..Na RC ilikuwaje mpaka wakajuana na huyo anayedai ni " malaya aliyekubuhu " ?
..ndio maana nasisitiza RC ajitokeze na kueleza ukweli kuhusu nini kilitokea kati yake na huyo msichana.
just step into the shoes, umesingiziwa kitu cha ajabu kama icho, wewe ni Mwenyekiti wa ulinzi na usalama Mkoa mzima, RPC na Mapolisi wote wa kwako, RSO na TISS yote MKoa ya kwako, na wengine wote, wewe ni mteuliwa wa Rais. kweli usingiziwe kitu kikubwa kama icho halafu usichachamae, utulie kimya tu, uanze kupigia simu marafiki wa binti waombe msamaha, umeenda hadi chuo kutafuta rafiki zake, umeenda kwa mamake unatoa hadi 3m, unatoa 10m kwa binti. kwa deni gani? kwa kitu gani ambacho hukufanya hadi uhangaike namna hii? kweli angekuwa ametungiwa Polisi wangemkamata, Rais angemtumbua? kwamba Rais huwa anatumbua bila informations sahihi toka vyanzo vyake? just think.
Huyu jama kafanya, ndio maana anahaha kuhonga na kunyamazisha, una deni gani hadi uhonge na kuhangaika kama ulikuwa unadaiwa na icho kibinti cha chuo mwaka wa kwanza?binti wa 21 years ndio jamaa ahangaike hadi kuhonga?
Haya sasa RC atuambie, kama siku ya tukio hakuwa rock city, atoe ushahidi alikuwa wapi? alikuwa Geita au alikuwa Mwanza? analindwa na mapolisi, unafikiri mapolisi wakiulizwa na RPC waseme ukweli watasema uwongo? ndio maana huwa nawaambia hawa viongozi wanaolindwa na mapolisi, wale sio walinzi wako ni wachunguzi wako, wataeleza siku hiyo wapi ulienda, ulifanya nini na waliona nini na uliporudi kwenye gari ulikuwa unasemasema nini ulichotoka kufanya huko, wao wanaamini wale walinzi ni watunza siri wao. subutu.
yaani ninyi wateuliwa, ukiona umepewa mapolisi wanakulinda jua tukio likitokea hao walinzi wako ni wakwanza kuulizwa, wataulizwa siku hiyo ulienda wapi, waliona nini? waliona binti ameingia kwenye gari yako au la, na kama ni walinzi wako haiwezekani binti au yeyote aingie kwenye gari yako na walinzi wasikuone. nadhani hata Rais anachukua tu information toka kwa hao bordguards wako, wananyoosha maelezo. hata ukikutwa umekufa ujue hao walinzi ndio wakuulizwa. vivyo hivyo hata ukifanya jambo la ajabu, wataulizwa na watasema ukweli. mnaringa na vitambi ati mnalindwa kumbe mmejilisha kwenye mdomo wa mamba mjulikane zaidi. kalaga baho.