Bajaji aliyoacha marehemu mama imeanza kunigombanisha na baba yangu mzazi pamoja na dada yangu tumbo moja nifanyeje?

Bajaji aliyoacha marehemu mama imeanza kunigombanisha na baba yangu mzazi pamoja na dada yangu tumbo moja nifanyeje?

Tafuta chako Mali ya familia haifai. Epuka sana neno chetu tafuta chako sio chetu
Na akija kushtuka atakuwa kashachelewa, mi nina dada zangu nimewaacha wanachukua kodi miaka yote ila mpaka leo hakuna cha maana wamefanya, cha zaidi wanataka mimi ndo nikarabati nyumba tena!
 
Bajaji ni mali ya Mzee, muache afaidike nayo.
La sivyo, ungeinunua kama ilivyo na kuitengeneza au mngeingia mkataba kabla ya kuitengeneza.
Anafaidika nayo vipi ikiwa juu ya mawe?
 
Na akija kushtuka atakuwa kashachelewa, mi nina dada zangu nimewaacha wanachukua kodi miaka yote ila mpaka leo hakuna cha maana wamefanya, cha zaidi wanataka mimi ndo nikarabati nyumba tena!
Hatari sana Mimi mzee aliniambia nijenge Kiwanja Cha home aisee nilikaa nikafikiria nikasema huu ujinga najengaje nyumba ya familia yangu kwenye Kiwanja Cha mzee nikaona Bora nikaingie gharama ya kununua Kiwanja hata kikiwa kidogo vipi ilimradi kiwe changu na nijenge kwenye ardhi yangu ogopa sana neno chetu yaani mzee akishazeeka sana Hana pa kushika hata hiyo nyumba uliyojenga anaiona kama yake
 
Babako na dadakoo chuma ukete haooo wanataka ubaki masikni

ukiona awaeleki ondoka na spare moja baada ya nyingjnr
 
Babako na dadakoo chuma ukete haooo wanataka ubaki masikni

ukiona awaeleki ondoka na spare moja baada ya nyingjnr
Mjomba jitahidi siku Moja Moja uandike vizuri aisee yaani unaandika kama bata kaharisha
 
Heshima yenu! Wanajamii Jf!

Ushauri kwa kijana wenu Nina miaka 24 tu na ndio nimemaliza Chuo miezi miwili Sasa!

Katika harakati za kuona nisikae kinyonge Daslamu niliamua kurudi nyumbani bwana! Geita
Basi dada yangu akawa amenipa 260000/=, nilimwambia nitafanya biashara ya kutembeza mayai kwa wauza chips, migawahani, masokoni na kwenye maduka ya hommie accessories

(Yani laki moja kama mtaji wa trei 11 za mayai pamoja na 160k wa ajili ya kununua baiskeli ya kufanyia delivery)

Sikununua Ile baiskeli moja kwa moja nikapata wazo nyumbani kuna BAjAj nikitengeneza nawaza ikapiga kazi inaweza rudisha hela na nikawa na mtaji mkubwa plus kupunguza kuchelewesha delivery

Nikainunulia betri N50 pamoja na ufundi laki Ile hela ya mtaji wa mayii ikaisha.
BAJAj Ile imekaa miaka 10 ni aina RE toleo A la 2012 Ila imepaki toka Niko form one 2014-2024 nimepita vidato vyote hadi Chuo nimemaliza imepaki Ata mama kafariki mwaka Jana kaiacha.

Bajaji hii ilkua ni zawadi ambayo mama alipewa kama zawadi sababu ya kuwa muwekaji wa pesa mzuri katika Benk mojawapo! Giant aliitunza miaka kumi kwa ajili yangu!
Basi mimi niliitoa na kumkabidhi dereva bajaji mzoefu awe analeta kiasi cha 20k Kila siku huku namm najifunza Kila siku vifaa vyote vilvyo kwenye engine il nijue kipi kizima kipi kibovu sababu imekaa 10 years

Baba alinipinga sana nisitoe bajaji sababu hawaamini mafundi na Sina experience ya bajaji (baba yangu huwa hanisapoti kwa jambo lolote la mafanikio yangu)

Dada yangu nae akaja kunipinga kwanini nimetoa bajaji kwa mtu Bila kumshirikisha
(mimi siku taka kumshirikisha sababu yeye ni muoga wa kutake risk) Ila Sasa kashagundua amenipiga stop nisiguse chochote.

mimi niliitoa bajaji kwa kudhumuni la kupata mtaji na kusave kwa ajili ya kusaidiana na dada kukarabati nyumba za marehemu mama maana baba Hana msaada kwetu!,

Ila dada yangu amenizuia nisishike bajaji! Nimekaa nimetafakari nawaza kuondoka nyumbani. Niache Kila kitu nikatafte vyangu?? Ila ROHO inaniuma nyumbani kuna nyumba za kurekebisha zimechakaa dada yangu hawezi peke ake?,, je nikiondoka nikaamuachia majukumu yote nitakuwa sahihi?? Na kinachoniudhi nikuwa mimi naamini katika biashara za usafiri kama tax, Bajaj Ila ye haamini amenizuia lakini Nina malengo mazuri!

Nifanyeje nitelekeze nyumba nirudi dsm!! Au nibaki hommie!??
Uandishi tu unaonyesha hiki ni kisa cha kutunga.
 
Back
Top Bottom