Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Chapati ya Kichina, mmea unaoishi kwenye maji, Kombucha/tea mushroom

Ukiupata rudi hapa utugawie. Mimi niliutumia miaka ya 80

Bado sijaupata mkuu,

Ila kuna mwamba hapo juu katushauri tujaribu pale chuo kikuu (udsm).

Bila shaka kama nitafanikiwa kuupata nitaleta mrejesho hapa! Au yeyote atakaye upata pia basi please atushirikishe maana wahenga wanasema "kizuri kula na wenzako!"
 
Umenikumbusha mbali mkuu, nakumbuka mama alikuaga ananipa juice yake, chachu tamu, likawa linazaa chapati nyingine.
Itabidi tukikutana na wachina tuwaulize, hata mimi natamani kujua inapopatikana, nikipata jibu nitakuambia
Aisee we jamaa umenifanya niuukumbuke huo mmea....nilikuwa sijamuelewa mleta mada, tena nakumbuka mama alikuwa anauweka kabatini na kuufungia ili tusimalize juisi yake

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mmmh! Mkuu, bahati mbaya sikubahatika kuupiga picha wakati bado niko nao!

Pia miaka hiyo simu hazija eneo sana, kama zilikuwepo basi kwa watu wachache sana, nakumbuka simu yangu ya kwanza kumiliki nilikuwa SIEMENS C 25 kubwa kama kipande cha Sabuni enzi hizo tunaziita "MSHINDI" (aina ya sabuni) tena nilikuwa hazina camera! Miaka ya mwanzoni mwa 2000! Kabla ya kumilika NOKIA enzi hizo tunaziita "JENEZA" aha aha haaa! Hatari sana mkuu!

Ingekuwa ninalo sasa mbona tayari picha muda mrefu tu!
Hiyo simu ulinunua sh ngapi mkuu km unakumbuka?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Hazina madhara kweli?

Hazina madhara mkuu,

Kwanza ni tiba na pia ni kiburudisho kizuri sana!

Fungus au fungi ni jamii ya mimea au wadudu (maana haipo kwenye kundi la mimea kamili wala wanyama) ambayo baadhi yao inatumika kwa manufaa mfano Uyoga (mushrooms) ni jamii hiyo fungus (fungi) ambayo ni chakula kizuri chenye protein nyingi.

Hamira (Yeasts) au baking powder, pia ni jamii ya fungus (fungi) ambayo hutumika kwenye chakula na kuleta ladha nzuri sana mfano kwenye kuoka mikate, keki, skonzi na maandazi.

Lakini havina madhara kwa binadamu.
 
Hii kitu alikuja nayo shangazi kama sio dingi kutoka mkoani mbeya.

Huu mmea hata Tanzania tunao sababu tuna utajiri wa species nyingi sana za mimea.

Ngoja nikutafutie jina na ukipatikana nitashare na ninyi hapa jina na ikibidi tugawane mbegu ni mzuri sana ile kitu tulikuwa tunaigida sana juice yake.

Tuliweka kwenye zaidi ya vyomba sita tukilina maji yake. Alikuja kuharibu bi mkubwa alipookoka akaambiwa na pastor wake kuwa kile kitu ni mapepo na ni maagano ya mizimu. Yule pastor choko sana hadi leo namind kichizi nikimuona natamani nimlabue makofi na mitama maaana ndie alimchanganya bi mkubwa akaona ule m'mea una uhausiano na maswala ya giza na kumbe ni ukosefu tu wa elimu ya mimea na tiba asili.

Bi mkubwa aliyamwaga yale masufuria yote kimya kimya ndo hadi leo sijuagi pa kuupata.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hiyo simu ulinunua sh ngapi mkuu km unakumbuka?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app

Daah, sikumbuki mkuu!

Kwani hata nilinunua basi?! Braza ambaye ndiye first born alianza kazi ndio akaniletea kama zawadi.
Ha ha haaa! Kitambo hicho nasoma pale Azania boyz upanga east. Hatari sana, japo shule tulikuwa haturubusiwi kwenda na hiyo kitu. Enzi hizo headmaster alikuwa Mr. David Kwayu, second master Mkongo, principal Mchompanga! Back in time!
 
Mmea mzuri sana unanikumbusha mbali ,naweza upata wapi huo mmea gheto ulikua unawekwa na bi mkubwa kwenye kile kifuniko cha jiko la kichina lisilotumika lile la mafuta ya Taa .Mleta mada nauhitaji
 
Mmea mzuri sana unanikumbusha mbali ,naweza upata wapi huo mmea gheto ulikua unawekwa na bi mkubwa kwenye kile kifuniko cha jiko la kichina lisilotumika lile la mafuta ya Taa .Mleta mada nauhitaji

Mkuu, lengo hasa la kuleta mada hii na Mimi ni hilo hilo la kuutafuta huu mmea wa ajabu, basi tuunganishe nguvu kuusaka !
 
mkiupata nami nahitaji, nimeishywa sana kwa bibi miaka ya 90, watu walianza kuzusha ni mapepo watu wakaanza kuzitupa
 
Eeewaaaa!!!

Hakika unaufahamu vizuri huu mmea! Ndio huo huo uliouelezea, mbegu yake ndio hiyo hiyo unapotanuka na kuubandua hiyo ndiyo mbegu yake mkuu!

Nilikaa nao karibu miaka 3 au 4 hivi, nilikuwa nauhudumia vizuri sana, na unapozaliana nilikuwa naupunguza na kuzitupa mbegu zake yaani yale mazalia yake.

Lakini sasa nikaja kusafiri na kujichelewa kurudi nikakuta umeshakufa kwa kunyauka, sasa natafuta kama kuna mtu ana huo mmea anisaidie utakapotoa mazalia yake (mbegu).

Shukrani sana!
mkuu vipi kama nitaenda kuuweka ziwani siutaishi maisha marefu sana!
 
mkuu vipi kama nitaenda kuuweka ziwani siutaishi maisha marefu sana!

Mkuu, sijawahi kujaribu hii njia,

Lakini naamini kila kitu kina mazingira yake ya ku-survive! Mfano kuku anaweza kuishi bandani mpaka akanawiri lakini ukimpeleka porini akafa au akaliwa na wanyama wakali.

Vivyo hivyo huu mmea mazingira yake ni kuutunza hivyo, maana kwenye ziwa huwezi kuipata juice yake itatoweka na maji yote , pili unaweza kuharibiwa na wanyama wengine wa majini, japo najua asili yake lazima ulitokea kwenye maji kama, ziwa, mto, bwawa au chemchem.
 
Back
Top Bottom