Barabara ya Morocco - Mwenge imetanuliwa ila njia zimepungua toka 5 hadi 4

Barabara ya Morocco - Mwenge imetanuliwa ila njia zimepungua toka 5 hadi 4

Njia Morocco - Mwenge ilitanuliwa na kua na njia nne kwa kigezeo cha kutumika kwa pesa za Uhuru, hiyo unayosema ni njia ya tano haikua njia bali ni utenganisho wa njia hizo mbili, ni sawa na kutoka palm beach kwenda uhuru heights useme ni njia tano, hapana utakua unakosea
Baada ya hii barabara kutanuliwa na kua na njia nne hakukua na service road pembeni wala mitaro mikubwa ya maji, kama unakumbuka.
Phase 3 ambayo ndio sasa inatanuliwa kuwekwa mitaro mikubwa ya maji, njia za waenda kwa miguu, taa za barabarani pamoja na service road na katikati kuacha eneo kwaajili ya BRT phase 4.

Mwendazake alisema hiyo njia imetengenezwa na hela za uhuru lakini nijuavyo hiyo njia kwanzia Tegeta mpaka posta hua chini ya Japana kwa matengenezo na upanuzi



View attachment 1774237
View attachment 1774238

Nimeweka na picha kuonesha kua zilikua barabara nne, mbili zinapanda mbili zinashuka. Katikati haikua barabara rasmi ya kutumika
 
Njia Morocco - Mwenge ilitanuliwa na kua na njia nne kwa kigezeo cha kutumika kwa pesa za Uhuru, hiyo unayosema ni njia ya tano haikua njia bali ni utenganisho wa njia hizo mbili, ni sawa na kutoka palm beach kwenda uhuru heights useme ni njia tano, hapana utakua unakosea...
1.) Unaposema haikuwa njia wakati iliwekwa lami na gari zilikuwa zinapita, tena hasa wakati wa Rush hour ilipunguza msongamano, nami nitakuuliza, njia maana yake ni nini?

2.)Je, goals za mradi zilikuwa ni nini hasa? Kama mitaro ya maji na service road zilikuwepo, labda useme service road haikuwa na lami, lakini je? Mabilioni yote yaliyotumika kufumua barabara ya njia 5 na kuweka njia 4, tena barabara ambayo ilikuwa ni mpya kabisa iliyojengwa kwa pesa za uhuru, ilikuwa ni ili tu tuweke lami njia ya waenda kwa miguu pembeni na kutanua mitaro ya maji?, halafu BRT tena ikija miaka ijayo ianze kufumua fumua baadhi ya vipande vya hii barabara tena?

Na wakati huo huo tumerudi nyuma kutoka njia 5 hadi njia 4?! Kwanini tusingeendelea kufaidi flow ya magari kwa njia 5 wakati tukisubiri mradi wa mwendo kasi ujengwe kwa mara moja na hizo pesa zikatumike sehemu nyingine yenye uhitaji? Mtu anaekupa msaada wa kukuvunjia nyumba toka vyumba vi5 hadi vi4 ni anakusaidia au anakurudisha nyuma?

3.) kwahiyo BRT siku ikianza tutegemee tena dhahama ya kufungwa kwa barabara na kuchimbuliwa chimbuliwa ili kuhuisha miundo mbinu ya vituo vya BRT, Junction zake na barabara, ni akili ya wapi hii jamani?
 
1.) Unaposema haikuwa njia wakati iliwekwa lami na gari zilikuwa zinapita, tena hasa wakati wa Rush hour ilipunguza msongamano, nami nitakuuliza, njia maana yake ni nini?...
Je, kutoka palm Beach kwenda posta inahesabika ni njia nne au tano?

Kwa wakati ule walitanua barabara na haikua na kiwango kama wanachojenga hivi sasa, miuondombinu wanayoongeza hivi sasa haikua kama mwanzo, naona lengo lako ni kubisha na kutotaka kuelewa barabara iliotanuliwa leo ikija kufumiliwa na kujengwa upya kwa miaka mitano badae ni jambo la kawaida sana,
 
Je kutoka palm Beach kwenda posta inahesabika ni njia nne au tano?
Kwa wakati ule walitanua barabara na haikua na kiwango kama wanachojenga hivi sasa, miuondombinu wanayoongeza hivi sasa haikua kama mwanzo, naona lengo lako ni kubisha na kutotaka kuelewa barabara iliotanuliwa leo ikija kufumiliwa na kujengwa upya kwa miaka mitano badae ni jambo la kawaida sana,
1.)Hiyo njia siifahamu, ila nieleweshe kwa hii ninayo ifahamu na nimeitumia sana tena kwa manufaa makubwa, ambayo wewe unasema haikuwa njia. Ilikuwa na lami na gari zilipita na ilipunguza sana msongamano wakati wa rushhour, sasa je nauliza, njia ni nini? Maana nisije nikawa nabishana kwa Kichina kumbe mtu anaongea kiJapan.

2.) Hapo uliposema kujenga barabara ya mabilioni ili uje ufumue baada ya miaka mitano ni jambo la kawaida, ndio nimeanza kupata shaka juu ya utimamu kichwani kwako.
 
1.) Unaposema haikuwa njia wakati iliwekwa lami na gari zilikuwa zinapita, tena hasa wakati wa Rush hour ilipunguza msongamano, nami nitakuuliza, njia maana yake ni nini?...
Nadhani ni rahisi kuufikiria kinachojengwa sasa na BRT kama mradi mmoja hata kama vitajengwa kwa kupishana kidogo. Ukiichukulia hivyo maana yake matokeo itakuwa ni njia sita, nne za sasa na mbili za BRT.

Ambacho ungetakiwa kulalamikia ni hizo njia tano unazozipenda maana hazikujengwa kwa kuangalia mpango wa muda mrefu, bali kwa ajili ya kupata umaarufu. Hizo ndio zimejengwa huku tukijua tutazivunja muda si mrefu. Hizi za sasa zitadumu muda mrefu.
 
Nadhani ni rahisi kuufikiria kinachojengwa sasa na BRT kama mradi mmoja hata kama vitajengwa kwa kupishana kidogo. Ukiichukulia hivyo maana yake matokeo itakuwa ni njia sita, nne za sasa na mbili za BRT.
Ambacho ungetakiwa kulalamikia ni hizo njia tano unazozipenda maana hazikujengwa kwa kuangalia mpango wa muda mrefu, bali kwa ajili ya kupata umaarufu. Hizo ndio zimejengwa huku tukijua tutazivunja muda si mrefu. Hizi za sasa zitadumu muda mrefu.
Mradi wa BRT assume ukajengwa miaka mi5 baadae baada ya kukamilika kwa BRT ya mbagala na BRT ya Karume, katika kipindi hiko cha miaka mi5 ni kwanini tusingendelea tu kufaidi flow kubwa ya magari ya njia 5?

Badala yake tumetumia pesa nyingi kuweka njia 4 na bado baada ya miaka mi5 hii barabara nayo itabidi ifumukiwe baadhi ya vipande ili kuhuisha na miundo mbinu ya BRT, haraka ilikuwa ya nini?

Kwanini wasingesubiri hiyo mika mi5 ili mradi ufanyike kwa pamoja kama ilivyokuwa kwa BRT phase 1? Ya nini kutuondolea njia 5 na kuweka njia4 ? Faida yake nini?

Napendekeza zile kerbstone za katikati ziondolewe iki tuendelee kua na njia 5 hadi hapo BRT itakapokuja.
 
 
Wakuu Kwema??

Mimi naishi Sinza (Makazi), na Shughuli zangu (Kazi) ni Posta. Mara zote hutumia njia hii ya kuanzia Sayansi mpaka Morocco napitiliza mpaka Posta. Njia hii toka inaanza kujengwa naiona, na mpaka sasa ilipofikia pia nimeiona. Na hata kabla haijajengwa hii mpya ya sasa still nilikua niitumia ile ya awali.

Hii barabara ilikua na njia nne, lakini sherehe fulani hivi za Uhuru nadhan kuna Mkuu mmoja akaamrisha iongezwe kua njia 5 na ikaongezwa. Sasa kuna kaujenzi kanafanyika pale sijui hata kanamaanisha nini. Kuta za fence zimevunjwa, parking zimeondolewa au kupunguzwa, Lami ya awali ikakwanguliwa ikawekwa ingine pamoja na kuweka vitofali lakini matokeo yake njia zimerudi kua nne.

Yaan baada ya Magazijuto yote hayo na gharama zote zilizotumika njia zimepunguzwa, nini sababu sasa hapa? Yaan gharama zote hizi zinazofanyika pamoja na kuwatia watu hasara ya kupunguza ukubwa wa parking zao lengo ndio kupunguza lanes kutoka 5 mpaka 4? Ili iweje?? Zile 5 za awali ambazo zilikua zinaacha parking za majengo ya watu salama zilikua zina shida gani?

Mwenye uelewa please msaada
 
Wakuu Kwema??

Mimi naishi Sinza (Makazi), na Shughuli zangu (Kazi) ni Posta. Mara zote hutumia njia hii ya kuanzia Sayansi mpaka Morocco napitiliza mpaka Posta. Njia hii toka inaanza kujengwa naiona, na mpaka sasa ilipofikia pia nimeiona. Na hata kabla haijajengwa hii mpya ya sasa still nilikua niitumia ile ya awali.

Hii barabara ilikua na njia nne, lakini sherehe fulani hivi za Uhuru nadhan kuna Mkuu mmoja akaamrisha iongezwe kua njia 5 na ikaongezwa. Sasa kuna kaujenzi kanafanyika pale sijui hata kanamaanisha nini. Kuta za fence zimevunjwa, parking zimeondolewa au kupunguzwa, Lami ya awali ikakwanguliwa ikawekwa ingine pamoja na kuweka vitofali lakini matokeo yake njia zimerudi kua nne.

Yaan baada ya Magazijuto yote hayo na gharama zote zilizotumika njia zimepunguzwa, nini sababu sasa hapa? Yaan gharama zote hizi zinazofanyika pamoja na kuwatia watu hasara ya kupunguza ukubwa wa parking zao lengo ndio kupunguza lanes kutoka 5 mpaka 4? Ili iweje?? Zile 5 za awali ambazo zilikua zinaacha parking za majengo ya watu salama zilikua zina shida gani?

Mwenye uelewa please msaada
Picha
 
Wakuu Kwema??

Mimi naishi Sinza (Makazi), na Shughuli zangu (Kazi) ni Posta. Mara zote hutumia njia hii ya kuanzia Sayansi mpaka Morocco napitiliza mpaka Posta. Njia hii toka inaanza kujengwa naiona, na mpaka sasa ilipofikia pia nimeiona. Na hata kabla haijajengwa hii mpya ya sasa still nilikua niitumia ile ya awali.
...
Haijakamilika. Ikikamilika itakuwa na njia sita. Nne magari ya kawaida na mbili mwendokasi.
 
Wakuu Kwema??

Mimi naishi Sinza (Makazi), na Shughuli zangu (Kazi) ni Posta. Mara zote hutumia njia hii ya kuanzia Sayansi mpaka Morocco napitiliza mpaka Posta. Njia hii toka inaanza kujengwa naiona, na mpaka sasa ilipofikia pia nimeiona. Na hata kabla haijajengwa hii mpya ya sasa still nilikua niitumia ile ya awali...
Kwa vile unatumia hiyo barabara kila siku kwenda mjini, mimi nakushauri siku ukiwa na nafasi shuka hapo barabara inapojengwa uwaulize hao wanaojenga (wasimamizi) watakupa ufafanuzi mzuri sana.
 
 
 
Back
Top Bottom