CCM: Tunafuatilia mienendo ya viongozi wetu wanaopotosha umma, kwenda kinyume na maelekezo ya Mwenyekiti wetu

Suala la chanjo ya UVIKO ni ajenda ya ulimwengu mzima.

Kila atakayerefusha mdomo kuipinga huishia kufa au kuanguka publically.

Kuna mawili...

1) Utafutwa ubunge

2. Utauliwa.
Na lile kanisa lake lipo kwenye road Reserve inabidi alihamishe
 
Kama humjui gwajima vzur ww kijana wa leoo muulizee mstaafu kikwete na makonda watakupa habari zake..
Gwajima ni mutu na nusu erooo..
 
Pacha umeweza kuwaza nje ya box. Mambo haya yanahitaji sana upeo mkubwa kuweza kuyang'amua.
 
Huyu si ndo yule jamaa alikulaga kondoo ...hivi kumbe alipata nafasi ya kuingia mjengoniπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Atapewa adhabu ya karipio, labda akaze kichwa afukuzwe ahamie upinzani agombee tena🀣
 
Gwajima apewe ulinzi, huyo ni asset adimu sana kuwahi kutokea nchini. strong man at work!, tikisa vyura wote. Sijajua amezungumza kama PHd holder, kama Bishop, kama Member of parliament, kama mwanaCCM ama kazungumza kama mwananchi wa kawaida. Hapa ndipo sijamuelewa...ila kwa ujumla mm binafsi namuelewa sana Gwajima kama Bishop, God bless him
 
Huyo hata akifukuzwa uanachama naona ni kazi bure tu, hivi ana cha kupoteza kweli? Au ndio umaarufu ndio utakubwa mkubwa? Sijui.
 
Shaka nilikwisha mpuuza tangu alipo toa tamko juu ya yule mbunge viti maalumu Majige
 
Kwa mujibu wa katibu mwenezi ndg Shaka wote waliopinga maagizo na maelekezo ya mwenyekiti juu ya suala la chanjo ya korona na tozo wajiandaye kukiona cha mtema kuni.


Source:ITV
 
Pacha umeweza kuwaza nje ya box. Mambo haya yanahitaji sana upeo mkubwa kuweza kuyang'amua.
Pacha hii sinema safari hii ni kiboko ya karne. Mama akiendelea kujifanya kaziba masikio kwetu viherehere wa JamiiForums tunao jaribu kumpigia kelele na kumuuzia ramani ya vita. Imekula kwake.

Sisi Yetu [emoji102][emoji102]
 
Huwa sielewi matumizi ya nafasi ya mwenezi,amekuwa hakimu badala yakuunganisha watu kwa Sera na upendo.
Wanaotoa hoja wanachanganua,yeye anakuja na command ya jina la mtu.Hatari sana
 
Kishaonja Asali sasa anachonga mzinga.
 
Kwa mujibu wa katibu mwenezi ndg Shaka wote waliopinga maagizo na maelekezo ya mwenyekiti juu ya suala la chanjo ya korona na tozo wajiandaye kukiona cha mtema kuni.


Source:ITV
CCM hawawezi kumgusa Gwajima,ana 'watu' wakimgusa chama kinasambaratika mchana kweupeeeeee. Hawamuwezi amejipanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…