CHADEMA kukataa mualiko wa NEC wakati wanasubiri mualiko wa Rais Samia ni kichekesho

CHADEMA kukataa mualiko wa NEC wakati wanasubiri mualiko wa Rais Samia ni kichekesho

Kumbuka kuna "cause and effect"--- Samia kuwa Rais ni effect lakini Cause yake ni NEC, sasa Chadema watakuwa wajinga kulaumu effect na kuacha kulaumu Cause na kutafuta njia ya kudumu kudhibiti cause kama hiyo ili effect ya aina hiyo isijetokea tena.

Mfano ni huu; huwezi kuwalaumu wote mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa na wazazi waliomzaa bali wazazi ndio wa kulaumiwa, sasa hatuwezi kuwalaumu Wote Samia aliyepewa urais na NEC bali NEC ndio mlaumiwa kwa kukiuka wajibu wake kisheria na njia mojawapo iliyopo ya kudai na kulalamika ni kupitia huyo huyo mtoto wa NEC Rais Samia.
Uwezo huu wa uchambuzi ungekuwa unatumika na uongozi wa Chadema, chama kinge kuwa mbali.

Ninazo evidences nyingi ambazo uongozi wa Chadema haufanyi kabisa au hata kusikiliza synthesis analysis ya major events ili kupata critical path analysis huwa hilo halipo kabisa .

Na ukitaka wafuate uchambuzi wa kitaalamu wa kila jambo, watakwambia toa usomi wako hapa. Wataalamu ambao wanaweza kusikilizwa Chadema ni Wana sheria tuu, na sababu uongozi unafanya ya kuishi kisiasa kwa kuvunja sheria.

Ndio maana si shangai vilaza kuwa uongozi wote wa juu kabisa wa Chadema,
 
Bwashee, hata huko kwa rais wameshaghairi asipokutana nao peke yao. Akiwaweka kwenye kundi la vyama vyote basi hawaendi!
Ujinga uliomo chadema sasa hivi hata kwa fimbo hatuwezi kuutoa.
Uzuri mmoja tozo haziangalii huyu ni mataga or huyu ni chadema 🤣🤣🤣
 
Iko wazi Chadema na vyama vingine vilivyokataa kuhudhuria Mualiko wa NEC kwenye kutoa ripoti ya Uchaguzi wa 2020 sababu ilikuwa ni malalamiko yao juu ya wanachokiita dhuluma kwenye uchaguzi huo. WAMEKWENDA mbali zaidi hata wengine kugomea ruzuku, kugoma kupeleka majina ya wabunge wa viti maalum na kugomea chaguzi za marudio.

Kwa uwazi kabisa mtazamo wa CDM ni kuwa chaguzi za S/M 2019 na MKUU 2020 zilikuwa ni batili na walioshinda hawawatambui. Ajabu ya CHADEMA ktk hili ni uleule undumilakuwili wa "Sizitaki mbichi hizi" kwani inaonekana wako tayari kukutana na Rais Samia kwa ajili ya kufanya mjadala wa kisiasa sijui maridhiano ya kitaifa, they know much.

SWALI hapa wanataka kukutana na Rais aliyetokana na uchaguzi waliouita batili, What does that mean?. Maana yake hawatambui ushindi wa JPM/SSH mwaka 2020. Je wanataka kukutana na SAMIA yeye kama nani?. Kama ni Rais ameupata kutokana na uchaguzi upi?, je kama wanamambua hivyo kuna haja kutoutambua huo uchaguzi? It is just a logical fact!

CHADEMA katika kususia jambo bado wamefeli na wanafeli, mwaka 2015 walisusa na kutotambua Urais wa JPM na walifika mbali wakamuita Lowassa kuwa "Rais wa Mioyo ya Watanzania" (Sitaki kuongelea tena huu upuuzi wao maana huyu Rais amerudi kwao kumenoga). In the end bado walikuwa wanajipendekeza kutaka maridhiano mara kutaka kuonana na JPM ili kusikilizwa kilio chao wakati hawakumtambua kama Rais. Funny indeed

Kuna mawili ambayo CDM yanawashinda na wataendelea kuwa Ndumilakuwili mpaka kesho baada ya kuamua moja:-
1. Kama unasusa basi susa mazima ijulikane UMESUSA KIUME NA UNA MSIMAMO kisha dai tume huru KWA NGUVU ZOTE.
2.Show some respect kisha omba kukutana na RAIS ufikishe kilio chako awasikilize shida zenu.

Zaidi ya hapo ni Undumilakuwili na kuendelea kuonekana hawana msimamo . UNAMSUSIA KUKU WAKATI MAYAI YAKE YANAKUTOA MATE.


Kuna wakati tunafanya propaganda isiyo na mashiko. Vyama vyote vilivyokataa kushiki hafla ya Jana wapo sahihi
Maana waliikata mimba hivyoawana sababu kushiriki kwenye ubatizo wa mtoto.

Nchi lazima iwe na mkuu wake bila kujalishha amepatikana vipi. Majadiliano yafanywe kupata mwafaka.
Hivyo tu
 
Na hilo la kujiona wao ni bora na muhimu kuliko vyama vingine vyote vya upinzani litaendelea kuwakwamisha miaka nenda rudi, kwasababu vyama vingine vitaendelea kutowapa ushirikiano katika madai yao yote. Hiki ni chama ambacho hakina political strategists kabisa; kimejaa watu wa mitulinga tu. Utadhani Jeshi la Sungusungu!
Ni chama kipi kina hizo sifa ulizozitaja?
 
Kwa walio andikwa hapa na hakika mimi sijaona bado ninavyotakiwa kuongea. Hiyo Chadema wewe huifahamu kama ninayo ifahamu mimi.

Nimejiunga nayo nipo chuo, mwaka wa pili tuu baada ya kuanzishwa.
Rais Mwinyi alitufukuza na kufunga chuo 1994, tukapoteza
Mwaka, na bado niliendelea kuwa Chadema. Wazazi wakanipeleka nje kusoma zaidi, ili pia nipate nafasi ya kuachana na Chadema, niliporudi bado nikawa Chadema.

Ila nilihama 2015 moja kwa moja, labda kwenye social justices tuu ndio nakuwa sympathiser.

Huku kwa wazazi Lyamungo Sinde, Machame. Chadema ni maisha ya kila siku.
Kama hivi sasa hapa tupo Msibani kwa mama Mtei na Bi mkubwa wangu na Mwenyekiti wako hayapo.

Sisi ndio wale tukitaka kuibomoa Chadema utalia na kubadilisha Chama siku hiyo hiyo.

Ninachu shukuru sana hapa Jimbo lá Hai Chadema tumeisafisha, tumeijeruhi sana kiasi inaelekea kufa tumeisafisha na kuipiga deki kwa Machine na

KIJANA WETU MHESHIMIWA MNO LENGAI OLE SABAYA

kamaliza wizi wa kutumia silaha na mtandao wake,
Wizi wa magari na mtandao mzima.
maisha ya dhulma kwishney Ubabe usio na mpango keishney.

Bi mkubwa mama Grace unaweza kulala bila kufunga milango na sio lazima gari aiingize parking ya ndani ya nyumba. Hata akiziacha kwenye lawn tuu siku hizi inatosha.

Wazawa wasio na ardhi, aibu hiyo imekwisha, jimbo letu Wakristo ni wengi. Lakini ndilo lenye idadi kubwa ya Waislamu wazawa katika majimbo ya Kilimanjaro wanafuatiwa na Mwanga. Vitu vyote vilivyo kuwa karaha kwa Waislamu wame sawazishiwa, kama shule zao, maeneo yao ya misikiti, ardhi za Jumuiya zao.

These are long-standing social injustices we have been living with in Hai District for ages.

Madonda ndugu ya Hai CCM IMEYAPONESHA. .
 
Kuna wakati tunafanya propaganda isiyo na mashiko. Vyama vyote vilivyokataa kushiki hafla ya Jana wapo sahihi
Maana waliikata mimba hivyoawana sababu kushiriki kwenye ubatizo wa mtoto.

Nchi lazima iwe na mkuu wake bila kujalishha amepatikana vipi. Majadiliano yafanywe kupata mwafaka.
Hivyo tu
Well said
 
Ukiangalia kwa haraka nikuwa NEC inaendelea kujitangaza kuwa haikubaliki, na haiaminiki na watu wowote zaidi ya wale walio nufaika nao.
Hapa kuna ushirika wa NEC na wanufaika nao yaani CCM and Allies.
Kukataliwa huku kunaionyesha dunia tatizo letu la kikatiba lilivyo. Ila kwa watawala, hawaoni wala kusikia mana mlo umepofusha macho.
Ninacho shukuru ni kuona mambo hayahaya yanaamsha watu walio lala. Ingawa hawatapinga kwa mapigano, ila wanaandaliwa kuwa tayati kuunga mkono mtu atakae jitolea kupinga kwa mapigano.
 
Ningewashangaa sana Chadema kama wangelikwenda huko wakati anayewaalika ndiye anamshikilia Mwenyekiti Mbowe!
 
Nimekunyoosha, nimeongea na ma'am yako atakupigia Sasa hivi akwambie baba yako ni Nani maana huyo unayejidai naye Ni wa kufikia

Nimekunyoosha, nimeongea na ma'am yako atakupigia Sasa hivi akwambie baba yako ni Nani maana huyo unayejidai naye Ni wa kufikia
Retired, mbona leo umejaa matusi hivyo? Tena haziko proportional na hoja. Unazimwaga tu.
 
Na hilo la kujiona wao ni bora na muhimu kuliko vyama vingine vyote vya upinzani litaendelea kuwakwamisha miaka nenda rudi, kwasababu vyama vingine vitaendelea kutowapa ushirikiano katika madai yao yote. Hiki ni chama ambacho hakina political strategists kabisa; kimejaa watu wa mitulinga tu. Utadhani Jeshi la Sungusungu!
Kwa hiyo unalazimisha chadema wakae pamoja na cuf au vile vyama pandikizi vinavyojiita ni vyama vya upinzani kumbe mlango wa nyuma ni ccm???Unaelewa maana ya upinzani wewe??Kama mtu umekubali kuwa mpinzani unatakiwa uwe na maono yako kufuatana na falsafa ya chama husika.
 
Unasemaje kuhusu ACT-Wazalendo, CUF, NCCR-Mageuzi ambao pia walikataa kwa sababu hiyo hiyo? Ama mimba yako hiyo mtoto hujigeuza tu pale anapotajwa CHADEMA?
Iko wazi Chadema na vyama vingine vilivyokataa kuhudhuria Mualiko wa NEC kwenye kutoa ripoti ya Uchaguzi wa 2020 sababu ilikuwa ni malalamiko yao juu ya wanachokiita dhuluma kwenye uchaguzi huo. WAMEKWENDA mbali zaidi hata wengine kugomea ruzuku, kugoma kupeleka majina ya wabunge wa viti maalum na kugomea chaguzi za marudio.

Kwa uwazi kabisa mtazamo wa CDM ni kuwa chaguzi za S/M 2019 na MKUU 2020 zilikuwa ni batili na walioshinda hawawatambui. Ajabu ya CHADEMA ktk hili ni uleule undumilakuwili wa "Sizitaki mbichi hizi" kwani inaonekana wako tayari kukutana na Rais Samia kwa ajili ya kufanya mjadala wa kisiasa sijui maridhiano ya kitaifa, they know much.

SWALI hapa wanataka kukutana na Rais aliyetokana na uchaguzi waliouita batili, What does that mean?. Maana yake hawatambui ushindi wa JPM/SSH mwaka 2020. Je wanataka kukutana na SAMIA yeye kama nani?. Kama ni Rais ameupata kutokana na uchaguzi upi?, je kama wanamambua hivyo kuna haja kutoutambua huo uchaguzi? It is just a logical fact!

CHADEMA katika kususia jambo bado wamefeli na wanafeli, mwaka 2015 walisusa na kutotambua Urais wa JPM na walifika mbali wakamuita Lowassa kuwa "Rais wa Mioyo ya Watanzania" (Sitaki kuongelea tena huu upuuzi wao maana huyu Rais amerudi kwao kumenoga). In the end bado walikuwa wanajipendekeza kutaka maridhiano mara kutaka kuonana na JPM ili kusikilizwa kilio chao wakati hawakumtambua kama Rais. Funny indeed

Kuna mawili ambayo CDM yanawashinda na wataendelea kuwa Ndumilakuwili mpaka kesho baada ya kuamua moja:-
1. Kama unasusa basi susa mazima ijulikane UMESUSA KIUME NA UNA MSIMAMO kisha dai tume huru KWA NGUVU ZOTE.
2.Show some respect kisha omba kukutana na RAIS ufikishe kilio chako awasikilize shida zenu.

Zaidi ya hapo ni Undumilakuwili na kuendelea kuonekana hawana msimamo . UNAMSUSIA KUKU WAKATI MAYAI YAKE YANAKUTOA MATE.

 
Samia si katokana na huo uchaguzi batili? Hiyo ina maana urais wake ni batili pia, then why mnataka kuonana na Rais batili?
Kuonana naye ni lazima pamoja na ubatili wa kuwepo kwenye kiti kile ili kuweka mambo sawa,kukataa kukutana na Samia ni kushindwa kutimiza wajibu na haki ya kisiasa katika kudai madai halali,pia Samiah ni mwanadamu pengine anadanganywa sana na watu wa kariba yako lakini atakapokutana na viongozi wa Chadema ana kwa ana kuna maswala yaliyojificha chini ya pazia yataibuliwa na atayafanyia kazi.
Vilevile Chadema kama chama kikuu cha upinzani wana madhaifu yao ambayo Rais Samiah anayajua pamoja na watu wengine kama wewe,atawaambia wasasahishe sehemu fulani ili mambo yaende sawa.Hivyo lengo la kukutana si ushabiki bali ni maridhiano kwa usalama wetu na usalama wa nchi yetu.
 
Ni kwa mwenye ufinyu wa akili tu ndiyo anaweza kuandika hivi. Mpaka hapo nchi itakapoingia kwenye machafuko ya kutisha kwa UCHAFUZI wa uchaguzi ndiyo mtatia akili kichwani.

Machafuko hayata muathiri mmoja, hata wewe unayeombea Taifa liingie kwenye machafuko hutakwepa athari za moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja.
 
Safi sana.
Kitu ambacho hujui, hata ukipindua nchi na ukaweza bado utaitwa rais, CHADEMA wapo sahihi kabisa, Samia hata angekuwa amefanya mapinduzi bado angekuwa ni rais japo hatakuwa amepatikana na njia ya kidemokrasia
 
Back
Top Bottom