Binti yangu (miaka 24) anataka kuondoka nyumbani akapange

Binti yangu (miaka 24) anataka kuondoka nyumbani akapange

Labda ameshakutana na sitaki ndoa anataka kumpa ujauzito. Mwambie kuwa huo uhuru anaotaka una hatari zake, na ww mzazi hutakuwa na la kufanya zaidi ya kumsikitikia pale hatari hizo zitakapomwangusha. Mpe mifano hai unayoifahamu halafu muache aamue.
 
Habari wadu, Kama nilivyoaandika katika title nikuwa binti yangu anataka kuleft home AKAPANGE! hili Jambo limenishangaza Sana ukizingatia hapa nyumbani Kuna kila kitu na nahitaji yote Nampa je kunaweza kukawa na kitu nyuma ya pazia?
Daaah, miaka 24 nahis kuna kauhuru anakakosa, kama vile kurudi home mda autakao yeye, kula bata atakavyo yeye au rafiki zake tayari wameshatoka home wamepanga
 
Kuna uhuru anataka aupate. Mtoto wa kike akishaanza kuwa mkubwa yaani akivuka miaka 18 salama yake ni kuolewa na kuwa na mji wake ndipo mzazi utapata utulivu wa akili na umuombee atulie na akutane na mtu mtulivu. Kinyume chake atakapokwenda kujianzia maisha kiholela ni wanaume wachache sana huwa wanaamini binti anayeishi mwenyewe wengi huwa wanaonekana kuwa ni wahuni tu.

Na nje ya hapo anaweza kuwa na maisha ya kuzoea uhuru kiasi kwamba miaka mitatu tu ya kuishi kwa kupanga ikamharibu kitabia sababu atataka kuwa huru uliopitiliza mipaka ya kike hata akiolew atakuwa na viburi vya kujiamulia kuchelewa kurudi sababu ataona ni utumwa kufuata amri na maagizo ya mume wake.

Nadhani kama maisha ya nyumbani ni mazuri mwambie ajikaze tu avumilie maana hiyo kubanwa ndio kinga ya kumlinda. Wanawake wanaoishi kwa uhuru na kuliwa liwa hovyo huwa wana mwisho mbaya sana baadae kuliko wale ambao hata kama amechelewa kuolewa ila yupo chini ya himaya ya baba yake.
 
nakumbuka siku namwambia mama yangu nataka kua na chumba changu nje ya nyumbani nilijibiwa hivi hapa nyumbani hauko huru?? huli?? hulali?? unakwenda unakotaka uliwahi kuzuiwa?? uhuru gani mwanangu unaoutaka zaidi ya huo?? hapa kwangu utatoka ukiwa either umeolewa au umekufa ukiwa katika hali ya maiti


na ndio siku nilipogairi huo upuuzi.
Mama yako ni mwanamke anayejitambua sana. Na anakupenda sana. Asingefanya hivyo angekuwa amekutoa kafara.
 
nakumbuka siku namwambia mama yangu nataka kua na chumba changu nje ya nyumbani nilijibiwa hivi hapa nyumbani hauko huru?? huli?? hulali?? unakwenda unakotaka uliwahi kuzuiwa?? uhuru gani mwanangu unaoutaka zaidi ya huo?? hapa kwangu utatoka ukiwa either umeolewa au umekufa ukiwa katika hali ya maiti


na ndio siku nilipogairi huo upuuzi.
Ukisikia mama ndio huyo jibu wala sio refu maneno machache tuu, ila hahahaaaaa ukibishana nae hapo we kweli umepinda .
 
Back
Top Bottom