Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Nafunga bao la Ushindi dakika ya 89 kwenye Uchaguzi huu 2020

Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Watanzania mkae macho na mkae chonjo. Nafunga bao la Ushindi dakika ya 89 kwenye Uchaguzi huu 2020

Hatuwezi kufua nguo za ndani mbele za watu.
Membe: Nikiambiwa nirudi CCM siwezi kurudi
Ukishakuwa mteule wa Urais, kisheria hairuhusiwi kuseme unamuunga mkono rais fulani wakati na wewe ni mgombea wa huo urais. Ukisema hivyo unatakiwa upelekwe Milembe

Huyu Mzee ni mtata nimeishia kucheka tu simwelewi kabisaaaaa!!!

Hata Lowasa alisema hatarudi CCM na Sumaye naye alisema hayo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hesabu ya Mhe. Membe ni ngumu kidogo; yaani, 90bin*4=270bin (25:25-26:20).

 
Kuna uzi niliuleta hapa juzi ila ukabaniwa haukupita.

Kuna siri kubwa katika mipango ya ACT na CHADEMA lakini kwa maslahi mapana ya ushindi wa Lissu nisingependa kuyasema.

Kiufupi kuendelea kuwepo kwa Membe kwenye karatasi ya kura kuna baraka ya vyama vyote viwili. Jamaa amewekwa kimkakati zaidi.
Acha kupotosha wewe huna lolote,wee kidampa wa nanjilinji,eti ushindi wa Lissu Mara siri kubwa,huna haya
 
Kazungumza mambo mengi lakini nilichokiona ni hatari ya kuwapandisha viongozi wa dini kwenye majukwaa ya kisiasa.

Chadema wanakosea Sana, hiyo ndio tunaita political immaturity.
CCM haikumpandisha shekhe wa mkoa dsm.?.Au alikuwa hamuombei kura Magufuli?.
 
Salaam Wakuu,

Leo Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Ndugu Bernard Membe anaongea na Wahariri wa Vyombo vya habari Jijini Dar...
Jamani ukweli uko wazi korona imetingisha uchumi wa dunia nzima tena hapa Tanzania tuna nafuu, nenda hapo jirani kenya uone uchumi ulivyotetereka , wanalia , ulaya na Marekani ndio kabisaa .
 
Wapinzani gani hawa wasiojua mbele wala nyuma? Leo wanasema wanamsapoti Lisu, halafu anaibuka mwingine anasema mimi ndiyo mgombea urais wa ACT. What is the better way to describe this attitude than UTOPOLO at its best?
Ila we kidada una shobo had sio poa ,alaf unajisifu hapa et nimeaoma ulaya ,sijui mm genius wakat hata kureason tu hujui .
Mm nakuona Kama kijibwa kidogo Cha ccm kinachojifunza kubweka 🦮🦮.

Alaf acha kutisha watu kizembe namna hiyo ,ww Ni kijibwa fulani kimasikin kinachotaka kujikwamua maisha kwa kulamba makalio ya Wana siasa coz ili maisha yako yasogee lazima ushinde hapa kutetea hao inzi wa kijana[emoji867][emoji867]
 
Nimemsikiliza Membe. Ile kuanza tu yeye na Polepole na Bashiru. Kwenye mkutano Bagamoyo Mh Rais Msataafu Kikwete na Mwanae wamemzodoa Polepole.

Unganisha uone watu hawa watatu what they share in common?

Mh Rais wangu JPM kuwa muangalifu na kitu kinaitwa sangarara. Usizungwe na tabasamu. Membe kasubiri siku zote hizo za kampeni. Mmeshajiuliza kwa nini leo ndio kajitokeza? Na kajitokeza hisia ya kwanza kuonesha ni kuwashambulia watu uliofanya nao kazi chamani kwa kipindi cha Uenyeketi wako hadi hapa mlipo leo. Membe anatakakuonesha kuwa JPM, Bashiru na Polepole ndio wanao kipasua chama. Huu mheshimiwa ni moja ya mitihani mikubwa ulio kufikia. Dawa pekee hapo ni kuonesha msimamo ukiepelekwa na upepo wa propoganda hali itakuwa si hali.

Labda niongezee kura zako ulishazipata kipindi chote cha miaka hii 5 ya utendaji wako. Hakuna kura za maana zitakazo ongezeka kwa hizi wiki mbili tatu za kampeni.Sana sana utaishia kuwa exposed kwamba huna msimamo.
 
Chochote NEC wangesema, still Membe hana cha kupoteza kama kweli anasupport msimamo wa chama. NEC wakimfungia kufanya kampeni, hapo si ndiyo ingekuwa faida kwa ACT na msimamo wao wa kumuunga mkono Tundu Lissu? Membe hajielewi yule.
Kuna maslahi ya Zanzibar na wabunge na madiwani. Huwezi ruhusu chama kipate matatizo sasa.
 
Back
Top Bottom