Baraza Kuu la Waislam Tanzania latoa tamko kuhusu Mahakama ya Kadhi na Katiba iliyopendekezwa

Status
Not open for further replies.



Utamuona yule kibaraka wa CCM anaejiita shehe mkuu wa mkoa wa dar akipinga hili tamko huku povu likimtoka
 
Last edited by a moderator:
bado tamko la makafiri! kazi ipo!
kura ya hapana ya katiba...tulishavurugwa kitambo..iwe ndio au hapana bado watawala wameshinda.
Muhimu tujipange na watakao kuja...maana ndio wataweza kuokoa nchi na tukawa na dira!
kwangu kuhaidiwa/kupewa mahakama ya kadhi ili utoe kura ya ndio, HIYO NI RUSHWA.
 
kumbe na mufti hapatikani kisheria maana ofisi yake haiundwi kisheria.
hapo ndo utata unapoanza!
halafu nilishangaa kuona watu wanaingiza interest za dini ili hali awali ilifafanuliwa taifa kutokuwa na dini!
na tena muungano hautavunjwa tujadili namna ya kuboresha!
ujinga ni maradhi-nyerere
 
wapi alama yoyote kuenyesha kuwa waraka/tamko hili limetoka sehemu tajwa? japo jina na signature ya mwandishi? au japo kijimuhuli cha taasisi tajwa? hofu yangu isije ikawa nimeandika mimi na kuwasingizia waislamu wenzangu. nawasilisha.
 
Ndugu zangu waislamu ulazima wa serikali kugaramia hiyo mahakama yenu unatoka wapi ili hali mnajua haitahudumia kundi Fulani la walipako kodi acheni ubinafisi bana
 

Kuna hoja inakupita kushoto hapa bibie..,!!!

Nikwamba Tamko hili limetolewa na JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAM (T)

Kimsingi vyombo hivi ni tofauti ingawaje vyote ni vya Kiislam. Nadhani umepotoshwa na kichwa cha habari cha kaka Mohamed Said tuombe mods wabadirishe hicho kichwa cha habari. Lakini ni lini mtaacha kumlalamikia Nyerere juu ya uanzishwaji wa hilo BAKWATA?

Mbona basi ninyi mliohai hamchukui hatua zozote kuliondoa? Au mnataka Nyerere afufuke kutoka katika wafu aje awaondolee hilo Zimwi? Na mbona basi bado mwahitaji serikali ileile ambayo ilikuwa ikiongozwa na Nyerere wakati huo na ikaanzisha hii BAKWATA, mnataka sasa iwaanzishie Mahakama ya Kadhi? Mbona mi sielewi kitu hapa?? Kipi ni kipi bibie hebu funguka kidogo.

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Kwa hili la kupinga mahakama ya kadhi CCm naaunga mkono 100%. Nchi hii haina dini, ole yake serkali itakoyothubutu kukubaliana na jambo hili gumu linalovunja umoja wa nchi yetu.
 
msitutanie nyie iyo kitu haiwezi kua apa Tz ata Rais angekua sh simba
 

Msalani uko wapi uje uitete ccm
 

Kesho bakwata itakuja na kauli ya kupinga hili tamko wewe utakuabwapi
 
Acha kupotosha. kura ya hapana haimaanishi tunarudi kwenye katiba ya 1977. bali tunakwenda kurekebisha iyo katiba ya ccm

Pindi yanapofanyika hayo marekebisho tunakuwa tunatumia katiba ipi? Hata hivyo ikukae akilini kuwa hata yafanyike marekebisho mara hamsini, mahakama ya kadhi haiwezi kuwemo kwenye katiba. Mnavyofikiria nyie kupiga kura ya hapana ili kulazimisha Mahakama ya kadhi basi ndivyo wakristu tutakavyopiga kura ya hapana pindi mahakama ya kadhi itakapowekwa.
 
Siipendi CCM, lakini kwa suala la Mahakama ya kadhi, naiunga mkono CCM 100%.
 
Mahakama ya Kadhi kuanzishwa nchi hii haitatokea,Waislamu tafuteni mambo mengine ya msingi ya kudai kwasababu hili la mahakama ya kaadhi haliwezekani.
 
sielewi hapa

huelew nin nchi hii haina dini ila watu wake wana dini kwa mana ya kwamba uko huru kuabudu unavyojua ww na wala hutaingiliwa sasa unapotaka hela ya serikali itumike kwa mambo yenu ya dini hapo ndipo unapoleta matatizo
 
Mimi si muislamu na sitaki kuamini kua uanzishaji wa mahakama ya kadhi hapa Tanganyika utakua na athari kwa taifa.Mi nadhani ianzishwe tu mbona nchi nyingine wana mfumo huo na hakuna shida?.Mwaka huu msikubali ahadi.

Mahakama ya Kadhi ina athari kwa Kanisa na Nchi kwa sababu ni IBADA.Kazi ya ibada ni ya dini husika hivyo serikali haipaswi kujiegemeza kwenye Dini moja na kueneza Hadithi za Mtume.Kikanisa ina athari kwa sababu Kodi ya Mkristo aliyotoa baada ya kuuza Kitimoto itatumika kueneza Ibada ya Dini ya Kiislamu.Hiyo ni sawa na kushiriki kueneza Dini ya Kiislamu ambayo kimsingi sio Mungu wao anayotaka wayaishi;Kumbuka wakristo wanaaswa na Mungu wao kutokuabudu Miungu mingine.
 

Taasisi ipi, jumuiya ya waislam au bakwata?

Kwa kukusaidia bakwata imeasisiwa na nyerere na ndio muhimili mkubwa CCM kwa maswala ya uchaguzi
 
Last edited by a moderator:
Kumbe na wewe hujui mwelekeo, yaani upo upo tu, ndiyo maana umesema utafuata watakachosema waislamu nilifikiri utafuata misingi ya dini ya kiislamu.
 
Huu uzi utafungwa muda si mrefu.

Naam,na ufungwe maana hauna tija.Hapa tunajadili mambo ya kitaifa na sio ya vikundi.Hatuwezi kukaa hapa kujadili Mahakama ya Kiislamu kwa niaba ya wenye mahakama yao.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…