Bwana Tundu Lissu, Hoja ya Chato na Maendeleo ya sasa inajibika Kimantiki

Bwana Tundu Lissu, Hoja ya Chato na Maendeleo ya sasa inajibika Kimantiki

Kijiji kimoja kijulikanacho kama Chato ndani ya miaka mitano kimefanyiwa yafuatayo tofauti na kijiji kingine chochote Tanzania:-

1. International airport imejengwa
2. Taa za kuongozea magari barabarani zimewekwa.
3. Chuo cha utumishi wa umma kinajengwa.
4. Uwanja wa kimataifa wa michezo unajengwa (kijijini!)
5. Mabenki yamejengwa
6. Hospitali ya kimataifa ya rufaa inajengwa.
7. Mbuga ya kimataifa ya wanyamapori imeanzishwa.
8. Dhifa za kitaifa za kuwapokea wakuu wa nchi na serikali zinafanyika.
9. Viongozi wakuu wa nchi wanaapishwa.

Ni katika kijiji kipi kingine Tanzania japo robo ya hayo yamewahi kufanyika? Halafu huoni tatizo? Hata kama ni kunywa maji ya kijani sio kwa upofu huo!
Mkuu,kuna binadamu walitakiwa wawe "mifugo" badala ya wanyama au binadamu. Huyu ni kielelezo tosha.
 
Mbona ukiwa Chato ,Bukoba ni karibu lakini kuna uwanja wa ndege. Hujui uwanja wa ndege wa Chato unafaida nyingi ikiwa na matumizi ya dharula kama uwanja wa Mwanza kuna Tatizo.

Usipende kupinga kila jambo, akitoka madarakani mtakuja Chato kung'oa runway?

Kwani akitoka madarakani huu uwanja hautawanufaisha watanzania?
Ninajua una uwezo mdogo wa kuelewa mambo, nimesema kujenga uwanja wa kiwango hicho. Nimerudia zaidi ya mara kuwa uwanja wa kiwango hicho haukupaswa kujengewa umbali huo na uwanja wa Mwanza. Inaonekana umekuwa brainwashed kiasi huangalii mambo kwa mantiki tena, bali unalazimisha utetezi wa kijuha.
 
We mutungi, waliosema ni wengi,mbona umeelekeza majibu yako kwa lisu tu?
Hata huku mitaani wanasema,ulitakiwa kusema ngoja nitow ufafanuzi kwa watanzania tu.lisu Yuko huko wanakoishi watu.
 
Ninajua una uwezo mdogo wa kuelewa mambo, nimesema kujenga uwanja wa kiwango hicho. Nimerudia zaidi ya mara kuwa uwanja wa kiwango hicho haukupaswa kujengewa umbali huo na uwanja wa Mwanza. Inaonekana umekuwa brainwashed kiasi huangalii mambo kwa mantiki tena, bali unalazimisha utetezi wa kijuha.
Ahaaaa! Mwanza ni international airport,unataka iwe na backup ya airstrip?

Huu uwanja ungejengwa Kisarawe usingelalamika. Acha siasa za kizandiki
 
Yule aliyetoka kusini kwao watu walimsema
Oh mbona kuko ovyo
Tatizo sisi wanadamu hatueleweki kabisa

Ova
Mkubali sasa kuwa kuna upendeleo unafanyika Chato,baada ya hapo tutajadili hayo mengine!
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi
Hebu,
Toa vigezo vya kutojenga uwanja wa ndege Geita na badala yake kwenda kujenga Chato umbali wa kilometa takribani 90 ambako kuja population ya watu wasiozidi 130,000/- ilhali geita kuna population inayozidi 300,000 sambamba na wafanyabiasha wengi na wakubwa kuliko chato???

Tueleze sababu zilizopelekea kujenga hospitali ya rufaa chato wakati kuna nyingine ipo hatua za mwisho mjini Geita lakini mji kama tabora au kigoma hauna hospitali zenye sifa hata ya angalau geita??

kinachofanyika chato ni aibu kwa taifa.
 
Ahaaaa! Mwanza ni international airport,unataka iwe na backup ya airstrip?

Huu uwanja ungejengwa Kisarawe usingelalamika. Acha siasa za kizandiki

Pembeni ya Kilimanjaro airport kuna uwanja wa kiwango cha huo wa Chato kama Backup? Kumbuka Kilimanjaro ni mkubwa zaidi ya huo wa Mwanza. Hapa unajichoresha tu boss kwa Utetezi huu.
 
Pembeni ya Kilimanjaro airport kuna uwanja wa kiwango cha huo wa Chato kama Backup? Kumbuka Kilimanjaro ni mkubwa zaidi ya huo wa Mwanza. Hapa unajichoresha tu boss kwa Utetezi huu.
Pembeni ya kilimanjaro unamaanisha nini?
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi
Kuna hoja ya msingi hujaijibu,umekurupuka tu,
Swali liliulizwa,Kwanza hakuna ubaya anapotoka Raisi kuwa na vyote hivyo,swali je ni vipaumbele vya nchi?vipo kwenye irani?vipo kwenye mipango?au ni vipaumbele vya Raisi?Wilaya nzima Haina hata Timu ya mpira,unaenda kujenga uwanja wa mabilioni!?
Wakati inajengwa Mloganzira hospital,Uwanja wa Mkapa,na terminal three inapanuliwa hakuna aliyepiga kelele,hata mkazi wa Masasi,au Kyelwa,au N'gara,au masumbwe,u kalumwa,akisikia haimpi shida kuona kwamba Dar inapendelewa,
Sasa wewe unajenga uwanja wa Ndege Chato kwa shughuri gani za kiuchumi zilizopo ambazo zitaleta faida?
Tundu Lisu,ametoa mfano wa uwanja wa Ndege wa mpanda,ulijengwa wakati Pinda ni PM,Tena kwa mbwembwe,sasa hv,unaota nyasi,kupata hata Ndege moja kwa wiki,ni hanasa,haya ndio matumizi ya hovyo,wewe thibitisha airport ya Chato inaingiza pesa ngapi ukilinganisha na KIA.
Maiti ziliokotwa Coco Beach zikiwa kwenye viroba,azory gwanda,ben saa nane,wamepotea Kama upepo,.
Lisu alikula shaba 18!mchana kweupeee,Tena kwenye viunga vya bunge.harafu unasema jiwe hafanani na Mobutu!!
Mtoto wa Dada ndio boss hazina,Shemeji akapewa tenda ya kujenga uwanja bila kufata taratibu,kwa taarifa yako mwaka jana kwenye uchaguzi mtandao ulizimwa,Ili jiwe afanye yake,
 
Mkubali sasa kuwa kuna upendeleo unafanyika Chato,baada ya hapo tutajadili hayo mengine!
Hiyo ni nature ya mwadamu mkuu hata wewe ungekuwa kwenye nafasi kubwa ungependelea kwenu...lakini kama hauna ubinafsi na unapotoka!

Ova
 
Wangekuwa wabinafsi wangejenga kwao!Sasa siasa za nchi hii zinachukua sura mpya,tutaanza kuchaguana kikabila ili tu maendeleo yawahi maeneo ya ukanda wa kabila la Rais!Huku ndiko mnataka tufike?
Ukiona hivyo hawakupathamini kwao

Ova
 
Salaam Wana JF.

Nimesoma na kuona andiko la Bwana Tundu AM Lissu kutoka Ubelgiji akijenga hoja juu ya maendeleo ya vitu na watu ndani ya eneo la Chato anapotoka rais wa sasa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Sijaona mantiki ya Lissu kupotosha umma wa Watanzania dhidi ya maendeleo ya sasa kwa Chato. Aidha, kabla ya kujenga hoja zangu dhidi ya hoja za Lissu, nitumie jukwaa hili kukanusha upotoshaji wa kumfananisha Rais Magufuli na Madikteta wa Kiafrika akina Mobutu Sese Seko, Felix Houphouet-Boigny, Hastings Kamuzu Banda na wengineo, Kwa hoja hii Lissu umepotosha umma na awatake radhi Watanzania na Rais Mwenyewe, kamwe uwezi kuzifananisha sifa za Mobutu na JPM labda kama hujui uovu na ukatili wa Mobutu Sese Seko.

Aidha Bwana Lissu unaporejea Kitabu cha Peter Kenyon "Dictatorland, The Men Who Stole Africa" Anachokiongelea Mwandishi Peter kwa viongozi wa Kiafrika walionajisi nchi zao hakina uhalisia na kinachofanywa na Rais Magufuli kwa sasa ndani ya eneo la Chato, Mantiki ya Peter Kenyon ni kuwamulika viongozi waliotawala Afrika na kujitajilisha wao wenyewe kimaendeleo dhidi ya Umma yaani wenye nchi, Rais Magufuli anatajilisha Umma kimaendeleo badala yake binafsi ndipo hoja iliposimama hapa.

Bwana Lissu kama unavyojua ni ngumu sana kuzuia watu kusema lakini linapokuja suala la upotoshaji ni sharti tujenge hoja kuepusha kikombe hiki kutamalaki, Bwana Lissu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli katika Mkoa wa Geita wilayani Chato ni Jambo la kawaida kwa mantiki kuwa kusudio la Maendeleo hayo ni kwa manufaa ya Watanzania wote bila kujali eneo unalotoka, Umerejea awamu zilizopita ukiwataja viongozi wa awamu hizo nne kuwa hawakufanya kinachofanywa kwa sasa, Bwana Lissu nikujulishe kuwa kila nyakati na mambo yake.

Wakati wa Mwl. Nyerere alifanya kulingana na uhitaji na mipango ya wakati ule lakini pia alinyoshewa kidole na wakosoaji wake wa masuala ya maendeleo, Hivyo hivyo kwa Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwahiyo lawama za namna hii hazikuanza leo na kamwe huwezi kuzimaliza lakini zinapopotosha zinajibiwa kimantiki, hata hivyo kila utawala utofautiana kiutawala, tunachokiona sasa sio kile tutakachokiona awamu ijayo ya sita.

Tunge jenga hoja za kumushambulia Rais Magufuli endapo tu kama angekuwa anafanya maendeleo ya namna hii nje ya Tanzania, hata mimi ningeunga mkono hoja kwa kitendo hicho lakini kinachofanywa ni ndani ya ardhi ya Tanzania, Aidha ninge hoji na kukosoa endapo tu Rais Magufuli angekuwa anafanya kwa maslahi yake binafsi na familia yake, lakini kinachofanywa ni kwa maslahi ya umma, Je nongwa inatoka wapi? Au ni husuda tu wa kisiasa kwa sababu ya itikadi za vyama vyetu?

Bwanba Lissu unadriki kulinganisha Mobutu Sese Seko ,Felix Houphouet-Boigny na Rais Magufuli, Je unajua viongozi hawa walitumia kodi za walala hoi kufanya starehe na anasa nyingine za kufuru hata zilizokuwa kinyume na amri kumi za Mungu kwa kujenga majumba ya kifahari kwa familia zao na kuwekeza mapesa mengi kwenye makampuni yaliyo je ya mataifa yao, Kinachofanywa Chato ni uwekezaji wa anasa au kwa mustakabari wa maendeleo ya watu kwa kizazi cha leo na hapo badae? Je baada ya rais muda wake yote yaliyofanyika ndani ya geita yatakuwa mali ya serikali au familia ya Magufuli?

Je, hoja ya kupinga maendeleo ya Chato inatoka wapi na ina mantiki ipi? Hata hivyo bwana Lissu unapo ongelea kisa cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini bwana Zuma aligeuza kijiji chake cha Nkandla kuwa kama ambavyo Magufuli anaigeuza Chato Si kweli, Tuhuma za Zuma ni kujenga Jumba la Kifahari na baadhi ya mambo mengine ya anasa kwa kutumia kodi ya Wana Afrika Kusini badala ya kutumia pesa yake binafsi, na ndo maana mahakama iliamuru arudishe hela na akarudisha, Je ufanano wa Zuma na Magufuli upo wapi hapa bwana Lissu?

Nihitimishe andiko hili kwa kusema kinachoendelea mitandaoni kuhoji na kushambulia kile kinachofanyika Mkoani Geita wilayani chato kama kitu kisichokubalika kwa umma ni upotoshaji ambao sharti Watanzania tuupuuze na tuungane kwa pamoja kuendelea kuijenga nchi yetu katika dhana ya maendeleo na watu wake, Maendeleo hayana ukanda ilimradi tu kinachofanyika kiwe ndani ya ardhi ya Tanzania.

Deogratias Mutungi
Rais amehamia Chato kusimamia miradi ya kwao, unaposema itawanufaisha watanzania wote ni kuwafanya watanzania ni mabwege, ni vipi daraja lijengwe Chato mtu wa Katavi anufaike! Vivuko vinavyojengwa Chato havijawahi kuwanufaisha watu wa Kigoma, acha siasa za kitoto. Dodoma inahitaji haraka uwanja wa ndege na haitafaidika kwa uwanja wa Chato. Kama haki ingekuwa kama usemavyo basi hakuna sababu ya kujenga miradi sehemu tofautitofauti ingekuwa rahisi na nafuu miradi yote kujengwa Dar na nchi mzima kufaidika! Huu ni ujinga. Tetea mambo ya msingi usitetee huku wengine wamekuwa wakiomba zahanati na maji tangu Uhuru hawapati kwa sababu Rais hajatoka kwao.
 
Kuna hoja ya msingi hujaijibu,umekurupuka tu,
Swali liliulizwa,Kwanza hakuna ubaya anapotoka Raisi kuwa na vyote hivyo,swali je ni vipaumbele vya nchi?vipo kwenye irani?vipo kwenye mipango?au ni vipaumbele vya Raisi?Wilaya nzima Haina hata Timu ya mpira,unaenda kujenga uwanja wa mabilioni!?
Wakati inajengwa Mloganzira hospital,Uwanja wa Mkapa,na terminal three inapanuliwa hakuna aliyepiga kelele,hata mkazi wa Masasi,au Kyelwa,au N'gara,au masumbwe,u kalumwa,akisikia haimpi shida kuona kwamba Dar inapendelewa,
Sasa wewe unajenga uwanja wa Ndege Chato kwa shughuri gani za kiuchumi zilizopo ambazo zitaleta faida?
Tundu Lisu,ametoa mfano wa uwanja wa Ndege wa mpanda,ulijengwa wakati Pinda ni PM,Tena kwa mbwembwe,sasa hv,unaota nyasi,kupata hata Ndege moja kwa wiki,ni hanasa,haya ndio matumizi ya hovyo,wewe thibitisha airport ya Chato inaingiza pesa ngapi ukilinganisha na KIA.
Maiti ziliokotwa Coco Beach zikiwa kwenye viroba,azory gwanda,ben saa nane,wamepotea Kama upepo,.
Lisu alikula shaba 18!mchana kweupeee,Tena kwenye viunga vya bunge.harafu unasema jiwe hafanani na Mobutu!!
Mtoto wa Dada ndio boss hazina,Shemeji akapewa tenda ya kujenga uwanja bila kufata taratibu,kwa taarifa yako mwaka jana kwenye uchaguzi mtandao ulizimwa,Ili jiwe afanye yake,
Chukua like ya moyo wangu [emoji120]

Odhis *
 
Hiyo ni nature ya mwadamu mkuu hata wewe ungekuwa kwenye nafasi kubwa ungependelea kwenu...lakini kama hauna ubinafsi na unapotoka!

Ova
Ok,sasa tunaongea lugha moja!Chato inapendelewa kwasababu Rais anatoka huko!
Ova!
 
Pembeni ya Kilimanjaro airport kuna uwanja wa kiwango cha huo wa Chato kama Backup? Kumbuka Kilimanjaro ni mkubwa zaidi ya huo wa Mwanza. Hapa unajichoresha tu boss kwa Utetezi huu.
Arusha na Moshi kuna viwanja vya ndege ambavyo ni vidogo, viwanja hivi vilijengwa kwenye kila mji wakati wa ukoloni na KIA ukajengwa kushika nafasi ya hivyo viwili, usipotoshe.
 
Ukitoa ushabiki kichwani ukauweka pembeni ukabaki na akili Yako timamu utagundua Yanayofanyika huko kyato ni mbegu ambayo matunda yake yatakuwa ili uwe kiongozi wa eneo fulani Basi ni lazima pia uwe mzawa wa eneo hilo.

Watu wengi wataamini ili nipate maendeleo lazima nimchague wa kwetu. Naunga mkono hoja za Lisu, haya Yanayofanyika ni vipaumbele binafsi vilivyovikwa vazi la maendeleo.
 
Back
Top Bottom