Uchaguzi 2020 Chato: Msafara wa Tundu Lissu washambuliwa kwa mawe

Uchaguzi 2020 Chato: Msafara wa Tundu Lissu washambuliwa kwa mawe

Tukiwa na Taifa la watu kama wewe ni hatari sana.

Watawala ndio wanaotaka iwe hivyo lakini wao hawafanyi hivyo mana wanajua kuwa siasa ni sehemu ya maisha yao.
CCM wengi wanajali familia zao na maisha yao ndio kama unavyosema na ndio maana haya maovu yote yanatokea.

Ni wanyama tu ndio wanaojali maisha yao na watoto wao tu. Lakini Binadam anapaswa kujali maisha ya kila mmoja yawe ya haki. Ndio maana kuna wanajeshi wanaotoa maisha yao kwa ajili ya wengine waishi kwa amani na raha mustarehe. Mara nyingi hawa ni wale wanaotoka katika familia duni na wamekosa Fursa. Huwezi ukamkuta mtoto wa Waziri anakua Polisi au Mwalimu wa shule ya msingi au Sekondari ya Kata. Huwezi ukamuona mtoto wa Rais anakua Mgambo akalinde Geti la soko au la ushuru wa mazao.

Binafsi nawaheshimu sana watu wanaosimama upande wa maskini na upande Dhaifu. Hao ndio wanaopanda mbegu ya haki na mabadiliko tangu enzi za manabii.

Hivi unadhani Gwajima anaweza kugombea ubunge kupitia Chama cha upinzani wakati ni bilionea na ameshazoea maisha ya Raha.
Mara nyingi hua namtafakari JPM kuwa kama ni kweli ana uchungu na nchi hii mpaka anaona kuwa urais ni mzigo mkubwa je, ni kwa nini alishiriki katika maamuzi yote mabaya yaliyoliletea taifa hili hasara kubwa na kuibiwa tangu awamu ya Tatu?

Kwa nini hakuwahi kuipinga serikali na kuikosoa wazi wazi badala yake amekua akiitumia serikali kuwaumiza wananchi wakati akijua wazi kabisa kuwa Makosa yote yalisababishwa na serikali zilizopita. Mfano kuacha watu wajenge hovyo halafu anakuja anatumia dola kuwavunjia bila fidia .

Alipaswa akatae na kusema hawa ni watu wanyonge na maskini siwezi kuwavunjia bila kuwalipa fidia mana serikali ndiyo ilizembea watu wakawekeza fedha zao hapo. Hajawahi kusema wala kuumizwa na uonevu wa watu zaidi ya kuwaumiza . Nyumba za serikali ziliuzwa zote kwa makada wa CCM kwa bei ya kupeana huku wakijua wazi kuwa Tanzania ni nchi ya KIJAMAA lakini hakuwahi kupinga huo uporaji wa Mali za umma uliofanywa na wanaCCM kwa uroho wa kumiliki Mali zote za nchi hii.

Hakawahi kufanya kama alivyofanya Mrema alipoipinga serikali kwenye Kashafa ya Chavda na nyingine ,akaamua kuipinga serikali na akafukuzwa uwaziri kwa kusimamia Haki. Mrema alipata umaarufu wa kweli pamoja na kukosa Urais kutokana na kizingiti cha Mabilionea wanaomiliki Mali zote za nchi hii na vyeo vyote na familia zao. Mrema alikua ni mzalendo wa kweli mtetezi wa wanyonge mana alijitoa mhanga kupoteza madaraka ili asimamie haki.

Hawa wengine ni wazalendo wa kupigania maisha yao kama unavyoshauri ili wapate maisha mazuri.

Tumshukuru Mungu kwa kuwaleta duniani watu wasioangalia maisha yao binafsi. Ingekua wote wana roho za ubinafsi utumwa na ukoloni mpaka Leo ungekuwa upo Duniani . Afrika kusini imepata Uhuru kwa sababu ya vijana waliokua wamejitolea kupigania Haki.

CCM inaongozwa na mabilionea waliotumia Fursa ya Kujiita wajamaa na kupora Mali zote za umma kupitia madaraka.
Nyumba zote za Osterbay. Masaki, Upanga , Na maeno yote muhimu kwenye miji yote iliporwa na Makada wa CCM wakiopo na waliopita . Walishirikiana kujilimbikizia mali kupitia madaraka.

Watu kama hao ambao kwao uongozi ni biashara inayowatajirisha sana huku wakiwa wanaweza kufanya wanachotaka kwa MTU yeyote bila kuulizwa na MTU yeyote usipokua MTU mmoja tu ambaye ni Rais ,kwa maana kwamba akikaa kimya ndio basi; kamwe huwezi kushindana nao bila kuwa na watu wanaoweza kujitolea na kukabilana nao .

WanaCCM wengi wanaogonbea mpaka Udiwani ni wale wenye utajiri mkubwa , wanachofanya ni kumwaga pesa na kuandaa vijana ili wafanye vurugu hata kuua watu na wakija polisi kuchunguza wanawahonga mapesa ili taarifa zibadilishwe ionekane kuwa hakuna jambo baya lililofanywa na WanaCCM hao hivyo panakua hakuna Kesi.

Uroho wa Makada wa CCM umezalisha taifa la watu waovu wasiojali uhai wa MTU mwingine asiye na faida ya kimadaraka kweo.
Ditopile marehemu alipiga MTU risasi hadharani lakini kutokana na ukada wake wa CCM kesi ilibadilika na kuwa ndogo kabisa na kuachiwa. Mungu ndiye aliyeamua mwenyewe kama atakavyoendekea kuamua dhidi ya madhalimu..

Haki itasimama hata kama Viongozi wa dini wote watanunuliwa na kusema kuwa wao ndio wanaoamua ipi ni haki na ipi ni dhuluma. Yani kwa sasa viongozi wa dini hawajui kutofautisha kati ya haki na wajibu wa serikali kujenga miundo mbinu kwa kodi za watu. Kwao miundo mbinu ni kazi ya MTU anayejitolea na sio Kuwa na Bunge linalopanga kuwa Pale pajengwe daraja na likajengwa na Bajeti ikatilewa bila kutesa na kuuana kwa ushabiki.

Yaani kwa sasa mpaka viongozi wa dini wanaongea kwa kuuma meno utafikiri kuna mtu amechukua sadaka yao akainunulia sigara. Mchungaji anaongea kwa hasira kabisa na kwa chuki utafikiri Naye ni mgombea kama Gwajima . Eti tumchgue Huyu ni mchaMungu na yule ni msaliti . Wamesahau kuwa Yesu alikataa kupewa Fahari za dunia kwa kupinga kumsujudia Shetani. Viongozi wa dini wameonyeshwa fahari ya dunia na kumsuhudia CCM mkuu.

Hii ni post bora kabisa katika Uzi huu. Ni watu wachache sana wanaoweza kuwaza hivi, na kuweka mawazo yao vyema katika mtiririko huu.
 
Watoto wao Kivipi wakati nimeshakuambia kuwa dunia hii kuna watu wameumbwa ili watetee maisha ya wengine.

Hivi nyie CCM madaraka ndio mnatoaga watoto wenu kwenda kupambana na majambazi au Magaidi?

Hivi vurugu zinatokana na Watu kupiga kura na kamapeni au zinatokana na dhuluma zinazofanywa na Wasimamizi ambao kiukweli wanapaswa kusimamia Haki.?

Hivi ni wapi ambapo hua hapatokei fujo haki inapokosekana.

Ni mpumbavu tu atakuunga mkono kwa sababu hujui gharama za watu wanaojitolea kwa ajili ya wengine ilivyokubwa.
Hata CCM wanawatangulia polisi ambao ni watoto wa maskini kwenda kuua watu na kupata maadaui huku wao wakinywa bia na kujilimbikizia mali . Haoa hao polisi akipewa rushwa ya buku mbili wanamfukuza kazi kama mbwa na kumtungia sheria ya kikokotoo. Hiyo ndiyo haki! Watu walioingia madarakani kwa rushwa na dhulma watawezaje kwenda kuongoza watu na kupinga rushwa ?
Nyie ndio mnaojiwaza tu matumbo yenu ndio maana hamjali hata ujai wa watu wengine alimradi mnapata kwa kupitia ujambaza kuuza madawa na mikataba mibovu . Nchi imejaa mikataba mibovu kwa sababu hamjali kuisoma kwa makini ili muifanyie marekebisho ,mnachoangalia ni 10% . Wabunge wa CCM hawataki uhuru wa Bunge na Bunge Live ili watete wengine. Wako pale kuangalia nafsi zao ili Mwenyekiti asije akawafukuza au kukata majina yao. Hiyo ndiyo dunia unayoitaka . Dunia ya watu wanaofanana na wanyama. Dunia ya watu ambao hata akipita na kuona Unaporwa au Kupigwa watu wakae kimya mana hayawahusu na hawawezi kuingilia kumsaidia mtu mana wanaweza wakaumizwa kwa kumtetea mwingine.
Mnataka dunia ambayo Polisi wakipigiwa siku kuwa kuna uhalifu waogope kwa sababu nao ni binadamu wanajali maisha yao na familia zao , na anayeibiwa ni mtu mwingine.

Kila unachokifurahia leo kuna watu waliumia kwa sababu hiyo.
Leo wakina Gwajima Kakobe na Wengine unaowaona wakiunga mkono fahari za Dunia na kukataa Haki na usawa kwa wanadamu huku wakihakasisha kuwa wengine ni wasaliti na hawapaswi kuishi ,wakesahau kuwa kuna waliopigania Haki ya kuabudu na uhuru wa kuabudu. Marehemu Moses kolola aliteswa sana alipoanza kuhubiri Ulokole Tanzania wakati wa Awamu ya kwanza na kuitwa mchochezi kwa sababu tu aliyakosoa makanisa makongwe na hayo ndiyo yaliyokuwa na matajiri wengi na watawala walisali huko. moses Kolola alijitoa kutetea kila anachokiamini mpaka alipokuja Mwinyi ambaye ni muislam lakini mwenye Utu na aliyeguswa na shida za wengine akaamua kuwa Kolola asibughudhiwe kwani ana uhuru wa kuamini anachoona kinafaa ,akasema Ruksa. Mwinyi akapigwa vita na wagandamizaji na waroho wa damu za watu wanaopenda kuona binadamu wenzao wakiteseka kwa umaskini na kukosa uhuru huku wao wakiwa na maisha safi.

Suala la Akwilina lilipaswa liwaguse wahusika wote.
Aliyepiga risasi binadamu mwenzake kwa sababu ya ukereketwa alipaswa awajibishwe.
Mkurugenzi aliyeacha kutimiza wajibu wake kwa haki alipaswa awajibishwe.
Mbowe aliyehamasisha maandamano bila kibali alipaswa naye awajibishwe. Hiyo ndiyo haki !! Damu ya Akwiline ,Damu ya Karume,Damu ya Dr.Sengondo Mvungi,Damu ya Alfonsi mawazo, Damu ya Wazanzibari wapatao 27 2001 , Damu ya Sokoine, Damu ya Horace Kolimba, Damu ya Azori Gwanda, Damu ya Ben Saanane iliyomwagwa kwa sababu tu ya misimamo yao na mawazo yao Hakika Mungu na asili ya Viumbe itajibu kwa vizazi vya wahusika.
Sengondo na Sokoine walitangulizwa na akina nani ?
Wapumzike kwa amani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natamani kujua washambuliaji ni akina nani, wametumwa na nani na kwa maslahi gani, so far polisi wamechukua hatua gani?

Haya mambo yanaleta picha mbaya sana kwa ccm
umechelewa sana!
 
Yaani nimecheka kwa nguvu, halafu inaonekana ww utakuwa ni Mzee lazima, maana ndio huwa wanatumiaga maneno kama haya ya kwako. Yaani watu tuone mtu katekwa kabisa uniambie siasa ni somo pana sana! Mimi nazungumzia uhalisia wa siasa, ww unaniletea habari ulizokaririshwa kwenye chuo cha siasa hapo kivukoni. Kaa Kimya tu maana huna jipya.
Uzee sio tatizo wala ugonjwa. Wenye mawazo mazuri na mabaya wote huzeeka. Kama walivyokuwa kuwa akina Mandela na sasa akina Mtei, Warioba...n.k Ukizaliwa tu na ukaishi muda mrefu bila kufa ujue uzee utakuja tu. Na mwisho, ujana pekee si kigezo cha mawazo mapya na chanya. Kuna vijana “wamezeeka” kimawazo mpaka wanatoka unga.
Nilitaka tu kufunguka kwenye hilo.
 
Ni vigumu sana kwa Tajiri(CCM)kuingia katika Ufalme wa Mbinguni(IKULU)kama ilivo vigumu kwa Ngamia(Magufuli) kupenya kwene Tundu(Tundu Lissu) la Sindano(Sanduku la Kura)!😂😂😂
Kwa 2020 ni vigumu sana. Dalili zote zinaonesha hivyo
 
Mwambieni kichaa wenu Lissu kwamba aache lugha za kifedhuli dhidi ya Rais, na pia anapoomba kura sio mpambano wa yeye binafsi na Magufuli aache kumuattack perosanally ashadihishe hoja kati ya chadema na ccm sio magufuli na Lissu, akiendelea hivyo atapigwa maeneo mengi tu nje ya Chato
Kati ya watu ambao hawafati maelekezo ya wajinga ni pamoja na LISSU.

Magufuli na jeshi lake walipomshambulia kwa risasi ilikuwa sawa?

Magufuli ni mgombea kama alivyo Rungwe, kama anataka asisemwe mabaya yake basi akatawale familia yake.
 
Hutawasikia tume ya uchaguzi wakilaani kwa vile ni chadema wanashambuliwa ,ingekuwa CCM ndo wanashambuliwa utaona watakavyokuja kasi kulaani kama faru aliyejeruhiwa kwa risasi
Ile tume hata kama ni ya ccm aisee haijielewi. Hata kutoa japo matamko ya kuzuga tu hawawezi?
 
Uzee sio tatizo wala ugonjwa. Wenye mawazo mazuri na mabaya wote huzeeka. Kama walivyokuwa kuwa akina Mandela na sasa akina Mtei, Warioba...n.k Ukizaliwa tu na ukaishi muda mrefu bila kufa ujue uzee utakuja tu. Na mwisho, ujana pekee si kigezo cha mawazo mapya na chanya. Kuna vijana “wamezeeka” kimawazo mpaka wanatoka unga.
Nilitaka tu kufunguka kwenye hilo.

Hongera kwa kufunguka, ila huyo niliyemuambia kanipata vizuri.
 
Hutawasikia tume ya uchaguzi wakilaani kwa vile ni chadema wanashambuliwa ,ingekuwa CCM ndo wanashambuliwa utaona watakavyokuja kasi kulaani kama faru aliyejeruhiwa kwa risasi

Wanaopanga kushambuliwa kwa cdm ndio maboss wa hiyo tume, hivyo ccm wakikutana na madhila yoyote wanawatuma tume kuwatetea.
 
Chadema mnatengeneza movie za kihindi Tunataka Amani hatutaki vita
Haki kwanza.. Amani itakuwepo tu kukiwa na haki.
Swala vita mnalosema Lissu ametumwa na wazungu, unafikiri kama kweli ametumwa huyo IGP Siro atawazuia hao wazungu kweli wakija.
 
Back
Top Bottom