Ilishawah kunitokea baadhi yao wana tabia za hovyo.hiyo ishawahi mkuta mtu wangu wa karibu ana walikua wote wadada muweka hela na mpokeaji (teller) kapewa anasema hela haijakamilika dada kamwambia hizo hela zimehakikiwa na watu zaidi ya wawili.
Teller anabisha akaambiwa angalia huko chini na mtu akaangalia akaikuta akasema eti hakuiona wakati inadondoka anaomba samahani.
Mzazi/Mtu yeyote anaweza kuja kuhisi mtu wake wa karibu kamuibia kumbe kaibiwa huko huko BANK,Msala wanapata waliongia ofisini/nyumba/na wa kwanza kufungua SAFE..hao watu majumba mabovu huwaangukia bila sababu za msingi.Ilishawah kunitokea baadhi yao wana tabia za hovyo.
na Muda wa kuhesabu nao uwe nao,inakua na maana gani sasa hela zinatoka BANK uhesabu.Bulk withdrawal unatakiwa kuingia ndani ili upate space ya kuhesabu kwa nafasi...
BANK wana mashine za kuhesabia,wanawalipa watu wana vitendea kazi vyote vya kuhakiki namba.Bulk withdrawal unatakiwa kuingia ndani ili upate space ya kuhesabu kwa nafasi...
Laki ya buku 🤣🤣🤣
Wewe unataka milioni ya buku kwa matumizi gani?View attachment 2839574
Hiyo sio nyingi mkuu ni kakutembea nacho mfukoni tu hako.
na shida sio kutembea nayo,shida ni uhesabu chenchi Milioni ya Buku.
Vibunda Kumi vyote uvihakiki,umalizane hapo uingie kwenye noti za buku mbili,uje buku 5 umalizie kuhakiki za ten ten.
Hapo ni BANK A unasafari ingine kwenda BANK B na C nk... hivi utahesabu hizo hela kila siku kwa ratiba hiyo?
Atm kutoa laki 4 Mpaka itimie lengo mkuu kibarua chake si haba.
na tunaenda ndani wakat mwingine kwa ajili ya chenchi unatoa 6m unamwambia akupe buku za 500k na 2000 za 500k then 1m akupe 5000 tu, hizo burungutu unazopewa mkuu kusema uzihesabu Njaaa inauma hapo hapo.
Na wafanyaniashara wakubwa sio wa viburungutu vya mil 5,10 hapo.sio rahisi hivyo mkuu kama walivyoandika,Kumbuka Pale kwa teller hamna kiti useme ukae uhesabu, Umesimama nusu saa kwenye foleni zamu yako inafika usimame tena uanze hesabu maburungutu ya noti zilizoshikana kazi yake si haba mzeee.
Atleast kuna Tawi CRDB wamefungua kwa ajili ya WAFANYABIASHARA wakubwa humu ndani hamna kusimama mnakaa chini kwenye SOFA mnakula kipupwe.👇👇
View attachment 2838961
Atleast Bank zote zingekua matawi yao ndani yako hivi mnakaa mtu ungepata Nguvu ya kwenda hesabu hela pale dirishani.
ila haya matawi Mengine unayowahi siti ya kusimama unaweka kabisa NAMBA unamwambia wa mbele ako "NIPO NYUMA YAKO"
Kuhesabu hela yataka Moyo Boss,Hamna kazi ngumu kama hiyo naikimbiaga mimi.
Kuna teller mmoja aliniibia alafu namjua nakumbuka nilienda kama million sita hivi,Nimekua ni mtu wa kuchukua Pesa mara kwa mara Bank na mara nyingi ni mtu ambae sikuaga na utaratibu wa Kuhesabu Pesa ninazo pewa toka BANK.
Lakini niwahakikishie wale ma teller either ni wao au mtu anaewapa yale maburungutu anakua anapiga hela.
Mara nyingi nikitoa Salio la maburungutu huwa unachukua yakiwa kwenye rubber band unapewa unatia kwenye BAG unasepa.
Kutokana na wingi wake huwezi kuhesabu hizo pesa mara zote huo ndio ukweli.
Haya maburungutu yapo aina mbili kuna yale ya NOTI mpya zinazokua na ki karatasi kushika noti zote (hizo hazina shida)
Kuna Hizi Burungutu ambazo noti zake ni Used unakuta zipo tayari counter pale kwa ajili ya kupewa wateja
[emoji116][emoji116][emoji116]
View attachment 2838836
Hizi burungutu Ndugu zanguni nawambia Ukweli nimejiridhisha kwa asilimia 100 na zaidi kwamba haya maburungutu huwa hayatimiii.
Si yote ila nakuhakikishia Ambae anabisha naomba afanye utafiti wake kisha arudi kunipa mrejesho.
Nimekua na kawaida sana ya kwenda Kuomba chenchi ninapokua nimeishiwa kwenye ofisi zangu.
Kwahyo unaweza PEWA burungutu la 2000,1000 na 5000. Mara nyingi kama mjuavyo biashara si muda wote wateja wapo.
Kuna nyakati wateja hamna mnakaa mnatizamana, Nikaona nijipe kazi ya kupanga Zile Noti za bank kwenye mafungu ya laki (noti za 5000) na 10k kwa (noti za buku na buku mbili)
Nikawa nahesabu hesabu hesabu, mara nyingi nakutaga upungufu kwenye noti za 2000 na 1000 ndio zinapochomolewa pesa.
Kila nikihesabu ni lazima kuna mafungu ntayakuta yamemiss 2000 na kwenye buku inamiss Buku.
Hawachomoi nyingi yani laki ya buku wanatoa buku na Laki ya 2000 wanatoa 2000.
Huwezi shtuka haraka utahisi umejichanganya, kilichonfanya nishtuke ni baada ya kuingia na hela kwenye chumba kisicho na pesa kabisa na begi langu nikamwaga pesa mezani kuhesabu.
Sikuamini nilihisi mazingaombwe kweli hela zimemiss.
Nikiumganisha DOTS nikapata majibu kumbe hawa watu hizi ndio tabia zao.
Unaweza jiuliza Teller anapataje marupurupu ila kumbe njia yao ni hiyo.
Wewe unae waamini BANK kwa kutohesabu pesa wanazokupa ipo siku utapga watoto wako wafanyakazi wako ukisema wamekuibia ila Nakwambia Leo hiii BANK ni WEZI mtapga watu wenu wa karibu mtawahisi na kuwafikiria vibaya lakini ukweli ni kwamba BANK kuna wezi wa kimya kimya.
Kama unaaamini hela bank hawaibi endelea.
Nimemaliza.
Afu kwanini ukiwaambia issue ya tuangalie camera hawataki.....wanasolve kimyakimya,kwnini?Kweli kabisa kuna siku nimetoka kadoo bureau de change, hela imehesibiwa vizuri nakuwa makini kabisa, nimefika holland hse yule bitch ananimbia imepungua 60k aisee nilimuwashia moto, nikaomba tuangalie camera manager akamuita yule malaya pembeni, nikaambiwa hili litashughulikiwa internally waka deposit mchongo wangu
kibali cha kuview footprints za camera za bank ruhusa yake mpaka ifike kwa mwenye CRDB yani🤣🤣😅🤣Afu kwanini ukiwaambia issue ya tuangalie camera hawataki.....wanasolve kimyakimya,kwnini?
Kuna teller aliniambia pesa yangu imepungua 540,000....nilistuka sanaa,nkapiga hesabu zangu nikasema hapana tatizo lipo kwa teller....nkaongea na manager tuangalie kwenye camera,nikaambiwa niwape muda jioni watalishughulikia nikawa mpole,jioni nikapigiwa simu nikachukue pesa yangu.
Wapo mateller waaminifu na wengne sio waaminifu...ila kwenye pesa usimwamini mtu.
nimeianza hiii kitu saivi naonekana mnoko kinoma wakiniona tu unaona kabisa body language imebadlikaMimi huwa sizipokei mpaka teller azipitishe kwenye mashine ya kuhesabu huko naona! Tena huwa natamka wazi naomba uzipitishe kwenye mashine nione.