Changamoto za kufanya kazi na Mtu anayekaribia kustaafu kwa heshima

Changamoto za kufanya kazi na Mtu anayekaribia kustaafu kwa heshima

Nawasalimu,

Twende kwenye mada.

Kuna mzee wangu tumefanya kazi poa sana Three years back.

Amebakisha 1year, 3 Months kustaafu rasmi utumishi.

Imekua changamoto sana kufanya nae kazi kipindi hiki, anaonekana mtu mwenye mawazo sana, na kugeuka kuwa mkosoaji wa kila kitu tunachofanya.

Kwasababu ya cheo alichonacho kumshauri inakuwa ngumu sana,

Hivi wakuu huwa ni kawaida Watarajiwa wastaafu kuwa na hizi tabia?

Kazi zinakuwa ngumu kidogo.

Hebu share uzoefu wako
Stress za kutojiandaa zinamsumbua... huwa kama wameingiwa roho ya mauti.
 
Si mchezo mkuu.

Anaogopa sana, yani vitu vidogo ana mind balaa.

Kuna zile warsha za wanaotarajia kustaafu, hizo ndio hataki kusikia kabisa.

Mungu amsaidie kwa kweli.
Inawezekana kuna mambo hakuyaweka sawa wakati akiwa kwenye nafasi, sasa ajira inafikia tamati anapatwa na msongo.

Hilo liwe fundisho kwako, ujipange na kukamilisha malengo yako kabla jua lako halijazama.
 
Si mchezo mkuu.

Anaogopa sana, yani vitu vidogo ana mind balaa.

Kuna zile warsha za wanaotarajia kustaafu, hizo ndio hataki kusikia kabisa.

Mungu amsaidie kwa kweli.
Ndio ujinga wao si arudi akasome magazeti HQ yanakaaga tu yanataka walipo vijana ili yawachafulie faili hovyo kabisa haya mazee
 
Nawasalimu,

Twende kwenye mada.

Kuna mzee wangu tumefanya kazi poa sana Three years back.

Amebakisha 1year, 3 Months kustaafu rasmi utumishi.

Imekua changamoto sana kufanya nae kazi kipindi hiki, anaonekana mtu mwenye mawazo sana, na kugeuka kuwa mkosoaji wa kila kitu tunachofanya.

Kwasababu ya cheo alichonacho kumshauri inakuwa ngumu sana,

Hivi wakuu huwa ni kawaida Watarajiwa wastaafu kuwa na hizi tabia?

Kazi zinakuwa ngumu kidogo.

Hebu share uzoefu wako
Siyo kwa watu wote, wengine wanastaafu kwa hiyari miaka 55 tu wafanye mishe zao.
 
Kuna limoja linaondoka oktoba kutwa kuwachafulia mafaili wa chini yake sijui niliharibie nisanue ishu zake kulitia Jamba Jamba likose mafao kutwa kuandika mibarua kuwalima wachini yake utadhani toto la kike,pana mijitu ya hovyo sana makazini.
Hivi ukimfukuzisha kazi mtoto wa mwenzio utapewa mshahara wake.
Hadi unastaafu wewe nawe ungeharibiwa ungefika hapo?
Mungu Huwa anayalipa.
Kuna moja hovyo sana likikuwa libosi la mkoa mzima wa Dar likastaafu likapata milion 250.
Leo linakaanga chips mbagala.
From boss wa mkoa to kijiwe Cha chips.
Boss yeyeto mpambanaji huwezi kuta kuchwa anashinda kuwachafulia wa chini mafaili.
Huwa yanachoka vibaya hatari haya manoko yakistaafu tumeyaona mengi tu yanapiga mizinga.
 
Stress,unafikiri kuamka asubuhi hujui unaenda wapi ni kitu kidogo?
Kwani si kuna PS Mkuu, tatzo wazee wanafikiri PS ni za watoto na vijana, embu fikiria umestaafu zako unanunua PS 5 yako na Tv ya 56'' hapo unaanza fuga kuku wa mayai ukiwalisha asubuhi mchana ni kuwachungulia alafu unarudi kucheza PS 5 yako sebuleni 😂😂😂

Anyway mimi sitaacha kamwe kucheza PS
 
Ukiwa umejiandaa vizuri hutakuwa na stress za kustaafu. Ila kama pesa ulikuwa unafuja unakumbuka shuka alfajiri ndiyo utakuwa na stress na visirani Sana. Mtu kama Una mshahara mzuri hakikisha unakuwa a fixed deposit ya 500m by the time unastaafu na fixed assets za kutosha. Hapa hutapata tabu kabisa na kila mwaka utakuwa unatengeneza faida zaidi ya mil 50 na pension yako. Na mapato kwenye assets. Yaani wewe ni kufanya mazoezi na KAZI ndogondogo nyumbani. Narudia uzeeni usilale au kukaa kusoma.magazeti. Bora ufuge hata kuku wa kienyeji uwatembelee bandani. Uzee maana yake ni kufanya viungo vyako active. Ukikaa sebuleni au nje kusoma magazeti utaporomoka viungo kwa speed ya radi.
 
Kwani si kuna PS Mkuu, tatzo wazee wanafikiri PS ni za watoto na vijana, embu fikiria umestaafu zako unanunua PS 5 yako na Tv ya 56'' hapo unaanza fuga kuku wa mayai ukiwalisha asubuhi mchana ni kuwachungulia alafu unarudi kucheza PS 5 yako sebuleni 😂😂😂

Anyway mimi sitaacha kamwe kucheza PS
Umenichekesha sana 😂😂
Mimi nilishajaribu hayo makitu aisee naona sielewi. Yanavutia lakini vitoto vidogo vitaalamu vilikua vinanikanda nikaona ni kuaibishwa huku.
 
Back
Top Bottom