mimi nilikuwepo wakati wa kampeni za 1995

Augustiono E. Mrema hakufikia alichofanya E. Lowassa kwasababu Lowassa alikuwa sababu ya vijana wengi sana kupata ubunge na power...Mrema hakufanya hivyo
Nazungumzia ushindani kwenye nafasi ya urais .
 
Watanzania ni wepesi wa kupumbazika sana na kujisahau haraka, maovu ya Lowassa si hata ya kusameheka, itafaa zaidi kama alitubia dhambi zake kabla hajalimwaga kwenda kwa Baba mwenye makazi yake ya Mtakuja paradise. Tusiogope kusema ukweli Lowassa aliumiza wengi kwa udhulumati, uporaji na umafia. Mwaka 2004 na 2005 alishiriki kikamilifu kumchafua ndugu Salim Ahmed Salim acha aende ndio imeisha hio.

Umaarufu wa Lowassa ni yeye kuwa fisadi na kuunda kundi la kuchafua watu nyakati za siasa hasa kuelekea chaguzi ndani ya chama. Kwa miaka mingi alituhumiwa kuihujumu Chadema na vyama vya upinzani chaguzi za Mkoa wa Arusha.

Kila baya litalipwa hapa hapa duniani, haishangazi ndiomana amepata mateso lipizi ya kuugua muda mrefu. Mungu ameamua acha inyeshe tuendelee kuona kuvuja kwa jumba.

Imeisha hio hainaga unafiki

Wadiz
 
Huna ushahidi ulioweka hapa....
Ndio maana tutakuita muongo tu.
 
Watu wote wamehuzunishwa na kifo cha Mh. Edward. Ila kuna mtu mmoja wa misiba yani anapendaga kuwa mbele kwenye misiba ila katika msiba huu hadi sasa ni kimiaa
 
Watu wote wamehuzunishwa na kifo cha Mh. Edward. Ila kuna mtu mmoja wa misiba yani anapendaga kuwa mbele kwenye misiba ila katika msiba huu hadi sasa ni kimiaa
Ni kawaida tu.kukosana kupo..kutozikana kupo mpaka kwenye ngaz ya family ndugu wa damu kabisaa..Atajitokeza tu ,uzur JK hakosagi cha kusema. Atawashangaza
 
Kuna watu huwa hawaongei ongei ila akili zao kwenye mipango na mikakati huwa hazifichiki. Ishu ya maji kanda ya ziwa..idea ya shule za kata... hayo angalau watanzania wanayajua lakin wala hakua anapiga piga kelele.
 
Watanzania ni wepesi wa kupumbazika sana na kujisahau haraka, maovu ya Lowassa si hata ya kusameheka, itafaa zaidi kama alitubia dhambi zake kabla hajalimwaga kwenda kwa Baba mwenye makazi yake ya Mtakuja paradise. Tusiogope kusema ukweli Lowassa aliumiza wengi kwa udhulumati, uporaji na umafia. Mwaka 2004 na 2005 alishiriki kikamilifu kumchafua ndugu Salim Ahmed Salim acha aende ndio imeisha hio.

Umaarufu wa Lowassa ni yeye kuwa fisadi na kuunda kundi la kuchafua watu nyakati za siasa hasa kuelekea chaguzi ndani ya chama. Kwa miaka mingi alituhumiwa kuihujumu Chadema na vyama vya upinzani chaguzi za Mkoa wa Arusha.

Kila baya litalipwa hapa hapa duniani, haishangazi ndiomana amepata mateso lipizi ya kuugua muda mrefu. Mungu ameamua acha inyeshe tuendelee kuona kuvuja kwa jumba.

Imeisha hio hainaga unafiki

Wadiz
we jamaa acha unafiki, kuna mwanasiasa gani asiye mchafu wa kuchafua wenzake, mbona hushangai wanaomsifia sasa akiwa kalala umauti
 
Mbona kama unakuwa mnafiki, ina maana hujui siasa za maji taka za makundi ya wawania urais ndani ya ccm kila unapokuja uchaguzi mkuu? Usijitoe ufahamu, hata lowassa mwenyewe ni muhanga na muathirika wa siasa za makundi ya wawania urais ndani ya ccm. Unamuona lowassa tu kuwa alikuwa mmafia, kwani huwaoni mafia wengine waliofanya siasa za kimafia kukwamisha wenzao kuupata urais ndani ya chama chao? Achana na siasa za majitaka walizofanyiana makundi ya wawania urais ndani ya ccm huo ni mtindo wao wa kuchezeana rafu wenyewe kwa wenyewe na mwisho huelewana na kuwa kitu kimoja tena mshindi anapopatikana
 
Nilisoma naye Arusha Secondary School akinitangulia miaka miwili, niseme tuu sisi tuliotokea Arusha mjini tulizidiwa na Masai toka Monduli akawa Parade band leader, Head Prefect na best Basketballer
Alikuwa na nyota na haiba ya kupendwa.
Hivi Lowassa ni masai !.Lowassa ni mmeru aliyehamia Monduli wanakoishi jamii ya wamasai.
 
Back
Top Bottom