Pre GE2025 CCM wamchangia Lissu Milioni 5 atengeneze gari lake. Lissu azipokea
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ndugu akiungana na shetani bado ni ndugu! EeeeenHeeeee!
Tunao ndugu wauaji, wezi na mengineo mengi kinyume chetu, lakini bado ni ndugu zetu na hatuwajibiki kwa matendo yao. Je, hao askari watesaji na sisi tuzichukie na kuzitenga familia zao?
 
Naamini mpaka tunavyoandika hapa CCM hawana jiwe lolote la kumpigia Lissu, na ndio maana kila akiwarushia mawe yake CCM wote hunyamaza kimya.

Lakini kitendo cha Lissu kupokea hizo 5.3mil ndio litakuwa kosa kubwa, CCM wataimba huo wimbo mpaka next year kwenye kampeni za uchaguzi mkuu.

Sioni sababu kwanini wapewe hiyo nafasi, hizo pesa zinaweza kabisa patikana kwa namna nyingine, waendelee kuhamasisha michango ili kulinda taswira ya Lissu kule tunapoelekea.
 
..wanasema wameingiza kwenye akaunti ya Lissu aliyoelekeza watu wachangiaji.

..ila hili na jambo la kusitisha kwamba wamechangia huku wakifanya kejeli.

..Mch.Msigwa haikumpasa kujidhalilisha kiwango hicho.
Nimekupata sana mkuu.

Lissu ni mtu mahiri, ccm wanataka kuleta taharuki kwa hili, lakini Lissu kwa wakati wake atalitolea ufafanuzi na wenye akili watamuelewa.

Tunamhitaji sana Lissu kwenye urais mwakani, na hiyo ndiyo hofu ya ccm na vibaraka wao waliojibanza ndani ya chadema.
 
Lakini kitendo cha Lissu kupokea hizo 5.3mil ndio litakuwa kosa kubwa, CCM wataimba huo wimbo mpaka next year kwenye kampeni za uchaguzi mkuu.
Lissu anao uwezo wa kuzima hoja zao, tuupe muda nafasi.

Najua maadui wa Lissu ndani ya chadema ndio watauimba wimbo wa Lissu kuchangiwa na ccm kuliko hata ccm wenyewe watakavyoimba.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amewaongoza wajumbe wa NEC alioongoza nao ziarani mkoani Mwanza na wanachama wa chama hicho mkoani humo wamemchangia Shilingi Milioni Tano Makamu Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu ili kufanyia matengenezo gari yake.

Kada wa CCM, Mchungaji Peter Msigwa akiwa kwenye mkutano wa chama hicho kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza alimuomba Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Nchimbi kuhamasisha wanachama wa CCM kumchangia Lissu ili gari hilo limuwezeshe kufanya shughuli za siasa.

Kwa upande wake, Dkt Emmanuel Nchimbi amesema siasa si uadui hivyo ni vyema kushikana mkono pale panapobidi kwani wanasiasa wote wanaijenga Tanzania.
Alipotafutwa kuzungumzia kitendo hicho kilichofanywa na CCM, Lissu amewashukuru CCM kwa mchango na kwamba atazipokea fedha hizo kama ambayo amekuwa akipokea kutoka kwa makundi tofauti ya watu.

"Nawashukuru, kama nilivyosema...hatukusema tunachangiwa na wanaChadema peke yao, kama nilivyotibiwa, sikutibiwa na wanaChadema peke yao. Kwa hiyo, wakichangia nitazipokea, sina sababu ya kukataa," amesema Lissu.


Mwananchi
Pokea Lissu waliokuchangia wanakukubali ndiyo maana wamekubali kuchanga. Hata huyo Makalla ameonesha anakukubali. Ndiyo maana kachangisha wanaomzunguuka mama! Wamechoka pia wanaficha uovu wao.
 
Mh. Tundu Antiphas Lissu hakuomba kuchangiwa na CCM, full stop. Wanaochanga wanafanya hivyo kwa hiari yao. Kwa watu wenye akili ndogo ni vigumu sana kuelewa kinachoendelea. Ninavyomjua Mh. Lissu CCM anajua anachofanya kwani CCM kama walivyo nguruwe wanajikaanga kwa mafuta yao wenyewe. Wembe uko pale pale...
 
..subiri Lissu aanze kumbonda Mama Abduli utasikia wanavyomlaumu.
Na huwa anawaambiaga, kama ni hongo ili ninyamaze - Hapana. Aliwahi kusema maneno hayo walimlaumu eti anamsema vibaya Mama wakati amemsaidia mengi!
 
Tunafuatilia siasa za nchi hii kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za mtaa, kuna tukio juzi la kamata kamata Na kuwapiga viongozi wa Chadema Mbeya, limejeruhi sana 4R za Mhs Rais.

Haikuwepo sababu kubwa ya kuchukua hatua kali kama hiyo wakati huu wa kutafuta kura za watanzania kupitia 4R.

CCM wakiongozwa na uzoefu wa Dkt. Nchimbi wameona wapindue meza kwa kumchangia Lissu gari ili kupooza makali na kubadilisha ajenda.

CHADEMA inaoneshwa jinsi siasa inavyochezwa. jifunzeni.
 
Tunao ndugu wauaji, wezi na mengineo mengi kinyume chetu, lakini bado ni ndugu zetu na hatuwajibiki kwa matendo yao. Je, hao askari watesaji na sisi tuzichukie na kuzitenga familia zao?
Hapana, siyo "kuzitenga familia zao", ni kuwatenga wao waovu. Mkijihusisha nao bila hata ya kukemea maovu yao nanyi mtakuwa waovu kama hao ndugu zenu.
 
.
IMG-20240816-WA0090.jpg
 
Nashangaa kwa nini ndugu yangu Lissu kapunguza moto wa kuhamasisha michango. Au kuchangisha ilikuwa njia ya kutakatisha fedha ionekane zimetoka kwa wananchi
 
Nashangaa kwa nini ndugu yangu Lissu kapunguza moto wa kuhamasisha michango. Au kuchangisha ilikuwa njia ya kutakatisha fedha ionekane zimetoka kwa wananchi
CCM yooooote 24/7 hawaishi kumuwaza Lissu, Ama Mbowe ama CHADEMA😀
Yaani muda wote ni hivyo tuu mpaka wanasahau kufanya yao
 
Nashangaa kwa nini ndugu yangu Lissu kapunguza moto wa kuhamasisha michango. Au kuchangisha ilikuwa njia ya kutakatisha fedha ionekane zimetoka kwa wananchi
CCM yooooote 24/7 hawaishi kumuwaza Lissu, Ama Mbowe ama CHADEMA😀
Yaani muda wote ni hivyo tuu mpaka wanasahau kufanya yao
 
Nashangaa kwa nini ndugu yangu Lissu kapunguza moto wa kuhamasisha michango. Au kuchangisha ilikuwa njia ya kutakatisha fedha ionekane zimetoka kwa wananchi
Wewe umechangia sh ngapi?
 
Hivi mtu ambaye alikuwa Mbunge ,Mwanasheria Msomi ,hivi unategemea aendeshe Maisha kwa mchango yako? Kabla ya kuanza kuchangisha maisha ulikuwa unamuendeshea wewe? Kama unaona ana faidi na wewe weka namba tukuchangie.
 
Back
Top Bottom