The hammer
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 2,397
- 1,786
Habarini watu wa Mungu, mimi ninavutiwa kufanya biashara ya kuuza mbao Nairobi, mtaji kwangu suo tatizo sana, msaada ninaohitaji kwenu ni process za kupata kibali, kama kuna mtu anafaham utaratibu mzima wa kibali au taratibu nyingine zinazohusiana anisaidie tafadhali.
Asanteni sana
Nimecheka sanaaaHawa watu wa Pm hawa sometimes huu ni ulemavu
tushirikishe na wengine hapa kwa manufaa na ya wengine pia...Hiyo Biashara Nina Idea nayo ni PM Nita kumpa guidance.
Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.
Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.
Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.
Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.
Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Eucalyptus sio miti mizuri kupanda sababu inakunywa maji Mengi sana na kuleta ukame eneo husika sikushaur upande tena Ila pines, grevillea, casuarina Montana ni bora zaidi.Mimi nigependa kuwahamasisha wanJF kupanda miti ya mbao hasa mbao nyeupe (pines and cypress). Miti hii inasitawi sana sehemu za nyanda za juu kusini.
Mimi nilianza kupanda miti hii kama miaka kumi iliyopita. Nimepanda miti mingi kila mwaka bila kukosa. Kwa sasa ninazo ekari nyingi za miti hii. Vile vile miaka ya karibuni nimepanda eucalyptus.
Wakati naanza kupanda miti mche mmoja nilikuwa nanunua kwa Shs 50 na kuupanda kwa Shs 20. Kwa vile napanda miti mingi (zaidi ya laki moja kwa mwaka) baadaye niliamua kuotesha miche mimi mwenyewe ili kupunguza gharama.
Gharama zaidi ya miche na upandaji ni barabara za moto kuzunguka msitu. Hata hivyo nilinunua ngómbe na kuwaweka kwenye shamba ili wale majani yanayozunguka msitu. Wamenisaidia sana.
Unaweza kupanda miti kidogo kidogo kila mwaka kutumia mshahara wako kama nilivyofanya mimi. Baada ya miaka kadhaa utakuwa na miti mingi na utaweza kuwa unauza miti au kupasua mbao kila mwaka.
Wakuu habari za majukumu. Mimi pia ningependa kupata shamba kuanzia ekari 20 hadi 50 haswa lililooteshwa miti tayari. Wasiwasi wangu ni kupigwa/kutapeliwa. Je ninaweza kufanyaje nipate shamba kiuhalali na kisheria? Ninaomba kama kuna mtu ana shamba tayari maeneo ya Njombe au Kilolo ambaye anaweza kunisaidia kupata shamba kihalali nitashukuru sana.
Eucalyptus sio miti mizuri kupanda sababu inakunywa maji Mengi sana na kuleta ukame eneo husika sikushaur upande tena Ila pines, grevillea, casuarina Montana ni bora zaidi
Bahati mbaya kwa sasa hivi sipo maeneo kwa hiyo ni vigumu kukuelekeza. Naomba umpm Malila yeye mara nyingi huwa anakwenda maeneo hayo.CC Malila
KVM
Malila Njoo basi utusaidie kuhusu kuuziwa shamba za miti please mkuu.Bahati mbaya kwa sasa hivi sipo maeneo kwa hiyo ni vigumu kukuelekeza. Naomba umpm Malila yeye mara nyingi huwa anakwenda maeneo hayo
Ila tu kwa uzoefu wangu wengi wanaouza mashamba yenye miti huwa wamepanda eka chache kama moja, mbili hadi tano. Wanaouza zaidi ya eka 20 ni wapandaji wakubwa na wapo wachache. Ila kwa hali ya sasa unaweza kuwapata baada ya mianya mingi ya mapato kuzibwa. Malila
Malila njoo basi utusaidie kuhusu kuuziwa shamba za miti plsssss mkuu
Ni kweli najishughulisha sana na hii project, kwenye hii project kumeingia vibaka, tena wengine wanapata hata nafasi za wazi za kupiga wasiojua. Hata mimi nimeshapigwa, kwa hiyo najua. Sasa hivi usikubali kununua shamba la familia bila kupata document ya kikao cha familia husika. Ukisikia shamba la miti linauzwa inabidi uchunguze sana, unaweza kuta muuzaji analiuza sababu lina mgogoro ambao wewe hutauona mapema, shamba la hivyo inabidi utafute ushahidi wa kutosha, au lilikosewa kuoteshwa,au uvunaji wake utakuwa pasua kichwa nk. Ukisikia hili shamba linauzwa na muuzaji anashida sana, fungua macho.
Mashamba yanayouzwa na vijiji achana nayo, yanasumbua sana. Usikwepe kulipa ushuru wa kijiji, kisha chukua pay slip, kila kitu kifanyike ofisini mchana kweupe, na malipo kama ni hela nyingi, pitishia benki.
Naweza kuwasaidia kupata mashamba ya kuotesha miti kwa bei nzuri sababu nafahamu yalipo na mimi nipo hapo, naweza kuwasaidia kupata mashamba yenye miti tayari ( Mufindi/Kilolo/Njombe) katika maeneo nilikootesha mimi, sababu wauzaji wa mashamba ktk vijiji niliko walau naweza kupata taarifa sahihi.
karibuni.
Kwa sasa nafanya coordination ya upandaji miti kwa wadau 410, wengine wamo humu na wengine wako nje ya jf. Msimu huu pekee tumeotesha miche milioni tatu na ushee, tumeotesha/nimesimamia kuotesha pines na mlingoti katika wilaya za Mufindi, Kilolo,Njombe na Madaba. Bei ya chini bila kupita kwa dalali ni Tsh 70,000/ kwa eka katika maeneo yasiyo na miundo mbinu. Na maeneo yenye miundombinu bei inafika Tsh 120,000/ kwa eka. Miche na manpower naweza kukusaidia.Shukrani kwa kujitolea kutoa elimu ya bure mkuu, najua kama ukipata wafuasi huenda wengine wakawa wateja wako ukatuuzia miche. Kwa sasa heka moja isiyopandwa inaweza kwenda kwa kiasi gani? Na wewe unazalisha miti ya aina gani? Nikinunua miche kwako unaweza kufanikisha upatikanaji wa vijana wa kupanda japo kwa maelewano tofauti kati yao na mimi?
Shukrani.