Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Nafunga bao la Ushindi dakika ya 89 kwenye Uchaguzi huu 2020

Nilijaribu Kula mihogo wiki 2 mfululizo na dagaa aisee Ile kitu inashibisha hatari SASA tatizo muda wote usingizi kitambi cha hatari nimeacha SHS 1000 mihogo na dagaa unashiba kutwa nzima.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 Hii ni kweli kabisa?
 
Ninachokiaona Membe amejaribu kukwepa mishare ya NEC
kama angesema anamuunga mkono Lisu huwezi kujua NEC wangesema nini. To me he is smart guy maana ni mgombea gani asiyefanya kampeni!!
Chochote NEC wangesema, still Membe hana cha kupoteza kama kweli anasupport msimamo wa chama. NEC wakimfungia kufanya kampeni, hapo si ndiyo ingekuwa faida kwa ACT na msimamo wao wa kumuunga mkono Tundu Lissu? Membe hajielewi yule.
 
Zanzibar wapo laki nne na sitini elfu tunapiga siku mbili lakini wenzetu wapo Milioni 29 wanapiga siku moja.
 
Chochote NEC wangesema, still Membe hana cha kupoteza kama kweli anasupport msimamo wa chama. NEC wakimfungia kufanya kampeni, hapo si ndiyo ingekuwa faida kwa ACT na msimamo wao wa kumuunga mkono Tundu Lissu? Membe hajielewi yule.
No NEC wasingefungia ACT tu wangemlenga Lissu kwa kusema mmefanya muungano haramu
So tusimlaumu Membe lets read between lines
 
Wakuu, Hakiki B.K.M Ni Mbobevu,
Na hakika vyama mbadala vinahitaji zaidi kuwa namna walivyo kuliko kuungana.

Nimemsikiliza kwa umakini Sana Leo.

1: Amenusuru vyama mbadala Sana.
Kwa kuto jitoa kwake Kunalinda vyama mbadala,
Amebaki kama mbadala endapo T.A.M.L akitolewa kwa hujma,
Basi upepo wote unageukia kwake.

2: Amezungumza mambo mazito
Mf: kushauri tarehe za upigaji kura Zanzibar,

3: Amekuja tofauti na wengi walivyotegemea.
Namna anavyozungumza ni kiukomavu zaidi, kwa kumsikiliza haraka haraka ni vigumu Sana kumuelewa.

Yote kwa yote NEC na ZEC pimeni ushauri wake, endapo kuna haja ya kuufuata ufuatwe.

Kumb: kufuata ushauri ni hiari, ila majuto ni mjukuu
 
Membe kasema urais ni wake au wa TAL tu, maana ngome ya CCM tayari wameishaivunja! CCM ni kama nyuki kutwa kutengeneza asali(miundo mbinu) hata kama ni tamu kuna vingine pia (nyongeza ya mishahara, fao la kujitoa nk )vinahitajika kuwepo, Jamani dakika ya 89 twende na TAL!!
 
Nimeamini Membe kweli ni Jasusi Mbobezi. Goli la dakika ya 89 huwa linauma kuliko x-pen...ameongea kitaalam zaidi kuruka kiunzi cha NEC maana walikuwa wanasubiri tamko lake tu wavifungie hivi vyama viwili[emoji122][emoji122][emoji122]hongera sana Jasusi. Mtego umeutegua kuwaokoa wenzako. Hapa ni akili kubwa tu zinaweza kuusoma mchezo
 
Wengi kwa sasa hawana akili ya kutosha yakumuelewa Membe, Wasubiri dakika ya 89
Uko sahihi, Watu hawajamuelewa Membe. Bado nasema he is trying to act smart.
Anachofanya ni kushambulia ili kum cover mwenzio aingie sehemu fulani.

Kuna uhusiano mkumbwa wa Maalim kuwa na Lissu leo na mkutano wa Membe na ameshasema Maalim na Zitto wanasema kama individual so yeye anatoa msimamo wa chama. Good cover up
 
Hivi ni mtu gani anayejiandaa kumkabili adui, halafu amuoneshe na kumuelekeza aina ya silaha atakayotumia kumuangamiza, Membe akalale inaonekana licha ya kuwa mkongwe kwenye siasa Kuna vitu hakujifunza.
 
Naona kaingia kama Dr Slaa na Lipumba walivyoingia uchaguzi wa 2015 kumpa ushindi JPM. Huyu jamaa hafai tena. Upinzani wa kweli utatoka huko huko upinzani na sio CCM
 
Tusubiri muda unavyoenda tunaendelea kujua na kujifunza zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…