Uchaguzi 2020 'Charisma' ya Tundu Lissu itazidi kumpa shida sana Magufuli na CCM kwa ujumla

Uchaguzi 2020 'Charisma' ya Tundu Lissu itazidi kumpa shida sana Magufuli na CCM kwa ujumla

Jamaa kilichobakia sasa, anatakiwa tu kusoma hotuba aliyoandikiwa na wasaidizi wake, na tena asome "word by word" na kwa utulivu na wala pasipo kuingiza vionjo vyake mwenyewe ama utani wowote ule.

Kwa maana hata akijaribu kufanya utani anajikuta anatumia maneno magumu ambayo hutuma ujumbe kwa walengwa kama anatoa kashfa. Akikwazika ama kuudhiwa hapo ndipo inageuka kuwa balaa nyingine, hasira zote zinakuwa ktk mafaili anayolala nayo chumbani kwake, hapo ndipo tumbua na teuzi zinapoanzia kwa wasaidizi wake.

Wewe ogopa mtu ambaye wasaidizi wake wengi wa karibu waliokuwa serikalini wamekimbia nyadhifa zao ili kutaka kwenda kutafuta unafuu wa "stresses" ktk ajira za mhimili wa bunge.
 
Lissu hatoshinda.,,
CCM walifanikiwa sana kuiba kura enzi ya Mkapa na Kikwete kwa sababu hao wawili walikuwa ni viongozi wenye Charisma na mvuto.

Huu mwaka itakuwa ngumu sana kwa Magufuli na CCM kufanya janja janja maana kwenye kampeni wanaenda kushindwa vibaya.

Kwa ufupi Lissu anachokifanya ni kuamsha hisia za nguvu ya umma, ndo maana bado nna imani huu mwaka chochote chaweza tokea
 
Huu ni ukweli usionashaka...nmemfuatilia karibu mikutano miwili ya kampeni..huyu Tundu ni mtu makini sana kweny kupanga sentensi. Sema kwa kuwa siasa za kiafrica ni sayansi basi lakini kama si vingnevo huyu atakuapua kura nyingi za wananchi. Na ikulu a naiona kimo cha mbuzi asbui na mapema 28.10.2020!!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Huu mwaka naaamini utazaa matokeo tofauti, anything can happen. Mi huwa naamini hakuna kinachoshindikanaga hii dunia. Halafu pia udhaifu wa Magufuli ndio utawapa shida wataotaka kumpa ushindi wa mezani. Ni ngumu sana kumbeba asiyebebeka
 
Charisma - compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others.

Kwa tafsiri ya kiswahili, Charisma ni ule mvuto mtu anaokuwa nao mpaka unatamani kama anaongea aendelee kuongea.

Katika siasa Charisma ni kitu cha umuhimu sana, kama huna Charisma, huwezi kuvutia watu wakakusikiliza.

CCM wana bahati mbaya sana kukosa viongozi wenye Charisma, ndo mana unaona kwenye kampeni wamekuwa wanatumia sana wasanii wa bongo fleva ili kuweka mvuto ambao ulistahili kuletwa na viongozi wao, kinyume chake ni sahihi kabisa, CHADEMA wana viongozi wenye Charisma ya hali ya juu sana, mtu kama Halima Mdee, Tundu Lissu, Mnyika, au Mbowe wakianza kuongea huwezi tamani ashushe mic, ni viongozi ambao wanaweza kuunganisha maneno mfululizo kwa lisaa lizima wakimwaga point ambazo hadhira inataka kuzisikia.

Nimemsikiliza leo Magufuli akiwa Shinyanga, honestly, unaona kabisa hata namna anavyounganisha sentensi, ni kama vile anakuwa anakosa coordination ya meneno. Magufuli anaweza kuongea sentensi kumi ambazo zinakinzana zenyewe kwa zenyewe, kitu ambacho kwa mtu unayemsikiliza ni rahisi sana kupoteza hamu ya kumsikiliza.

Ndo maana ya ule usemi wa kwamba, 'viongozi wanazaliwa' kama huna Charisma, huwezi kuongoza watu wakakupenda kwa sababu ni ngumu pia kwa mtu asiye na Charisma kuelewa changamoto za wengine. Ndo mana unamsikia Magufuli akituahidi tena kutumia mabilioni mengine ya kununua ndege.

Kama mambo yataendelea kwenda hivi, ni kwamba Magufuli ataonekana anaongea bila kuwa na hoja na mambo yanavoenda mvuto wa Magufuli kwa wapiga kura unazidi kupuputika, upande wa pili, Charisma inambeba Lissu kwa nguvu sana, wengine tulishakata tamaa na siasa lakini, namna Lissu anavofanya mambo mpaka sasa, ametuinua sana morali zetu, na hii yote ni nguvu ya Charisma aliyojaliwa ambayo wengine wamenyimwa.
Amen🙏
 
Charisma haikupeleki ikulu. Kuna kasiri ka muhimu sana kanakupeleka ikulu
Ingekuwa tunaamini sana hicho unachokiita siri, Africa ingekuwa bado inatawaliwa na wazungu.

Kilichotufanya Africa ikapata uhuru ni uhodari wa viongozi wazuri wenye Charisma kama kina Nyerere.

Kwahiyo sielewi kwanini una downplay nguvu ya Charisma.
 
Kiukweli upande wa upinzani tulikuwa tushakata tamaa mm nikiwa mmojawapo, lakini molari imekuja kupanda ghafla
Issue kubwa kwa sasa ni kuhakikisha kwanza tundu lissu anakaa midomoni pa watu.

Siku ya kura watanzania tukapige kura kwa wingi, then tuone sasa huo ushindi wa mezani unakujaje.

Huu mwaka ni wa kipekee sana, bado naamini
 
anakinzana balaa. juzi aliwadanganya watu wa ikungi eti anampenda lissu akakinzana na ile kauli ya siku ya ripoti ya makinikia kuhusu kazi za wanajeshi kule kwenye vita.

atuachie nchi yetu hafai. hana utu. muuaji wa demokrasia. siyo mstaarabu.
Maana yake magufuli anahubiri asichokiamini hata yeye. Ni muongo kupindukia.

Mtu anayepingana na kauli zake mwenyewe siwezi kumpa kura yangu. At least ntatembea kwa ufahari kwamba nafsi yangu ilishamkataa
 
Unajua huyu jamaa alijinadi sana (mtu wa press)kila siku saa hivyo watanzania ni kama walimzoea sana sasa hata asimame kwenye jukwaa la shaba ule mvuto haupo tena watu washamwona wa kawaida sana.
 
Jamaa kilichobakia sasa, anatakiwa tu kusoma hotuba aliyoandikiwa na wasaidizi wake, na tena asome "word by word" na kwa utulivu na wala pasipo kuingiza vionjo vyake mwenyewe ama utani wowote ule.

Kwa maana hata akijaribu kufanya utani anajikuta anatumia maneno magumu ambayo hutuma ujumbe kwa walengwa kama anatoa kashfa. Akikwazika ama kuudhiwa hapo ndipo inageuka kuwa balaa nyingine, hasira zote zinakuwa ktk mafaili anayolala nayo chumbani kwake, hapo ndipo tumbua na teuzi zinapoanzia kwa wasaidizi wake.

Wewe ogopa mtu ambaye wasaidizi wake wengi wa karibu waliokuwa serikalini wamekimbia nyadhifa zao ili kutaka kwenda kutafuta unafuu wa "stresses" ktk ajira za mhimili wa bunge.
Mara nyingi jamaa akifanya utani lazima awaaibishe wanawake, sijui ni kwanini?
 
Back
Top Bottom