BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi

BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi

Japo unaandika kwa ushabiki wa kishamba ila ujue baada ya huyo samia kuapishwa chadema waliandika barua ya kuonana na rais lkn hawakuitwa.

Bali wapumbavu wa kiuvccm ndio waliokuwanasema na kauli za kusema rais hawezi kuonana na msaliti sasa hawo ndio uchungu wa mimba utazidi.
Inawezekana pia ni Rais ndiye aliyeomba kukutana na Lissu. Hilo of course hawawezi kuliweka wazi. Kwa jinsi Lissu alivyoongea na kuchambua kesi ya Mbowe jana siamini kama kweli ni yeye aliye initiate. Off course kama maongezi yamekwenda vizuri, Lissu hatakuwa na sababu ya kudisclose such info.
 
Acha kujitoa ufahamu kamanda. Rais Samia anahudhuria kikao cha AU-EU kinachohusisha viongozi wengi wa Africa. Kubali tu kuwa Lisu katumia fursa kujipendekeza na kupiga magoti.


Hata Kenya alikuwa anaenda kwa kitu kingine😂 sio ! Fungua macho acheni kuwa mbumbumbu. Hivi unajua kwamba hizi appointment zinapitia kwa kiongozi kenya na walitakiwa kuongea kwenye simu kabla ya mbowe kushikwa lakini wapambe wakabana. Lissu ndiye alipigiwa simu na kiongozi mkubwa kutoka kenya na kuambiwa ampigie Mama yaani Mama hawezi kuwaamini wapambe wake kwenye mambo ya siasa maana wana machafu mengi mkuu
 
Ingekuwa ajabu sana asingeonana naye na pengine kila mtu angeshangaa...

Whether we like it or not, na bila kujali udhaifu na mapungufu yake kama binadamu, Rais Samia ndiye kiongozi mkuu wa nchi yetu na kauli yake katika jambo lolote huwa ndiyo ya mwisho. Mungu amjalie na aone ukweli wa mambo upande wa pili yanayotokea ktk nchi yake...

Kitendo cha kuikataa roho mbaya ya chuki na ya kiuaji ya mwendazake John P. Magufuli na kuonana na huyu ndugu uso kwa uso na kuzungumza bila kujali kama ni Tundu Lissu ameomba au Rais mwenyewe ameamua hivyo, ni jambo jema sana na kupongezwa...

This is the new beginning ya CHADEMA. Hopefully pia wakimbizi wote wa kisiasa waliokimbia mdomo wa dictator John P. Magufuli na kukimbilia nchi za kigeni, mlango uko wazi sasa kurejea ktk nchi yao....

Hongera TL, hongereni CHADEMA na hongereni wana harakati wa haki za binadamu na utawala bora wote...
hiyo John P. ungemalizia tu POMBE
 
Kuna mambo unatakiwa uyaangalie. Lissu yuko nje kwa kuhofia serikali ambayo mkuu wake ni Samia. Serikali inasemwa na lissu huko ughaibuni na hii ni mbaya inatia doa. So, hii ina maana kuna uadui. kwa kukutana kwao kuna faida kubwa kwetu sote ila wenye akili za mbuzi watashambulia tu vyama na kupandikiza chuki. Huu ni upumbavu sana.
Tuangalie tukio kwa upana na sio kiushabiki
Mmetuchangisha sana Hela za kesi ya Mbowe na mlikuwa mnazuia isiishe, Sasa mtajuta, mmekula sana Hela kwa kisingizio mnakusanya kusaidia kesi ya Mbowe
 
Uamuzi wa Mhe. Rais kukutana na Mhe. Lissu ni uamuzi wa busara sana. Huo ndiyo upendo, mshikamano kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.
 
CHADEMA mtawakuta ACT WAZALENDO huko kwenye siasa za maridhiano walishatangulia.
Acha hayo. Samia alimtembelea Lissu Nairobi alipopigwa masasi na sasa amemtembelea ukimbizini. Hii ni healing elewa. Samia ameinyesha ubinadamu, ni mtu mwema. tatizo ni wapuuzi wa ccm wanaomjaza fitna.
Samia ni tofauti na mtangulizi wake kwa sababu anajaribu kubalnnce kati mabavu ya ccm na ukweli wa wa mambo. Samia hana ubaya ila tamaa ya ma ccm na walio na madaraka ndio kikwazo.. lissu ni mwelewa sana pia.
 
Tunataka ukweli na Maliziano ili kuliponya taifa na wale waliotumika vibaya wawajibishwe kwa mujibu wa Sheria za nchi
 
Mama atawashangaza Wengi sana mnaombeza!

Viva Mama Samia Suluhu Hassan.

#NyukiWaMama
Mbona alishawashangaza kitambo? Na bado watatoka macho nje gololi tu aisee. Huyu ndiyo Rais wa wote na alisema alipoapishwa. Anatekeleza. Yaani Mungu anipe uhai nifurahie maisha kipindi chake chote mpaka 2030. Huyo atakayeingia wala sitajali Sana maana by that time nitakuwa niko busy na vijukuu na vitukuu vyangu na kupata hot news JF.
 
Ile lugha iliyotumika pale ni watu wachache waliielewa, huoni baada ya kunyoosha mkono kesho yake serikali iliona hakuna haja ya kuleta mashahidi wengine.

Mbowe alikubali kosa hivyo serikali imeona haina haja ya kuendelea kumshtaki, hivyo hivi karibuni anatoka mahabusu.

Acha kujifanya mjuaji ile Ni mahakama sio maigizo. Mahakamani my akikubali kosa anaingia plea of guilty. Sasa wewe unaleta story za amenyanyua mkono kuashiria amekubali. Unaelewa maana ya kukubali?. Yani anakiri alitenda ugaidi. Sasa Ni wakati gani ambapo Mbowe amekiri ugaidi?.

Viongozi wetu wanapokubali kuvunja uhasama tuwaunge mkono, sio kuleta stori za huyu kakubali. Kama mnataka siasa za uhasama endeleeni nazo wenyewe lakini tunataka turudi kwenye Uhuru wa kisiasa tulio kuwa nao kabla dictator hajaingia.
 
Shauri zako, acha kujifanya CCM kindakindaki. Mwenyekiti wa ccm kakutana na Makamu Mwenyekiti wa Chadema kuyajenga, wewe unatultea story za George Soros wa marekani. Tatizo nyie watu wa Chini ndio mnaojifnya kuipenda CCM wakati watoto wakubwa wanapewa uwaziri.

Mimi siyo CCM na wala sijawahi kuwa ila naelewa jinsi Dunia inavyokwenda na naweza ku connect dots, Tanzania siyo ya kwanza kufanyiwa umafia.

Ila kumekaribia kukucha, soon chadema watamjua Adui yao ni nani na kwa nini Mbowe yuko Jela, halafu bado kuna tifu litakuja la akina Makamba Zito vs Tundu Lisu kugombania power walioahidiana.

Kumbuka pamoja na chadema kumchukia Magufuli lkn Magufuli hakuwahi kumfunga Mbowe hata siku moja, Mbowe kafungwa na Uongozi wa Samia, sasa kwa nini ?

Go figure …
 
Back
Top Bottom