Bila UMAFIA hujawa tajiri bado. Umafia ndio dira ya utajiri

Nimeliona hilo pia! Nipo nalifanyia kazi..lazima mbinu zote uzipitie za kujilinda kiroho na kimwili vinginevyo unalamba mchanga mapema wewe na uzao wako..
Maana hata kama kitu ni cha halali kinaenda kukupa utajiri utakutana na vita sio vya nchi hii.

Ni kazi kweli kweli..maadui kila kona kutoboa kufika pale..ni vita vikubwa ya Kiroho na kimwili, hakuna lele mama..ukifanya mchezo unalamba mchanga.

Vinginevyo ukubali kuishi ordinary life ya kupata hela ya kubadilisha mboga, kulipa kodi, au kanyumba kako kamoja..e.t.c
 
Mbona sijawahi kuyaona Kwa Mark Zuckerberg,Jeff bezos, warren Buffett,amancio Ortega, Bernad arnault, Elon musk , Na matajiri wengine.


Matajiri wengi wa bongo Hela zao ni za makando kando lazima uwe na roho mbaya
Amancio Ortega ni bonge la drugs dealer.

Mbona hujawataja akina Bill Gates, Abrahamovich au sababu ushajua walipataje pataje utajiri wao?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Matajiri wa kibongo ni utapeli, kuuziwa mali / mashirika ya umma, ushirikina, wizi, biashara haramu / mihadarati na nyingine nyingi... Matajiri wetu pesa zao walizipata ghafla tu na hata ukiwauliza ulianza je, hawezi kupa jibu la maana zaidi nilianza kuuza karanga, mara nilikuwa na fundi baiskeli 🤔 Yaani utajiri wao ni hiyo siri na kamwe hawezi kwambia.

Hakuna utajiri kwenye kazi halali..
 
Hapa umechapia mwanzo mwisho ...

Facebook ilianzishwa na marafiki wa tatu Na Mark zuckerberg akiwemo.

Mtandao wa Twitter hakuwa Mark zucker
 

Kuna Maskini wa Akili na Mali atabisha
 
😂Kuna matajri au kuna wanaoishi kitajiri ni vitu tofauti.


Yaani nisinunue kitu cha uhakika na nimekipenda kisa masikini?sasa hela kazi yake ni nn?
 
Tajiri kuingia peponi ni kipengele maana wengi wanafanya kazi nyingi na shetani kuliko Mungu. Wanaua just to get shit straight
😂😂😂Hii dunia kuna jamaa nilimsikia anasema kwamba eti tajiri hana chuki ..wakati wapo matajiri wanachukia hata wanaopata kidogo na wanapnga kuwadhulumu kabisa kile kidogo wakose kabisa...
 
Maskini ni tatizo kubwa. hayo mawazo mgando yanakuja ukiwa na njaa. njia za kumiliki hela halali zipo nyingi bila umafia.

Maskini akishafeli maisha huwa anaona kila mwenye hels ni tapeli.

Tafuta hela tu hayk mawazo mgando utayasahau
Nakazia
 
Umenena ukweli kabisa hasa hapo kwa facebook.
Kitendo cha kumnunua whatsapp ndio umafia wenyewe. Yaani hiyo ni mbadala wa kuua ila kisasa.
Ni sawa na kampuni ya bus ya Ally's akiamua kununua kampuni ya bus ya Katarama wakati wapo ruti moja ya Dar-Mwanza.
Huo ndio umafia wenyewe.
 
Hii sipingi mzee acha iende
 

Maana ya Umafia ni nini? inawezekana wengine tunachangia ila hatuelewi maana yake.

Meta alinunua Whatsapp, laiti wasingefanya hvyo basi whatsapp isingejulika na ingekufia mbali.

Kama mwenye wazo angeona itakuja kulipa wala asingeuza. na asingeuza isingefika hapo ilipo.

Youtube ilijulikana baada ya kununuliwa na google, laiti google wasingefanya hvyo basi isingekuwepo.

Alafu mara nyingi wamiliki ndo wanawafata wanunuzi kuwapa idea yao au biashara yao

Mfano musk alitaka kuuza Telsa. yeye ndo alimfuata mnunuzi
 
Kuna tajiri wa mabasi hapo Morogoro alinunua basi la kwanza akiwa under 20 tena akiwa anasoma. Baada ya miaka miwili akaongeza mengine.
Sasa jaribu wewe uone.
 
Mbona sijawahi kuyaona Kwa Mark Zuckerberg,Jeff bezos, warren Buffett,amancio Ortega, Bernad arnault, Elon musk , Na matajiri wengine.


Matajiri wengi wa bongo Hela zao ni za makando kando lazima uwe na roho mbaya
Fuatilia mkuu.... hao wote unaowataja ni mabingwa wa figisu. Sema figisu za wazungu zina majina tofauti tu

Umewahi kusikia vitu kama "Corporate Raiders", huyo Arnault uliyemtolea mfano ni mmoja kati ya watu waliopata utajiri mkubwa kwa figisu figisu nyingi kweli kweli.

Ukipata muda pita hapa


View: https://www.youtube.com/watch?v=q-Id8vXoqiE
 
Kwani twitter ilikuwa ya Mark???😳😳😳
 
Sio kwamba facebook alipoona whatsapp iliyoanzishwa 2009 inatamba na yeye akaamua kuanzisha facebook messenger mwaka 2011 ili ku-compete na whatsapp.
Alipoona bado whatsapp hakamatiki na hawezi kushindana na facebook messenger yake,
Mwaka 2014 akaamua kutumia nguvu ya pesa ili kuua ushindani, akamfata na dau kubwa akainunua whatsapp.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…