Bashiru Ally: Heshima ya nchi yetu imeshuka, tunadhalilika kwa njaa

Bashiru Ally: Heshima ya nchi yetu imeshuka, tunadhalilika kwa njaa

Mh....Watu mnapita na ku like post ila hamchangii?

Okay mi mchango wangu ni, vyakula kupanda bei ni kutokana na ukame wa mwaka jana.

Japo serikali ilihifadhi chakula kingi kwenye maghala hadi maximum yake ya tani laki 2 bado chakula hicho hakikutosha

Swala hili halina suluhu ya muda mfupi, suluhu ya uhakika ni kutengeneza mifumo ya kilimo cha umwagiliaji ambayo itachukua muda na gharama

Ama kama tuagize mahindi ya bei rahisi kutoka Brazil na Argentina? Tukifanya hivyo jua wakulima wetu mahindi yao hayatauzika
Kwahiyo ni Bora wakulima wetu wauze mahindi Yao kwa bei ya juu na Wananchi waendelee na msoto?
 
Bashiru amezunguuka wee, lakini nadhani mkakati anaokusudia Serikali ichukue ni kuzuia chakula kuuzwa nje, sio mwingine. Kwangu huu ni mkakati wa kipuuzi na haujawahi kuleta manufaa ya kweli toka huko nyuma. Suluhu ya kweli ni kuzalisha tu, no otherwise. Njaa imekuwepo nchi hii tangu wakati wa ukoloni na hata katika awamu za kwanza hadi ya 5 na mara zote hizo mkakati wa kuzuia mazao haukuwa na manufaa endelevu. Unafifisha uwekezaji na unaifanya sekta ya kilimo isiaminike kwa mtu kuweka mtaji wake.

Bashe na Samia nadhani ndo wana mkakati wa kweli wa kuondoa tatizo la njaa nchi yetu. Kuwaingiza vijana kwenye uzalishaji kwa kuwapa mafunzo, ardhi, mtaji, miundombinu na masoko ya bidhaa zao. Dkt Bashiru kuzungumzia tatizo la njaa bila kuchangia namna bora zaidi ya kuufanya mpango huu ufanikiwe ni kutukosea watanzania na kumkosea Rais wetu au ni unafiki kama unafiki mwingine tu.

Hakuna mikakati ya muda mfupi itakayoweza kuondoa njaa Tanzania zaidi ya kuongeza uwekezaji na kuzalisha chakula cha kutosha. Na bahati mbaya, Dkt Bashiru hasema kwenye mchango wake kama ni mikakati gani hiyo serikali ifanye zaidi ya huu unaofanywa sasa hivi wa "building better tomorrow", badala yake ameiuliza maswali Serikali badala ya kuishauri. Ingependeza mchango wake angeutoa Alhamis siku ya maswali kwa Waziri Mkuu.
Hivi kama ukiuza mahindi Kenya gunia unaliuza laki 2 ila ukiuza nchini unauza laki 1 wewe utakimbilia kuuza wapi?

Kitu gani ambacho kitafanya wewe uache kwenda kuuza Kenya kwenye faida mara 2 kama sio zuio. Hivi unaweza ukapambana na demand ya kulisha nchi yetu na nchi, za jirani hadi watosheke demand ishuke kiasi kwamba watu wa nchini nao wapate ahueni.

Nachojua siku zote mfanyabiashara anajaligi faida yake tu hata kama nyumba ya jirani wanakufa njaa haimuhusu alimradi yeye wakwake wamekula wameshiba. Tabia za kishetani za ubinafsi aina hii ndio zilimfanyaga Nyerere akagombana na watu wengi na iko against humanity.

Kinachofanya bei zipande ni kwa sababu hamna mtu anayejali na waziri mwenye dhamana naye yuko kwenye mkumbo wa wafanyabiashara wakubwa wanaouza nje hivyo mfumo huo unam favor yeye. Hoja ya kusema kila mtu alime ni ya kishenzi. Atoe mabillion yake alioficha bank agawie watu maeneo na mitaji wakalime basi kama ni jambo rahisi.
 
Wewe ndio mpuuzi, hivi kama ukiuza mahindi Kenya gunia unaliuza laki 2 ila ukiuza nchini unauza laki 1 wewe utakimbilia kuuza wapi?

Kitu gani ambacho kitafanya wewe uache kwenda kuuza Kenya kwenye faida mara 2 kama sio zuio. Hivi unaweza ukapambana na demand ya kulisha nchi yetu na nchi, za jirani hadi watosheke demand ishuke kiasi kwamba watu wa nchini nao wapate ahueni.

Nachojua siku zote mfanyabiashara anajaligi faida yake tu hata kama nyumba ya jirani wanakufa njaa haimuhusu alimradi yeye wakwake wamekula wameshiba.

Kinachofanya bei zipande ni kwa sababu hamna mtu anayejali na waziri mwenye dhamana naye yuko kwenye mkumbo wa wafanyabiashara wakubwa wanaouza nje hivyo mfumo huo unam favor yeye. Hoja ya kusema kila mtu alime ni ya kishenzi. Atoe mabillion yake alioficha bank agawie watu maeneo na mitaji wakalime basi kama ni jambo rahisi.
Duniani kote, watu wanapigana vikumbo hadi vikwazo kutafuta masoko. Kama kuna bidhaa mnazalisha na mna soko la uhakika la kuuza kila mnachozalisha basi mjione mna bahati sana. Sijawahi kuona mwenye kiwanda au biashara akilia eti wateja wananunua sana bidhaa zake. Tufanye bidhaa za chakula kama bidhaa nyingine, tutafanikiwa sana lakini tukiona kuwa kazi ya kilimo ni kusukuma siku ziende mbele, tutakwama. Jiongeze.
 
Duniani kote, watu wanapigana vikumbo hadi vikwazo kutafuta masoko. Kama kuna bidhaa mnazalisha na mna soko la uhakika la kuuza kila mnachozalisha basi mjione mna bahati sana. Sijawahi kuona mwenye kiwanda au biashara akilia eti wateja wananunua sana bidhaa zake. Jiongeze.
Sawa unazungumzia kiwanda. But this situation has to be controlled.

Watu wasipofungiwa kuuza nje basi waambiwe wauze bei ambazo zinaendana na situation ya uchumi wetu. Ziwekwe bei elekezi tu maana bila hivyo kila mtu atalazimisha auze bei ya laki 2 kama anavyouza Kenya na hiki ndio kimeleta inflation.

Wakizuiwa kabisa kuuza nje bei zitadrop sababu demand itakuwa chini.
 
Jibu swali wewe basha wa Bishiru,ni wapi na lini aliwahi sikia Tzn Kuna njaa Hadi heshima ya Nchi kushuka?

Kuwa Rais mpenda Haki sio kuwachekea wapumbavu kama wewe na Bashiru wanaotafuta umaarufu Kwa kupotosha.
Amesema njaa hupelekea kushusha heshima. Sikiliza vizuri usikurupuke. Hajasema Tanzania kuna njaa ya kutisha
 
Yes,Mr bashiru,huyu ni mtu makini,mwaminifu,na ni mzalendo halisi,Ninampenda sana huyu mtu kwa hoja na mawazo yake,utendaji wake kwa mda mfupi kwenye chama na serikali,amefanikiwa kujitengenezea maadui wengi sana,
Huyu Bwana Bashiru hana adui yaani mtu apoteze mda kumuwkea bifu mjinga kama bashiru
Huyu kipindi ananeemeka nakiti cha enzi hakuona magu alivyokua akiwaambia wananchi waliokua wakisumbuliwa naukame njaa naumasikini hatawapa msaada wachakula wala chochote serikali haina shamba ila leo anajivika ngozi yakondoo mbwa huyu amuache Mama afanye kadri ya uwezo wa Jamhuri na sikipindikile walipo poka madaraka yakijamhuri nakua ya mtu mmjo

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Yes,Mr bashiru,huyu ni mtu makini,mwaminifu,na ni mzalendo halisi,Ninampenda sana huyu mtu kwa hoja na mawazo yake,utendaji wake kwa mda mfupi kwenye chama na serikali,amefanikiwa kujitengenezea maadui wengi sana,
Huyu Bwana Bashiru hana adui yaani mtu apoteze mda kumuwkea bifu mjinga kama bashiru
Huyu kipindi ananeemeka nakiti cha enzi hakuona magu alivyokua akiwaambia wananchi waliokua wakisumbuliwa naukame njaa naumasikini hatawapa msaada wachakula wala chochote serikali haina shamba ila leo anajivika ngozi yakondoo mbwa huyu amuache Mama afanye kadri ya uwezo wa Jamhuri na sikipindikile walipo poka madaraka yakijamhuri nakua ya mtu mmja

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Hakika anastahili kupongezwa kwa kusimamia Ukweli..tunahitaji viongozi wenye msimamo na wasioogopa kutoa maoni yenye tija kwa taifa
 
Sawa unazungumzia kiwanda. But this situation has to be controlled.

Watu wasipofungiwa kuuza nje basi waambiwe wauze bei ambazo zinaendana na situation ya uchumi wetu. Ziwekwe bei elekezi tu maana bila hivyo kila mtu atalazimisha auze bei ya laki 2 kama anavyouza Kenya na hiki ndio kimeleta inflation.

Wakizuiwa kabisa kuuza nje bei zitadrop sababu demand itakuwa chini.
Yote mawili hayawezekani na VERY WRONG na hapo ndipo tunapokosea tunapoamini kuwa jukumu la mkulima ni kumpa nafuu mtanzania mwingine. Kilimo ni shughuli kama shughuli nyingine na hivyo mhusika afanye kile anachoona sawa bila kuathiri sheria za nchi. Kwa mbaaali ningekuelewa kama ungesema bidhaa za chakula ziuzwe nje zikiwa processed tena kwa mbali sana lakini sio kuzuia kabisa. Huwezi kuweka bei kikomo kwenye mahindi au mchele iwapo unazalishwa nchini na iwapo unataka hiyo sekta ikue.

Bei elekezi inaweza kuwekwa kwenye bidhaa ambazo unaweza kujua gharama ya bidhaa hiyo at any point. Kama mahindi utayaleta kutoka nje kama kule zenj, yes utaweza kuweka bei elekezi lakini sio kwa informal way of production kama uliopo sasa, vinginevyo bei elekezi iwe kwa kila hatua katika kilimo (gharama ya ardhi iwe na kikomo, vibarua wawe na kikomo, uvunaji, usafirishaji nk). Na mwishowe, kila mkulima awe na mashine ya efd ili iweze kuonyesha bei aliyonunua mfanyabiashara kwa mkulima kiasi gani na ameingia gharama gani na yeye profit margin yake kiasi gani. Usione baadhi ya bidhaa kuwa na bei elekezi then ukadhani ni mchakato rahisi.
 
"Njaa inadhalilisha heshima na uhuru wa nchi, inatweza utu wa binadamu kwahiyo tatizo la mfumuko wa bei za vyakula ni tatizo ambalo tutake tusitake lazima tuongeze kiwango cha ubunifu kukabiliana nalo, hakuna ukomo wa ubunifu, wananchi wanakibiliana na tatizo hili.

"Nilikuwa nazungumza na wananchi mmoja amesema chakula cha asubuhi na mchana kinaunganishwa kwenye saa 5 na 6, mlo wa usiku unaunganishwa kati ya saa 11 na 12, hawasubiri kujadili mambo ya Ukraine na tabianchi, wameanza kuchukua hatua.
View attachment 2502022
Mimi nafikri bashiru anataka serikali, ifanye haraka kutafuta tatizo
1. Kutokutegemea mvua za misimu, kutafuta haraka hata maji ya chini ya ardhi, ambayo ni mengi. Ambapo ukafanyika kilimo cha umwagiliaji wa mazao ya muda mfupi.
2. Kuruhusu watu binafsi, kuchimba visima kwa ajili ya umwagiliaji.
Ana nia nzuri sana sema alitakiwa kushauri njia nilizotaja ataeleweka vizuri zaidi.
 
Bashiru amezunguuka wee, lakini nadhani mkakati anaokusudia Serikali ichukue ni kuzuia chakula kuuzwa nje, sio mwingine. Kwangu huu ni mkakati wa kipuuzi na haujawahi kuleta manufaa ya kweli toka huko nyuma. Suluhu ya kweli ni kuzalisha tu, no otherwise. Njaa imekuwepo nchi hii tangu wakati wa ukoloni na hata katika awamu za kwanza hadi ya 5 na mara zote hizo mkakati wa kuzuia mazao haukuwa na manufaa endelevu. Unafifisha uwekezaji na unaifanya sekta ya kilimo isiaminike kwa mtu kuweka mtaji wake.

Bashe na Samia nadhani ndo wana mkakati wa kweli wa kuondoa tatizo la njaa nchi yetu. Kuwaingiza vijana kwenye uzalishaji kwa kuwapa mafunzo, ardhi, mtaji, miundombinu na masoko ya bidhaa zao. Dkt Bashiru kuzungumzia tatizo la njaa bila kuchangia namna bora zaidi ya kuufanya mpango huu ufanikiwe ni kutukosea watanzania na kumkosea Rais wetu au ni unafiki kama unafiki mwingine tu.

Hakuna mikakati ya muda mfupi itakayoweza kuondoa njaa Tanzania zaidi ya kuongeza uwekezaji na kuzalisha chakula cha kutosha. Na bahati mbaya, Dkt Bashiru hasema kwenye mchango wake kama ni mikakati gani hiyo serikali ifanye zaidi ya huu unaofanywa sasa hivi wa "building better tomorrow", badala yake ameiuliza maswali Serikali badala ya kuishauri. Ingependeza mchango wake angeutoa Alhamis siku ya maswali kwa Waziri Mkuu.
Hata mzalishe kwa Wingi Kiasi gani, hatuwezi meet Demand ya nchi majirani. Hivyo lazima tutacreate Ombwe hapa kwetu......
Wanufaika moja kwa moja si wakulima ila ni Walanguzi wachache, ambao ni maelfu tu.
Nakuacha Mamilioni ya Watanzania wanaumia.
 
Huyu mtu ana asili na uzoefu katika masuala ya taaluma, lkn pia ni mtu aliyekopwa kwa ajili ya sababu za kiutendaji za kisiasa. "Analysis" yake inaaminika na pia yenye mantiki, kwa mazingira na muktadha wa kijamii na kiuchumi tunayoyapitia kama taifa.

Baniani mbaya, ila kiatu chake ni dawa. Huyu ni mtu mwenye uaminifu wa milengo ya siasa za kijamaa, ila ni mtu mwenye msimamo wa kile alichoaminishwa na kukiamini.
Hili nalo tutalitazama
 
Baadae mwaka huu huu 2023,

Umetabiriwa ukame na njaa ambayo haikuwahi Kutokea tangu uhuru.

Kukauka Kwa MTO Ruvu na vyanzo vya maji ni Ishara juu ya yajayo juu ya nchi.

Tumepewa muda wa kutumia mvua kidogo kulima na kuhifadhi chakula.

Nabii asema, njaa hiyo na ukame waeza chukua Hadi miaka 3 na nusu.

USHAURI.

1. SERIKALI.

Mfute KAZI ndugu BASHE na atafutwe waziri atakayefanya jitihada ktk KILIMO na kujenga maghala ya kuhifadhi chakula.

Jambo hii lilifanywa na YUSUPH enzi za FARAO ilipotokea njaa ya miaka 7.

2.WANANCHI.

Tumieni pesa zenu kununua chakula na kutunza Kwa kadri muwezavyo Ili kustahimili yajayo.

Pia hakikisheni mnapunguza uwekezaji na matumizi yasiyo ya lazima, kiufupi tufunge mikanda.

3. WAKULIMA.

Tumieni mvua hizi kulima Kwa bidii na kutunza vyakula na msiuze.

4.WANA wa MUNGU.

Tuzidishe MAOMBI ya TOBA na REHEMA juu ya nchi yetu nzuri ya TANZANIA Ili Mungu aiondoe ADHABU juu yetu.

Ee Mwenyezi Mungu, Tunakuomba utusikie.

Aaaamen.
 
Hata mzalishe kwa Wingi Kiasi gani, hatuwezi meet Demand ya nchi majirani. Hivyo lazima tutacreate Ombwe hapa kwetu......
Wanufaika moja kwa moja si wakulima ila ni Walanguzi wachache, ambao ni maelfu tu.
Nakuacha Mamilioni ya Watanzania wanaumia.
Kwani mzalishaji utakuwa peke yako? Hizo nchi nazo sitakuwa zinazalisha, hazitakaa ziwasubiri nyie tu.
 
Huyu Bwana ni Kati ya Wajamaa na Wazalendo wachache waliobaki katika Taifa letu.

Ili tuendelee tunahitaji wakina bashiru wengi kwenye Uongozi wa nchi na sio Wanufaika wa kuyengeneza matatizo ili wapate Fedha kupitia Matatizo.
 
Huyu mpuuzi alitakiwa sasa hivi awe jera alifuja mabilioni ya walipa kodi kwenda kununua wapinzani kwa kushirikiana na jiwe.
Hana cha kumfundisha bashe atutolee unafiki.
Kwanini hao wapinzani wakawa malaya malaya hadi wakajiuza?

Utanunua kisichojiuza?
 
Hata mzalishe kwa Wingi Kiasi gani, hatuwezi meet Demand ya nchi majirani. Hivyo lazima tutacreate Ombwe hapa kwetu......
Wanufaika moja kwa moja si wakulima ila ni Walanguzi wachache, ambao ni maelfu tu.
Nakuacha Mamilioni ya Watanzania wanaumia.
Wewe ni mkulima?
 
Akili zimerejea ? Kama kiongozi angetoa hata solution moja ambayo serikali ingefanya....kudhibiti mfumuko bei uliosababishwa na ukame mwaka jana
Solution iko kwenye hayo maswali aliyomuachia bashe hapo mwishoni
 
Back
Top Bottom