Changamoto katika ujenzi: Mafundi uchwara wanavyoharibu kazi

Changamoto katika ujenzi: Mafundi uchwara wanavyoharibu kazi

Kama hujaanza ujenzi hasa wa nyumba yako ya kwanza ya kuishi jitahidi sana upate elimu ya kutosha kwenye
Ununuzi wa ardhi/kiwanja
Mafundi wa kila idara
Makisio ya vifaa, ufundi
Muda sahihi wa kuanza ujenzi
Nini cha kuanza kufanya nknk
Fanya utafiti wa kutosha.. Pata makisio ya ujenzi kwa kila hatua kwa mafundi tofauti
Ukiachana na changamoto za kuongezewa gharama kwenye vifaa na gharama za ufundi ama kuibiwa kwa vifaa vilivyokwisha nunuliwa kuna hili la kuharibiwa kazi
Na kazi iliyoharibiwa ina changamoto kubwa zaidi za kurekebisha kuliko kazi mpya
Kuna mengi sana ya kuambiana hapa lakini machache makubwa ni haya
1. Usifanye malipo ya ardhi/kiwanja bila kujihakikishia umiliki wake, migogoro, mipaka nk
2. Usifanye malipo bila kujihakikishia serikalini ramani ya mipango miji
3. Usianze ujenzi bila kufanya ibada ya kutakasa ardhi.. Ukishindwa hapo basi ibada ya kuitakasa nyumba
4. Usianze ujenzi bila kujihakikishia sehemu salama ya kuweka vifaa vyote vitakavyohusika kwenye ujenzi
5. Usianze ujenzi kwa kufanya mkupuo wa manunuzi.. Anza na vitakavyohitajika kwa wakati huo tu.. Na kama kina baadhi utavipata mapema kwa bei nzuri kaa navyo mwenyewe
6. Piga kenchi ukiwa umejihakikishia uwepo wa mabati
7. Usifanye wiring kama hakuna mtu anayekaa hapo.. Utajuta
8. Usiiache nyumba tupu/peke yake unapoelekea kumaliza ujenzi wa awali
9. Kumbuka gharama za finishing ndio kaburi la pesa😂 hivyo jiandae
10. Jihadhari na majirani...😀🤔🙇🏿‍♂.... Wakati wa ujenzi na utakapohamia.. Kuna jirani anaweza kuwa rafiki wakati wa ujenzi lakini akaja kuwa adui mkubwa utakapohamiaView attachment 3234061
Mkuu nahisi nimedhulumiaa nifanyaje?
 
Ngumu sana kuwakimbia hapo ,lazima akuingize kwenye 18 zake na ale cha juu ,ukienda kununua kwenye duka unaotaka wewe let say ukakuta bei labda elfu 15 atakwambia twende duka la mbele wanauza 14 ,ukienda tu kwenye hilo duka utakuta bei 14 na utanunua kwa kuona kuna unafuu wa buku ,kumbe hapo yeye ana jero lake hapo.
Dawa ni kwenda mwenyewe kichwa kichwa kuhemea vifaa na usimshirikishe.

Kazi yake yeye ni kutaja vifaa vinavyohitajika, halafu mahemezi unazama dukani mwenyewe.
 
Lakini nimiwa na wale jamaa zako wa kilingeni sii wanaweza nilindia nyaya zangu bila kuwepo mtu
Utapigwa halafu utapigwa tena😂 vilinge vya siku hizi havina totauti na lile joka la kibisa
 
Hapo ndiyo dawa yao vinginevyo lazima wapige cha juu.
Hilo waweza kulidhibiti, lakini katika ujenzi kuna wizi wa kila aina usipokuwa makini.

Je unajua kuwa mota(tope)la saruji iliyochanganywa na mchanga tayari kwa ujenzi kuwa inauzwa na mafundi?

Je waelewa marundo ya mchanga kwenye site yako ni store ya kuhifadhia saruji na vifaa vingine vilivyoibwa vinavyosubirishwa kuondoshwa?

Je wajua kuwa vipande vya tofari pamoja na misumari iliyododoka katika kupaua inatafutwa kama sukari?

Je wajua kuwa saruji iliyokwisha kufumuliwa kwenye mifuko huuzwa kwa kupima kama chumvi?

Je wajua vipande vya mabati vinavyoonekana kutofaa kwa kazi yoyote hapo kwenye ujenzi wako kuwa ni pesa ya chap chap?

Je wajua pia kuwa siku ya kupaua ndiyo siku ya kukuibia bati zako utake usitake: Bati zilizopangwa kuvushwa hushikizwa ndani ya paa ya dari hata ukichungulia ni ngumu kubaini, usiku mafundi hurejea na kuzihamisha?

Mkuu, unapoanza ujenzi jitoe hasa kusimamia mwenyewe, usitume mtu kusimamia kwa niaba yako, hata mkeo hapana maana kuna ujanja mwingi sana wa wizi na upotoshaji wa manunuzi.
 
Back
Top Bottom