Barabara ya Morocco - Mwenge imetanuliwa ila njia zimepungua toka 5 hadi 4

Barabara ya Morocco - Mwenge imetanuliwa ila njia zimepungua toka 5 hadi 4

Wakuu Kwema??

Mimi naishi Sinza (Makazi), na Shughuli zangu (Kazi) ni Posta. Mara zote hutumia njia hii ya kuanzia Sayansi mpaka Morocco napitiliza mpaka Posta. Njia hii toka inaanza kujengwa naiona, na mpaka sasa ilipofikia pia nimeiona. Na hata kabla haijajengwa hii mpya ya sasa still nilikua niitumia ile ya awali...
Aliyetoa maelekezo kafa kama unaweza kufanya ufufuo naomba ufanye hivyo then tujadili(waache wafu wazikwe na wafu wenzao)
 
Hapana,siku hizi tumeondoa vihiyo kwenye safu ya viongozi watendaji.

Si unaona barabara ya katikati ina mortar nene zaidi na imewekewa kingo za vitofali vigumu!!!maana yake ni BRT hiyo.
Kama wamefanya hivyo ni njema maana hawa jamaa mipango yao huwa ya muda mfupi mfupi wa kuzima moto.
 
Kama wamefanya hivyo ni njema maana hawa jamaa mipango yao huwa ya muda mfupi mfupi wa kuzima moto.
Hakuna nafasi ya kufanya madudu mepesi namna hiyo, utasakamwa mpaka na mkeo nyumbani.

Kigogo-Boma nako kumekucha, kwa mistake za yard ya mwendokasi na barabara yake Jangwani, hatutegemei kosa lile kujirudia tena Kigogo.
 
Itakamilika lini lakini? Mbona miaka na miaka yenyewe inajengwa tu? Tena ni kakipisi kafupi tu!
Nafasi ya hapo katikati zitatoka barabara mbili. Kuwa na subra utaona itakavyokua kazi ikiisha. Hii kazi hajapewa mtanzania kazi itakua nzuri.
 
Kuna mwendokasi inakuja... lakini ukweli ni kwamba sasa hivi tuwe na at least 3x3. Hizi 2x2 hazichukui muda zinakuja kuwa kero.
 
Ni vema wangekuwa wanarahisisha haya maswali kwa kuweka mchoro wa hicho wanachotaka kujenga kuliko hivo wanavofanya, jambo lingine imekuwa na kona kona zisizo na Faida yoyote kwenye kupunguza traffic jam
 
Sasa huo si utaahira? Angalia mwendokasi zote jinsi zinavyojengwa, ile njia ya mwendokasi inakengwa sambamba na barabara za pembeni ili kuzihuisha na miundombinu za vituo, maji ya mvua, zebra crossing nk....
Mkuu ubora wa ile barabara unauonaje? Mm naona ata upana umeongezeka..na umezifanya barabara ziwe za one way..siyo zamani ambapo kulikua kunakupishana. So movement ya magari itakua kubwa na ajali pia zitapungua
 
Ndio na mimi nikuuliza, kulikuwa na haja gani ya kutumia matrillion ili kuounguza ufanisi wa barabara kutoka njia 5 hadi njia 4?! Yaani kabla ya ujenzi huu barabara ilikuwa na njia 5...
Road ilikua na mashimo ya hatari..haikuwa mpya hiyo mzee
 
Point hapa ni kua why upunguze wingi wa Lanes leo kwa ajili ya maandalizi ya mwendokasi itakayokuja kujengwa next three years or even more?
Kwani lanes zimepungua?

Hapo kabla zilikuwa ni 2x2, with an extra 5th lane in between kama one way, ikifanya kazi ya ama kurudi au kwenda town muda wa asubuhi na jioni...

Sasa hivi imekuwa 2x2 for public cars, 1x1 for the upcoming Morocco <> Tegeta BRT, and extra walkway kwa waenda kwa miguu...

Hivyo kuna hizo extras ambazo hazikuwepo...

Kupata njia pana zaidi ya ilivyo sasa ina maana watu walio kando ya barabara wangebomolewa majengo yao zaidi ya walivyobomolewa
 
Njia ya 5 ipo mifukoni mwa watu.
Vijana muache uzushi na negativity Kwa taifa lenu

pale kuna middle lane ambayo haijafunguliwa

most likely itakua ya DART

sijui kwanini watu tunapenda kuropokwa
 
Sasa huo si utaahira? Angalia mwendokasi zote jinsi zinavyojengwa, ile njia ya mwendokasi inakengwa sambamba na barabara za pembeni ili kuzihuisha na miundombinu za vituo, maji ya mvua, zebra crossing nk; hivyo lazima hii itakuja kufukuliwa hata kama si yote; ona BRT ya sasa toka Magomeni hadi karume, lazima barabara ya pembeni ifumukiwe kuendana na BRT lanes.

Halafu kwanini upunguze efficiency ya barabara toka njia 5 hadi 4 kwa excuse ya BRT? Kwanini usisubiri hadi ujenzi wa BRT uanze ili ifanyike moja kwa moja? Hebu niambie, ule ujenzi umeachieve nini ambacho hakikuwepo mwanzo zaidi ya kupunguza achievement iliyofsnywa nyuma toka njia 5 hadi 4? Goal ya mradi ilikuwa kuleta foleni au?
Mataahira mmekua wengi sana
 
Mkuu ubora wa ile barabara unauonaje? Mm naona ata upana umeongezeka..na umezifanya barabara ziwe za one way..siyo zamani ambapo kulikua kunakupishana. So movement ya magari itakua kubwa na ajali pia zitapungua
Kwanini wasingeacha zile njia 5 ukizingatia zilikuwa bado mpya baada ya kukarabatiwa kwa pesa za Uhuru?, badala yake matrilioni yametumika na zimekuwa 4 kutoka 5?
 
Road ilikua na mashimo ya hatari..haikuwa mpya hiyo mzee
Kwahiyo matrilioni yaliyotumika kupunguza njia toka 5 hadi 4 ni ili kuepuka kufanya periodic maintanance ya barabara kama inavyohitajika? Na hii ya sasa ikipata mashimo mtaivunja tena yote?
 
Kwani lanes zimepungua?

Hapo kabla zilikuwa ni 2x2, with an extra 5th lane in between kama one way, ikifanya kazi ya ama kurudi au kwenda town muda wa asubuhi na jioni...

Sasa hivi imekuwa 2x2 for public cars, 1x1 for the upcoming Morocco <> Tegeta BRT, and extra walkway kwa waenda kwa miguu...

Hivyo kuna hizo extras ambazo hazikuwepo...

Kupata njia pana zaidi ya ilivyo sasa ina maana watu walio kando ya barabara wangebomolewa majengo yao zaidi ya walivyobomolewa
Kwahiyo njia za magari toka njia 5 hadi 4 we unaona hazijapungua? Na kwanini usisubiri hadi ujenzi wa BRT uanze ndio uvunje ila kwa wakati huu watu wangeendelea kufaidi flow ya njia 5 badala ya 4?
 
Vijana muache uzushi na negativity Kwa taifa lenu

pale kuna middle lane ambayo haijafunguliwa

most likely itakua ya DART

sijui kwanini watu tunapenda kuropokwa
Kwanini upunguze njia toka 5 hadi 4 kwa mradi utakaokuja kujengwa miaka 5 hadi 10 baadae?
 
Back
Top Bottom