#COVID19 Chanjo ni hiari: Spika Ndugai ni nani kuipinga kauli ya Rais?

hizi ndio point sasa
 
kwa hiyo siku hizi chanjo zimebadirika? zimekuwa tofauti na chanjo za zingine tulizowahi kuchanjwa?

yaani chanjo za leo uchanjwe ama usichanjwe hatari ni ileile?
 
Kama hamjamjua Samia hadi muda huu mtateseka sana! Kuna vitu huwa anaviamua Ikulu kimya kimya halafu anawatupia zigo wasaidizi wake wenye roho ngumu wavitoe hadharani, wananchi mkilalamika atasema ok tutakaa chini tulifanyie kazi, hapo jua mshapigwa. Ref suala la tozo, kuyafungulia magazeti ya mwanahalisi na tanzania daima, sasa hili la chanjo majeshi yake yameanza kulitambulisha mdogo mdogo. Soon mtaambiwa hamna kuingia misikitini na kanisani bila chanjo
 
Mwajiri nani ananguvu ya kuzuia tamko la mh Rais?

Mwajiri mkuu ndiye aliyesema hivo na ndiye mlinzi wa wawajiliwa wote nani tena mwajiri anayempinga mwajiri mkuu?
Nimegundua siasa huzijui.muajiri mkuu kasha chanjwa tayari
 
Maana yake, sisi tumechanja na ukitaka kuja nasi chanja. Hutaki, ni hiyari yako, baki huko usije nasi, hilo tu!
Kwa Nini wewe uliyechanja usije nasi tusiochanja? Kwa Nini unakomaa upande wako tu?
 
kwa hiyo siku hizi chanjo zimebadirika? zimekuwa tofauti na chanjo za zingine tulizowahi kuchanjwa?

yaani chanjo za leo uchanjwe ama usichanjwe hatari ni ileile?
... sijakuelewa! Kwamba ukiwa na chanjo ya kifua kikuu that means hupati kifua kikuu? You are wrong! Vimelea vya kifua kikuu utapata na hata kifua kikuu utapata ila athari zake zinakuwa ndogo!

Swali mbona waathirika wa ukimwi hufa kwa kifua kikuu wakati walishawahi kupata chanjo ya kifua kikuu? Tafuta majibu ya hilo swali utaelewa maana na role ya chanjo mwilini maana inaonekana hujui.
 
Waliochanjwa nao wanaogopa kusambaziwa covid?
 
Kama nakuelewa vilee...!
 
Mkuu mbona hata Dkt. Hedwiga swai mkurugenzi wa tiba muhimbili alipinga hizi chanjo na alielezea kitaalamu kabisa.
 

Hapana, atakachofanya ni kuwa anahitaji vipimo vya masaa 48 yaliyopita kama huna Corona ili uingie bungeni kwa gharama yako mwenyewe kwa wabunge wote ambao hawaja chanja. Aliyechanja aonyeshe cerificate.
 
Hso maprofesa si ndio hao walisema miti shamba ndio yenyewe? tushike lipi sasa, halafu mbona unakuwa mkali utadhani wewe ndio miongoni mwa hao maprofesa bhana?
 
Huyu andunje wa Kongwa ni mpuuzi sana, kwanza wapiga kura wake wote wamechanjwa?
 
Maana yake, sisi tumechanja na ukitaka kuja nasi chanja. Hutaki, ni hiyari yako, baki huko usije nasi, hilo tu!
Wewe uliyechanja hutakiwi kuwa nasi tusiochanja ka jilock down .Na kuji I solate.Wewe Kama mvaa barakoa ukiona umati hawana barakoa wewe ndio unatakiwa kukimbia Kama umefumaniwa kuwakimbia umati usiovaa barakoa Wala social distance.Wewe ndio hutakiwi kuwa Nasi tusio chanja ambao ndio wengi.Wewe ndie utafite pa kuji.lock dunia yako

Ukiona mkutano wa hadhara hawajachanja na hawajavaa barakoa kimbia wewe ndie hutakiwi kuwa nao you are not part of them your part of wazungu . Africa na Tanzania unakalia Nini si uende huko kwao.

Wewe ndio usikanyage sokoni Wala mitaani Wala kupanda daladala Wala kwenda mkutano wa hadhara!!!

Minority can't overrun the majority take note.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…