Bwana Tundu Lissu, Hoja ya Chato na Maendeleo ya sasa inajibika Kimantiki

Bwana Tundu Lissu, Hoja ya Chato na Maendeleo ya sasa inajibika Kimantiki

..unasema Chato na Bukoba ni karibu, na Bukoba kuna uwanja wa ndege. Basi kwa msingi huo hakukuwa na haja ya kujenga uwanja wa ndege wa Chato. Zaidi, kama uwanja wa ndege wa Mwanza una matatizo wangeweza kutumia uwanja wa ndege wa Bukoba. Uwanja wa ndege wa Chato umejengwa kwa ajili ya kumfurahisha Bwana mkubwa na haukuwa kipaumbele cha Watanzania.
Kuwa muelewa,nilitaka kumfafanulia huyu dogo kuwa distance sio sababu kutojenga uwanja wa ndege.

Kumfurahisha ili iweje? Kwani ataishi milele?
 
Kijiji kimoja kijulikanacho kama Chato ndani ya miaka mitano kimefanyiwa yafuatayo tofauti na kijiji kingine chochote Tanzania:-

1. International airport imejengwa
2. Taa za kuongozea magari barabarani zimewekwa.
3. Chuo cha utumishi wa umma kinajengwa.
4. Uwanja wa kimataifa wa michezo unajengwa (kijijini!)
5. Mabenki yamejengwa
6. Hospitali ya kimataifa ya rufaa inajengwa.
7. Mbuga ya kimataifa ya wanyamapori imeanzishwa.
8. Dhifa za kitaifa za kuwapokea wakuu wa nchi na serikali zinafanyika.
9. Viongozi wakuu wa nchi wanaapishwa.

Ni katika kijiji kipi kingine Tanzania japo robo ya hayo yamewahi kufanyika? Halafu huoni tatizo? Hata kama ni kunywa maji ya kijani sio kwa upofu huo!
Mbona mkoa mmoja wa kaskazini ulipewa barabara za ramani, maji,na hata wazawa wa mkoa huo walisambazwa mikoa yote na kukiuka idadi ya quota system?
Acha unafiki,Tanu aka CCM ndio iliruhusu watu wa mkoa huo kuja Dar bila kibali,kwani Mwingereza aliwapiga marufuku.
 
Wamepita marais wangapi kwanini hawakukumbuka kwao?wali delay au walikuwa wabinafsi
Mtu kwao bwana ......kwa mwafrika

Ova
Wangekuwa wabinafsi wangejenga kwao!Sasa siasa za nchi hii zinachukua sura mpya,tutaanza kuchaguana kikabila ili tu maendeleo yawahi maeneo ya ukanda wa kabila la Rais!Huku ndiko mnataka tufike?
 
Mbona mkoa mmoja wa kaskazini ulipewa barabara za ramani, maji,na hata wazawa wa mkoa huo walisambazwa mikoa yote na kukiuka idadi ya quota system?
Acha unafiki,Tanu aka CCM ndio iliruhusu watu wa mkoa huo kuja Dar bila kibali,kwani Mwingereza aliwapiga marufuku.

..miradi ya maendeleo isambazwe ktk mikoa yote ya kanda ya ziwa siyo kupendelea kijiji na jimbo la bwana mkubwa.
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi
Rais Mstaafu Kikwete bado yuko hai na ni miaka 5 na miezi 3 tu iliyopita alikuwa madarakani, lakini sina kumbukumbu, na nakiri sikubuki ni lini Dhifa ya Kitaifa ilifanyika Msoga.
 
Tujiandae watanzania na upinzani ambao unageuka kua adui wa taifa. Hakika mtu kama lissu kwa sasa tunaweza kumwita adui wa taifa maana anatekeleza ajenda ya mabeberu dhidi ya nchi yake bila aibu. Hiyo makala aliyoandika imejaa uzandiki na uongo mtupu.
Kwamba hakuna hata kimoja chenye ukweli kati ya aliyosema.
1.Hakuna uwanja wa ndege wa kimataifa kijijini Chato.
2.Hakuna Hospitali ya rufaa Chato kijijini

Utetezi ni kwamba vyote hivyo vimejengwa nchini, sijajua kama Mobutu alijenga Morocco, au Zuma alijenga India.
 
..miradi ya maendeleo isambazwe ktk mikoa mingine ya kanda ya ziwa.

..siyo haki kulundika miradi mingi kiasi hicho kijijini na jimboni kwa bwana mkubwa.
Miradi mingi kama ipi imerundikwa Chato?

Mikoa mingine kanda ya ziwa haipelekewi miradi ya maendeleo? Unaifahamu Mara vizuri kabla ya 2015?
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi

Kuna dalili zote kuwa hujamwelewa Tundu Lissu...

In fact , unajibu hoja za TL kwa hasira za "tofauti za kiitikadi za kisiasa" tu na si kwa sbb ya hicho unachosema "upotoshaji"...

Unasema Magufuli asilinganishwe na kina Mobutu Seseseko, Dr. Hastings Kamzu Banda, Felix H. Bouigny na wengineo...

Na unasema kuwa lengo la kitabu la Peter Kenyon, "Dictatorland: Men Who Stole Africa" hakizungumzii viongozi wa aina ya Magufuli ambao lengo lake ni kuwaletea maendeleo watu nadhani kwa wewe kufikiri hawa wanaotajwa kwenye kitabu hicho hawakuwa na lengo hili: kuwaletea wananchi wao maendeleo..

Unaendelea kutetea hoja yako kwa kusema, kuwa, kitabu hicho kinazungumzia viongozi walioiba na kujitajirisha kupitia rasrimali za nchi zao na John Pombe Magufuli hawezi kuingia kwenye kundi la viongozi hao kwa vigezo na sababu anazozitaja Tundu Lissu na kinachofanyika Chato kijijini kwa Rais Magufuli...

Kwanza pole sana kwa sababu unadhani viongozi madikteta wezi huufanya wizi wao kama wezi au vibaka wa kawaida wanaovamia na kuvunja benki na kisha kukwapua mabegi ya pesa...

Laiti ungejitendea haki kwa kusoma kwa umakini uchambuzi wa Tundu Lissu na kisha uka - acknowledge tu na ukatulia, ungekuwa na busara sana....

Lakini Bahati mbaya kivuli cha itikadi za kisiasa zimekufunika na unaonekana u - kipofu wa fikra na kwa hiyo huwezi kuona chochote kizuri toka kwa watu wengine mnaotofautiana nao kiitikadi hususani mtu kama Tundu Lissu...

Nikuulize swali hili moja: Hivi wewe unadhani Rais Magufuli ni mtu mzuri na mtakatifu sana eti eeh...?

Pole sana. Sijui utajibu nini. Lakini najua ni vilevile tu. Nami nakuambia, UNAJIDANGANYA wewe na nafsi yako. Ninachoweza kukushauri, endelea kumwombea kama kiongozi wako ili arudi njia kuu, atoke kwenye upotofu, ukaidi na aache roho ya tamaa na uuaji...!

Ukifanya hivi, utakuwa unamsaidia sana...

Rais Magufuli hana tofauti na hao kina Felix F. B, Dr Hastings Kamzu Banda, Mobotu na wengine wanaosemwa na Peter Kenyon ktk kitabu chake...

Kwa kuwa Magufuli humuoni kusafiri nje ya nje unadhani siyo mwizi, ni mtu mwema sana na anawajali wananchi wake...

Deogratius Mutungi, dictator huwa haibi kwa njia hiyo unayodhani wewe...

Viongozi madikteta huiba kwa kutumia mifumo dhaifu ya kiutawala ya kiserikali na kinchi ambapo ktk uchambuzi wake Tundu Lissu amefafanua na kueleza kwa uzuri na urahisi sana kwa mtu yeyote mwenye akili na ufahamu mzuri kuelewa...

Dalili zote za dikteta mwizi ni haya anayoyafanya Rais Magufuli kwa kutupa kwenye dustbin vipaumbele vya kitaifa na kufanya maamuzi yake binafsi na kuyasimama kama vipaumbele vya taifa...

Viingozi wezi na madikteta hawajali sheria wala katiba. Kauli zao na maamuzi yao binafsi ndiyo sheria. Huyu ndiye Magufuli. Kwanini huoni hili...??

Viongozi madikteta mfano wa Magufuli, huendesha vikundi vya maauji, utekaji, na torture ya wapinzani wao kwa siri kubwa. Huyu ndiye Magufuli. Kwanini huoni na kuamini...??

Viongozi madikteta wa aina ya Magufuli wana hasira, hujipenda wenyewe, hawapendi watu wengine, ni wabinafsi na ma - ant-democracy. Huyu ndiye Magufuli. Kwanini huoni hili wewe...??

Hawa kina Mobutu, Houpgheiny - Bouigny, Kamzubanda na wengine ndivyo exactly walivyofanya...

Ngoja siku watu waje kuja na orodha ya mali na account za benki za kwake, rafiki zake, na ndugu zake zenye mafedha huko ndiyo utakuja kushangaa na kuishia kujijutia kwa kusema..

".....ala kumbe nilikuwa natetea shetani badala ya malaika bila kujua..!!

Pole sana. By then it could already been too late...!!
 
Miradi mingi kama ipi imerundikwa Chato?

Mikoa mingine kanda ya ziwa haipelekewi miradi ya maendeleo? Unaifahamu Mara vizuri kabla ya 2015?

..International Airport.

..Hospitali ya Rufaa.

..Ofisi za Mahakama.

..Uwanja wa mpira wa kimataifa.

..Ofisi za Tra.

..Ofisi za Msd.

..Chuo cha Veta.

..Benki ya Crdb.

..siyo haki kujenga miradi yote hiyo ktk jimbo moja wakati majimbo mengine ktk kanda ya ziwa nayo yana uhitaji.

..hakuna jimbo lolote lile ktk kanda ya ziwa ambalo limepewa miradi mingi ya maendeleo kama ilivyofanyika Chato.
 
Mbona mkoa mmoja wa kaskazini ulipewa barabara za ramani, maji,na hata wazawa wa mkoa huo walisambazwa mikoa yote na kukiuka idadi ya quota system?
Acha unafiki,Tanu aka CCM ndio iliruhusu watu wa mkoa huo kuja Dar bila kibali,kwani Mwingereza aliwapiga marufuku.
... jibu hoja acha vioja.
 
... kwa hiyo ni nguvu za wananchi wa Chato zinatekeleza miradi yote ile tena ndani ya muda mfupi baada ya "hamasa kubwa"?
Ni nguvu ya wananchi kwa kutumia kanuni za nchi kufika hapo walipo. Wanachato wamejipanga kimaendeleo kwa kutumia sheria zilizopitishwa na bunge. Hakuna upendeleo hapo.

Je hujawahi ona majimbo mawili ya uchaguzi, yanayofanana kijiografia yanaweza kutofautiana kimaendeleo kutokana na aina ya usimamizi wa mbunge waliomchagua?
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi
Watanzania hatupenda Sana kujua jambo na sababu zake. Mbali na ukweli kwamba Chato ipo Tanzania, zipo zababu muhimu Sana za maslahi ya kitaifa juu ya kinachoendelea Chato. Kwa bahati nzuri Leo asubuhi tulijadili hili hapa hapa JF.

 
Wangekuwa wabinafsi wangejenga kwao!Sasa siasa za nchi hii zinachukua sura mpya,tutaanza kuchaguana kikabila ili tu maendeleo yawahi maeneo ya ukanda wa kabila la Rais!Huku ndiko mnataka tufike?
Yule aliyetoka kusini kwao watu walimsema
Oh mbona kuko ovyo
Tatizo sisi wanadamu hatueleweki kabisa

Ova
 
Back
Top Bottom