Baraza la Sanaa Zanzibar: Wanaume Wanaosukwa kama Wanawake kukamatwa, faini ni Tsh. Milioni 1 au kifungo cha Miezi 6
Kwanini Mwanaume usuke na kufanana na Wanawake?

Kwa hili nawaunga mkono. Wasiishie hapo wawaadhibu na Wanaume wote wanaovaa hereni, kuweka nywele dawa na wavaao milegezo

Hatutaki Machoko.
 
Zenji hawana kazi, wanaenjoy tu mapesa kutoka Bara. Kwahiyo wameamua kujishughulisha na wasukaji.
 
Serikali ya Zanzibar imesema ni kosa kisheria mwanaume kuingia au kuishi viziwani Zanzibar akiwa amesuka nywele.

''Kwa mujibu wa sheria zetu ukikutwa utatozwa faini ya milioni moja za kitanzania ambayo ni zaidi ya dola 400 za kimarekani au kufungwa jela miezi sita au adhabu zote kwa pamoja,” imeeleza Serikali ya Zanzibar.

Akizungumza na BBC, Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Filamu na Utamaduni Zanzibar, Dkt Omar Adam amesema serikali kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi imeanza operesheni ya kukamata wanaume wote waliosuka nywele ikiwa ni utekelezaji wa sheria inayokataza wanaume kusuka nywele ili kulinda maadili na tamaduni za Zanzibar.

Dkt Omar amesema vijana wengi visiwani humo wamekuwa na hulka ya kusuka nywele kinyume na taratibu za wazanzibar.

Alisema,” Sifahamu kama kuna mzee yoyote hapa Zanzibar ambaye atamchukua mwanae wa kiume halafu ampeleke saluni kusuka nywele. Huu si utamaduni wa Zanzibar na sisi kama wasimamia sheria lazima tuzuie hili.”


SOURCE: BBC SWAHILI
Pia wapige marufuku wanawake kuvaa suruali, kwa utamaduni wa Kizanzibari na dini ya Kiislamu mwanamke anatakiwa avae buibui na si kuvaa suruali au gauni au sketi fupi.
 
Naona iko poa hii sheria inakuwaje mwaume unasuka unakuwa Kama mwanamke hapo Zanzibar nawapa heko.

Iko hivi

BBC wanaripoti kuwa mwaume yeyote akikamatwa amesuka huko visiwani ni jela miezi sita na faini

My take,hii sheria iletwe bongo haraka na tuongeze adhabu na nakosa Kama hereni na kupakatwa rangi

USSR
 
.
 

Attachments

  • IMG-20230711-WA0024.jpg
    IMG-20230711-WA0024.jpg
    63.9 KB · Views: 8
Mi nacho ona huyu jamaa kwa sababu kapewa para basi anataka watu wote wafanane ni sawa na kuomba Tajili afirisike hiyo serikali inayompa kiburi itapata wapi maokoto yake.....wakati mwingine busara ni ukimya tu kwani angekaa kimya watu Wasinge jua kama ni dkt.......? Sasa ona dokta anaiba Sindano...tena used
 
Naona iko poa hii sheria inakuwaje mwaume unasuka unakuwa Kama mwanamke hapo Zanzibar nawapa heko.

Iko hivi

BBC wanaripoti kuwa mwaume yeyote akikamatwa amesuka huko visiwani ni jela miezi sita na faini

My take,hii sheria iletwe bongo haraka na tuongeze adhabu na nakosa Kama hereni na kupakatwa rangi

USSR
 
Wanaume Zanzibar kusuka nywele faini Sh1 milioni.jpg

Muktasari:​

  • Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Elimu na Utamaduni Zanzibar, Dk Omar Adam amesema hatua hiyo inalenga kulinda silka na tamaduni za Kizanzibari.
Unguja. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepiga marufuku tabia ya wanaume kusuka nywele na anayekamatwa faini yake ni Sh1 milioni au kifungu cha miezi sita au vyote kwa pamoja.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Julai 11, 2023, Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Elimu na Utamaduni Zanzibar, Dk Omar Adam amesema hatua hiyo inalenga kulinda silika na tamaduni za Kizanzibari.
Amesema katazo hilo ni kwa mujibu wa sheria namba saba ya mwaka 2015 inayolenga kulinda utamaduni, mila na desturi za Mzanzibari bila kuathiri mambo mengine.
“Zanzibar hairuhusu mwanaume kusuka nywele faini ya kusuka nywele kwa Zanzibar ni Sh1 milioni au miezi sita jela au vyote kwa pamoja,” amesema.
Amesema hakuna kibali wala kulipia ili uruhusiwe kusuka nywele kwa mwanamme kama ambavyo awali ilisambaa kwennye mitandao ya kijamii.
“Sheria ilikuwa haijaanza kutekelezwa kwa kutoa faini lakini imeshatokea kama mara tatu mtu anakamatwa na kupewa onyo na wengine wapo wamejirekebisha na wengine wanaendelea kujirekebisha,” amesema
Hata hivyo, amesema katazo hilo haliwahusu Wamaasai kwasababu wanatambua kwamba huo ndio utamaduni wao kwamba mwanaume anasuka na mwanamke ananyoa au naye anasuka.
Kuhusu suala la kuathiri utalii wa Zanzibar, Katibu huyo amesema haliwezi kuathiri kwa sababu utafiti alioufanya kwanza watalii wengi hawasuki huo ni utamaduni ambao umetokea huku.
Kuhusu wasanii, amesema iwapo kuna msanii anataka kufanya shughuli zake wanaweza kukutana naye wakazungumza akavaa kofia mpaka anapokwenda kwenye maonyesho yake.
“Tunachosema suala la ushirikiano wa Muungano kisiwei kichaka cha kuharibu tamaduni silka na atamaduni za Kizanzibar ni akam ilivyo bangi hatuwezi kuruhusu kwamba ziendeel huku asili tuliochiwa na wazee wetu inapotea na katika sula hili tumejipanga tutakuwa wakali sana” alisema
Amesema watapitia hata kwenye shule kutoa elimu hiyo kwa walimu na wanafunzi ili kuwadhibiti wnafunzi wenye tabia hizo.
Sio mara ya kwanza kwa Zanzibar kutoa makatazo kama hayo, mwaka 2021 aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Lela Musa alipiga marufuku kuvaa nguo fupi (nusu uchi) kwa watalii ili kulinda utamaduni wa Zanzibar
Agizo hilo lilitolewa, huku ikielezwa iwapo wakibainika wameevaa nguo zisizo na stara atakamatwa anayewatembeza na kutozwa faini, hata hivyo jambo hilo utekelzaji wake haukuzingatiwa.
Pia, Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashidi Msaraka aliwahi kupiga marufuku vijana wanaonyoa viduku ambapo aliwahi kuwakamata na kuchukua mkasi kuwanyoa, hata hivyo nalo halikuwa na mwendelezo wake. chanzo. Wanaume Zanzibar kusuka nywele faini Sh1 milioni
 
Dkt.Omar Adam
Dkt. Adamu anajisafisha nyoyo tu ukilitizama hili shauri kiundani utaona amekosa kufikiria kwa kutumia huo utamaduni anaotaka kuulinda. Ana tumia mila na desturi za kikoloni!

Ni sawa na kuwaambia vijana wenzangu pale kiboroloni wakatae kusikia,kucheza mimbo ya Taarabu, miduara. DKt Adamu Amevuka mipaka na kukandamiza Uhuru wa watu. Anaviashiria vya Dictator kama walivyo wenzake wengi.
 
Katibu Mtendaji Baraza la sanaa, Sensa ya Filamu na Utamaduni, Dkt.Omar Adam leo kwenye Asubuhi Njema ya ZBC ameelezea mengi yanayohusu sekta ya sanaa, filamu na namna wanavyosimamia Mila, Desturi na Utamaduni wa Zanzibar.

Amesema "Moja ya kazi kubwa ya Baraza la sanaa Zanzibar ni kulinda Mila, Siha, desturi na Utamaduni wa Zanzibar, Baraza hili la sanaa pia lina minasaba na wananchi wote wa Zanzibar katika sekta ya filamu, sanaa na Utamaduni"

Ameongeza "Sisi kama Baraza hatufurahishwi kabisa na watu wanaoiga utamaduni wa nje ya Zanzibar kwasababu watu wengi wa nje wanakuja Zanzibar kujifunza kwasababu wanavutiwa na utamaduni, taratibu na desturi za Zanzibar"

Aidha, amebainisha "Askari wanakamata wanaume wote wanaosuka nywele kama za wasichana, Baraza la sanaa hatupendelei hilo na kuna kibali maalumu cha kusuka nywele ambacho ni milioni 1 na tumeweka bei hiyo ili kuwakomoa, sasa utachagua mwenyewe utoe milioni usuke au ununue kiwembe chako unyoe"

PhD aliipataje huyu? Au Ni daktari wa wanyama pori?
 
Katibu Mtendaji Baraza la sanaa, Sensa ya Filamu na Utamaduni, Dkt.Omar Adam leo kwenye Asubuhi Njema ya ZBC ameelezea mengi yanayohusu sekta ya sanaa, filamu na namna wanavyosimamia Mila, Desturi na Utamaduni wa Zanzibar.

Amesema "Moja ya kazi kubwa ya Baraza la sanaa Zanzibar ni kulinda Mila, Siha, desturi na Utamaduni wa Zanzibar, Baraza hili la sanaa pia lina minasaba na wananchi wote wa Zanzibar katika sekta ya filamu, sanaa na Utamaduni"

Ameongeza "Sisi kama Baraza hatufurahishwi kabisa na watu wanaoiga utamaduni wa nje ya Zanzibar kwasababu watu wengi wa nje wanakuja Zanzibar kujifunza kwasababu wanavutiwa na utamaduni, taratibu na desturi za Zanzibar"

Aidha, amebainisha "Askari wanakamata wanaume wote wanaosuka nywele kama za wasichana, Baraza la sanaa hatupendelei hilo na kuna kibali maalumu cha kusuka nywele ambacho ni milioni 1 na tumeweka bei hiyo ili kuwakomoa, sasa utachagua mwenyewe utoe milioni usuke au ununue kiwembe chako unyoe"

Akili za kijinga kabisa,unasema unalinda utamaduni wa zenj,lakini upo tayari kulipwa hera ili utamaduni uvunjwe!!wanaume walipie kibari cha kusuka!!
Sheria haitungwi kukomoa watu,bali kuweka na kulinda Jamii,
Shida ya kuangalia kila kitu kupitia macho ya dini
 
Wameona wachangishe 1M kwa wanaosuka...daah washaanza kuwa na Tozo za hovyo hovyo kama Bara...
 
Back
Top Bottom