BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi

BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi

Jaji hatatoa uamuzi, mwanasheria wa serikali ataondoa shauri kabla ya uamuzi, mmekula sana Hela zetu kwa kisingizio Cha kumchangia Mbowe, Maria sarungi ana mabilioni kayaficha kwa kisingizio anakusanya Hela za Mbowe za kesi
Sorry this is low!
 
Nyota njema inaibukia Tanzania wiki hii!
Tumwombee Rais SSH hekima na busara airudishe nchi katika mstari.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia, amekutana na kufanya Mazungu na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Tindu Lissu.

Ni baada ya Lissu kuomba kuonana naye.

Walizungumzia mambo mbalimbali kuhusu usitawi wa Tanzania.

Pia, soma

1). Makamu wa Rais, Samia Suluhu amtembelea Tundu Lissu hospitalini Nairobi

2). Tundu Lissu afutiwa kesi zote za uchochezi
View attachment 2121277
View attachment 2121284View attachment 2121285
View attachment 2121326


Ukweli unauma Lissu ajamfuata Mama bali Mama kamfuata Lissu safari yote kutoka France lengo la siri ni hili. Vyombo vingine vya usalama hasa IGP alikuwa anasingizia siasa kwa kazi mbovu anayofanya
 
Mkuu hivi unajua kusoma?
Taarifa ya Ikulu inasema Samia amekutana na Lissu nchini ubelgiji baada ya kuombwa na Lissu akutane naye.

Kwa kukusaidia tu, fahamu haya:
1. Wito wa kukutana uliletwa na CHADEMA kupitia Lissu.
2. Mkutano umefanyika ubelgiji mahali anapoishi sasa Lissu.

Sasa tukuulize, BAVICHA wataumiaje kwa hili tukio wakati msingi wake umeanzia CHADEMA na umehitimishwa ndani ya CHADEMA?

Mkuu, wa namna hii waache! Uhasama inaonekana kwao kuwa ni “value” kama bidii, heshima nk. Unaweza ukaona upopoma - “Bavicha” hakutajwa popote katika taarifa ya ikulu lakini inatajwa kwa sababu kuna ulazima wa kuleta drama!!
 
Mbowe akitoka maabusu atamfukuza uanachama Lisu

Ndio siasa za roho mbaya mlizofundishwa na mwendazake?. Uwe na aibu basi, mnapenda siasa za kuuana na kutekana. Huo mida haupo umeisha. Tunataka tuishi kwa kuheshimiana kama watanzania na kila chama kupewa haki yake.
 
Wale waliokuwa wanagomea vikao na serikali hapa nchini wanachanganyikiwa, Lissu level nyingine, anajua maana ya Siasa, tofauti na mburura zilizo hapa nchini. Zitto kabwe alisema mapema, Chadema wakambeza, Sasa Lissu anafata muelekeo wa ZZK, anaachana na Chadema wenye mawazo mgando, ya kizamani, wanaimba katiba tu kama kasuku, mwenzao anaozea jela, wao wanakusanya Hela wanagawana.

Kama nyie wanaume mshambulieni Lissu mitandaoni tuone
Kuna mambo unatakiwa uyaangalie. Lissu yuko nje kwa kuhofia serikali ambayo mkuu wake ni Samia. Serikali inasemwa na Lissu huko ughaibuni na hii ni mbaya inatia doa. So, hii ina maana kuna uadui. Kwa kukutana kwao kuna faida kubwa kwetu sote ila wenye akili za mbuzi watashambulia tu vyama na kupandikiza chuki. Huu ni upumbavu sana.
Tuangalie tukio kwa upana na sio kiushabiki
 
Wale waliokuwa wanagomea vikao na serikali hapa nchini wanachanganyikiwa, Lissu level nyingine, anajua maana ya Siasa, tofauti na mburura zilizo hapa nchini. Zitto kabwe alisema mapema, Chadema wakambeza, Sasa Lissu anafata muelekeo wa ZZK, anaachana na Chadema wenye mawazo mgando, ya kizamani, wanaimba katiba tu kama kasuku, mwenzao anaozea jela, wao wanakusanya Hela wanagawana.

Kama nyie wanaume mshambulieni Lissu mitandaoni tuone
Yaani kuna watu wanaichukia chadema hadi basi kwahiyo unadhani ccm mtamnunua Lissu?
 
Bavicha hawana la kuomgea zaidi ya kuona giza angekuwa Zitto kakutana na Rais kama Lissu JF ingechafuka kwa matusi.
 
Ukweli unauma Lissu ajamfuata Mama bali Mama kamfuata Lissu safari yote kutoka France lengo la siri ni hili. Vyombo vingine vya usalama hasa IGP alikuwa ana singizia siasa kwa kazi mbovu anayofanya
Acha kujitoa ufahamu kamanda. Rais Samia anahudhuria kikao cha AU-EU kinachohusisha viongozi wengi wa Africa. Kubali tu kuwa Lisu katumia fursa kujipendekeza na kupiga magoti.
 
Ahsante Rais wetu kwa kuonyesha upendo.
Sasa wanachadema mnapaswa mjue kua siasa sio UADUI.
Tulijenge Taifa letu kwa pamoja tusonge mbele.
 
Ile lugha iliyotumika pale ni watu wachache waliielewa, huoni baada ya kunyoosha mkono kesho yake serikali iliona hakuna haja ya kuleta mashahidi wengine.

Mbowe alikubali kosa hivyo serikali imeona haina haja ya kuendelea kumshtaki, hivyo hivi karibuni anatoka mahabusu.
Angekubali kosa tena ugaidi si ni magereza straight? Jidanganyeni wenyewe, sisi no. Essence ya kumstaki ilikuwa akubali Kisa ili aachiwe huru au ni kumfunga? Hangaya alitakaga hadharani kwamba wenzake Mbowe walishafunga yeye tuu ndo kabaki.
 
Ni ushindi kwa Chadema au Ushindi kwa CCM iliyopo madarakani?
Ninadhani wewe ndio mburura haswa. Chadema na Lissu walitaka kupata a negotiated position, siyo msamaha wa Rais ambao hauna justification. Chadema atatoka hapa triumphantly. Judge ataamua kuwa akina Mbowe hawana kesi ya kujibu; Jamhuri ilipeleka mashitaka fake mahakamani. Ushindi kwa Chadema. Wale wabunge viti maalum wataondolewa Bungeni na kisha Chadema ipeleke walioteuliwa na chama chao kwa mujubu wa sheria. Mwenyekiti wa NEC tayari amekwisha kuondolewa. Ni ushindi kwa Chadema. Yote haya ni payoff ya msimamo wa Chadema; viongozi na wanachama wao. Siasa za heshima hazihitaji easy going, umalaya na kujipendekeza kwa watawala kama alivyotaka Zitto Kabwe.
Umeelewa chinembe?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia, amekutana na kufanya Mazungu na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Tindu Lissu.

Ni baada ya Lissu kuomba kuonana naye.

Walizungumzia mambo mbalimbali kuhusu usitawi wa Tanzania.

Pia, soma

1). Makamu wa Rais, Samia Suluhu amtembelea Tundu Lissu hospitalini Nairobi

2). Tundu Lissu afutiwa kesi zote za uchochezi
View attachment 2121277
View attachment 2121284View attachment 2121285
View attachment 2121326
Pongezi nyingi sana kwa Mh. RAIS kwa Mazungumzo yako na Mh TUNDU LISSU huo ni Mwanzo Mwema wa NCHI YETU kurudi alipoiacha BABA wa TAIFA.

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Samia rais wa watu,za chini chini ni kuwa lissu amempigia magoti na kumbembeleza Sana mama Samia amuhurumie Dj Mbowe na ikiwezekana amwachie huru,keep calm wafuasi wa Mbowe huenda wakatabasamu this week.
Kwahiyo unathibitisha yale madai ya kwamba mahakama zetu Tanzania hazipo huru?
 
naona wafia vyama wanaanza kutoana damu sasa.

la muhimu ni TL kakutana na Mama, wamefanya mazungumzo juu wa mustakabadhi wa mambo mbalimbali, next step TL will be back, Mbowe will be out and they will both get down to their business..

Angalizo: CCM wananamna yao ya kudeal na mambo, ukiifuata ndoano kifala unanasa, and the good thing siasa zao sasa ziko chini ya wasukuma kete wa saigoni..

Hakuna lolote. Imebidi CCM wa bow down kwa CHADEMA. Maana CHADEMA wamestick kwenye msimamo wao bila kuyumba.
 
Hiyo salamu ya kupigana viwiko mmh!
Halafu badaae tena mnashikana mikono duh.
 
Hapo sawa, tunataka kiswahili chetu kitumike. Nashauri Heading ya uzi iwe, "Lissu akubaliwa kuzungumza na Rais Samia S. Hassan, mazungumzo yafanyika"
Kama hujui ni the opposite. Rais Samia akubaliwa kuzungumza na Tundu Lisu na mazungumzo yamefanyika. Kama hujui mazungumzo yaliyofaka ndiyo nafasi ambayo mama amekuwa akiitafuta kwa udi na uvumba ili kusafisha mapungufu ya kiongozi aliyonayo. Bahati mbaya polisi bado wanakinukisha huku bongo. Kama Raisi hatafanya independent assessment kuhusu madhira yanayotokana na polisihapa nchini, hata hizo juhudi anazohangaika nazo zitakuwa kazi bure.
 
Back
Top Bottom