Bungeni Dodoma: Rais Magufuli avunja Bunge la 11. Asema ajira 6,032,299 zimetengenezwa, Viwanda vipya 8,477 vimeanzishwa

"Sangara kwenye Ziwa Victoria wameongezeka kutoka Tani 417,936 hadi Tani 816, 964, urefu wake umeongezeka kutoka wastani wa CM 16 hadi CM 25.2 na hivyo samaki wetu kuanza kuhitajika katika soko la Ulaya na ndege zimeanza kuja Mwanza na kubeba" - Rais @MagufuliJP #JPMKuvunjaBunge
 
Pale wanapoimba,kusimama na kupiga makofi tuna imani na Magufuli ukiwa mpinzani utasimama au utaendelea kukaa
 
Muheshimiwa anaogopa sana matusi,,,,,,,,,,sijui kwa nini.
 
Sawa lakini Nyerere alikuwa anasoma hizo points ndio aendelee kuhutubia, na hituba za nyerere nyingi hazikuwa na takwimu lukuki kama hii ya Magu.

Hotuba ya Magu imejaa takwimu nyingi sana ndio maana nimesema siyo rahisi kukariri hotuba ndefu yenye takwimu nyingi hivyo.
Hotuba zake nyingine nyingi tu huwa hasomi, lakini hotuba kama ya leo siyo rahisi kukariri.
 
Ila ni kama mda unavyoenda siku hadi siku anaongea kwa upole kidogo na busara au kwa vile ni bungeni na kuna viongozi ,maana kule mikutano ya mtaani hachelewagi kuchafua hali ya hewa
 
Hicho sio kikohozi cha kubana hewa, ni kikohozi cha kuumwa. Kina muda sasa toka akiwa Chato.
kwani yeye ni nani hata asiumwe. aumwe na afe tu kwani ndio njia ya binadam, kikubwa ni kujitibia ukiumwa sasa povu kuwa anaumwa la nini?
 
Huyu spika bhana eti asiyepiga makofi mchawi ,sasa wapinzani wampigie makofi kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…