China ataiua US kwa presha, katangaza Kirin 9006C(chip) ya 5nm tech

China ataiua US kwa presha, katangaza Kirin 9006C(chip) ya 5nm tech

Naanza kuwaona waarabu wanatoka kwenye ramani aisee. Hali ni mbaya. Kama gari inakwenda 1000km per charge sio mchezo, kwenye website ya haya mabasi ya yutong wametoa basi za umeme, naona zina range ya 18 km itakuwa ni city buses kwa sababu zipo hadi hizi za mwendokasi.
Ni muda tu hapo na bus watatoa za 1000 km/charge.

Kuna mchezo serikali inafanya tuendelee kuhangaika na gari za mafuta, ile issue ya gari za Mahindra kutoka India, itakuwa ni issue ya kupambania biashara za wakubwa, kuna wababe wameshavuta gari za umeme hapa bongo.

Na kinachokwenda kutokea bidhaa kama hizi zikianza kuzalishwa China, ni wewe na bei yako, serikali inawaza sana.
Wanajifunika shuka kumekucha.
Nchi ya wachumia tumbo haiwezi zuia maendeleo ya kisayansi sanasana itachelewa na itajiumiza yenyewe. We huoni hata Waarabu wenyewe wameanza diversification ya oil dependent economy. Saudi Arabia hiyo hapo 50 Cent anapiga show😂

Waarabu smart kama UAE na Qatar hawataki ujinga wako na sovereign wealth funds wanawekeza sehemu tofauti.
 
China ina space technology inayokua haraka ila haina kelele kabisa na taarifa zake zimekuwa ignored na dunia. Watu ukiwaambia China inaizidi Russia kwenye space technology wanabisha.

Kwa sasa kwenye space itakuwa dominated by the US and China.
Yes, shida ni kwamba sisi tunafuatilia sana vitu vya west kuliko china. Hata picha za mars nyingi ninazoona ni za.kifaa cha kimarekani wakati china naye anakifaa chake pale kinafanya utafiti.
We are less informed about china ni mpala uwe unapenda kufuatilia vitu ndipo utajua hatua alizopiga
 
Huawei P60 ina run 5G mpaka satellite call nafikiri kwa makampuni yote duniani ya simu upande huo kwa matokeo mapya wao wanaongoza
Huawei P60 na P60 Pro zinatumia chipset ya mmarekani "Qualcomm Snapdragon 8+ Gen 1 4G

Ikiwa hardware ya simu tu inasupport mwisho 4G, hiyo Huawei P60 imepatia wapi uwezo wa ku-run 5G?
 
Yes, shida ni kwamba sisi tunafuatilia sana vitu vya west kuliko china. Hata picha za mars nyingi ninazoona ni za.kifaa cha kimarekani wakati china naye anakifaa chake pale kinafanya utafiti.
We are less informed about china ni mpala uwe unapenda kufuatilia vitu ndipo utajua hatua alizopiga
Unaisema James Webb telescope? Sidhani kama kuna kenge yeyote anaweza jitutumua kutengeneza dude kama lile hata tumpe miaka 10. James Webb kuna Uzi niliizungumzia wakati imerushwa, it's a very advanced technology. China kwa hapo bado mkuu, ingawa picha zake ni nzuri pia
 
Huawei P60 na P60 Pro zinatumia chipset ya mmarekani "Qualcomm Snapdragon 8+ Gen 1 4G

Ikiwa hardware ya simu tu inasupport mwisho 4G, hiyo Huawei P60 imepatia wapi uwezo wa ku-run 5G?
Atakuwa alimaanisha mate 60 pro si p60
 
Kilichopo kati ya US na china ni sawa na vita baridi ua tech.
Inahitaji uwekezaji. China ana pesa ya kutapanya nyingi tu kwa sasa anaweza kuitapanya kokote kwenye agency zake. Na ndio maana ulaya wamekuja kushtuka china anataka kunua kampuni zao zote ambazo zinashikilia technology adimu hadi sasa wameweka vikwazo haijalishi ni private company haziuzwi kwa mchina hivi hivi.
The game is on... Tutazame nini kitafuata
Natarajia vikwazo vipya vya China toka Ulaya kuhusu national security na by the way ni ulinzi wa uhai wa makampuni yao hasa upande wa EV

Maana usalama wa makampuni ya nyumbani yamewekwa hatiani kutokana na mchina kulivamia soko la ulaya na duniani kwa kiasi kikubwa.

Kuhusu China kuwa na pesa ni kweli pesa anayo na ruzuku anatoa sana tu tena kwa sasa hasa upande wa teknolojia.

Serikali ya Chna wana utaratibu kila baada ya kipindi cha muda fulani wanakuwa na national plan fulani kwa ajili ya sekta fulani wamefanya hivyo kwenye sekta mbalimbali na sasa kwa wamejiza titi upande wa teknolojia zote hii ni national plan.

Serikali yao inatoa pesa na inaongeza ushirikiano na kuwapa support kubwa yale makampuni yanayo onesha mwangaza katika eneo fulani na wanajenga research centers nyingi sana sasa.

Ila pesa sidhani kama wanatoa hovyo hovyo ila makini mkubwa na kwa hesabu kali kulingana na target yao.

Hawa mabawana wana kimbizana na muda by 2049 watakapo fikisha miaka 100 kuna target kama taifa wamepanga lazima wazifikie kabla ya huo muda hivyo ndio maana wapo race kwenye kila angle
 
Unaisema James Webb telescope? Sidhani kama kuna kenge yeyote anaweza jitutumua kutengeneza dude kama lile hata tumpe miaka 10. James Webb kuna Uzi niliizungumzia wakati imerushwa, it's a very advanced technology. China kwa hapo bado mkuu, ingawa picha zake ni nzuri pia
Mkuu lile dude limeanzwa tengenezwa 2004 kwa ushirikiano wa nasa na shirika la anga la ulaya.
Ukiangalia mpaka linakamilika na kurudhwa ni miaka mingi kaisi kwamba kuna baadhi ya vitu ndani yake vitakuwa outdated.
So, mimi ninaamini watu wanaweza kutake advantage ya tech ya sasa kuunda kitu bora zaidi.
Njia aliyosema atatumia alitoa sababu kwanini ni better kuliko kuweka darubini sehemu moja
 
Huawei P60 na P60 Pro zinatumia chipset ya mmarekani "Qualcomm Snapdragon 8+ Gen 1 4G

Ikiwa hardware ya simu tu inasupport mwisho 4G, hiyo Huawei P60 imepatia wapi uwezo wa ku-run 5G?
Huawei sasa haitumii chochote kile cha marekani waliwekewa vikwazo kwenye kila kitu.

Na hiyo model mpya ya Huawei kila kitu ni kutoka China upo nyuma ya muda sana
 
Yes, shida ni kwamba sisi tunafuatilia sana vitu vya west kuliko china. Hata picha za mars nyingi ninazoona ni za.kifaa cha kimarekani wakati china naye anakifaa chake pale kinafanya utafiti.
We are less informed about china ni mpala uwe unapenda kufuatilia vitu ndipo utajua hatua alizopiga
Nimefuatilia juujuu hiyo China National Space Administration "CNSA" au kwa Kichina inaitwa (Zhōngguó Guójiā Hángtiān Jú) nimeona imeanzishwa miaka 30 iliyopita na budget yake ni $8.9 Billions kwa mwaka. Nimefuatilia na mambo walioyafanya. Iko vizuri. Sio fair kuifananisha na Space X ya miaka 21 iliyopita ila bado hiyo CNSA sio ya kufananisha na NASA

Kama Space X tu ni ya private sector huko Marekani lakini ukiangalia na hiyo CNSA sioni kama wameachana mbali kihivyo tena CNSA inamilikiwa na serikali kabisa

NASA imeanza miaka 65 iliyopita na budget yao ni $25.4 Billions kwa mwaka. Wana mafanikio mengi sana kushinda CNSA na kwa kuwa wameanza kitambo wapo umbali mrefu sana mbele ya CNSA. Kufananisha CNSA na NASA ni njia nyingine ya kuitukana NASA.

CNSA inaweza kuwa vizuri kuliko Space X ila kamwe haiwezi kuifikia NASA hata kidogo na best part ni kwamba NASA nayo ni ya Marekani
 
Kwenye smartphones Huawei ameshaumizwa na Mmarekani

*Huawei P60 Pro ni simu expensive kama shilingi milioni mbili hivi na bado inaishia internet speed ya 4G tu kutokana na limitation za chipset ambazo Mmarekani amempatia, Nani anataka simu expensive isiyo na 5G tena haiko optimised na Google services

Huawei ataendelea kutengeneza simu zenye hardware nzuri ila kwenye software atakosana na wengi. Sio kwamba software yake ni mbaya ila haiko optimised kwa matumizi ya Google services, plus app developers wako busy na kutengeneza apps kwa ajili ya Android na iOS sio HarmonyOS.

Huawei itabidi aendelee kutumia Android kwenye simu zake za Ulaya maana bila Mmarekani hatoboi. Hiyo HarmonyOS aiache kwa Wachina hukohuko

Huawei kwenye soko harudi tena. Kwa China kwenye simu ongelea kampuni kama Xiaomi, Oppo, Vivo, One Plus, Honor, nk ila sio Huawei tena
Huawei yuko sokoni ametoa Mate60
 
Unaisema James Webb telescope? Sidhani kama kuna kenge yeyote anaweza jitutumua kutengeneza dude kama lile hata tumpe miaka 10. James Webb kuna Uzi niliizungumzia wakati imerushwa, it's a very advanced technology. China kwa hapo bado mkuu, ingawa picha zake ni nzuri pia
JWST hatari sana
 
Huawei sasa haitumii chochote kile cha marekani waliwekewa vikwazo kwenye kila kitu.

Na hiyo model mpya ya Huawei kila kitu ni kutoka China upo nyuma ya muda sana
Hahaha hiyo Mate 60 Pro ambayo imemtegemea Mchina inawafaa Wachina sio ulimwengu
Dunia bado inahitaji Google services na haina muda wa kusubiri app developers waanze kutengeneza app kwa ajili ya HarmonyOS pia
Hizo Petal Search, Petal Maps nk zinawafaa Wachina. Dunia inataka Google search, Google maps, nk
 
Nimefuatilia juujuu hiyo China National Space Administration "CNSA" au kwa Kichina inaitwa (Zhōngguó Guójiā Hángtiān Jú) nimeona imeanzishwa miaka 30 iliyopita na budget yake ni $8.9 Billions kwa mwaka. Nimefuatilia na mambo walioyafanya. Iko vizuri. Sio fair kuifananisha na Space X ya miaka 21 iliyopita ila bado hiyo CNSA sio ya kufananisha na NASA

Kama Space X tu ni ya private sector huko Marekani lakini ukiangalia na hiyo CNSA sioni kama wameachana mbali kihivyo tena CNSA inamilikiwa na serikali kabisa

NASA imeanza miaka 65 iliyopita na budget yao ni $25.4 Billions kwa mwaka. Wana mafanikio mengi sana kushinda CNSA na kwa kuwa wameanza kitambo wapo umbali mrefu sana mbele ya CNSA. Kufananisha CNSA na NASA ni njia nyingine ya kuitukana NASA.

CNSA inaweza kuwa vizuri kuliko Space X ila kamwe haiwezi kuifikia NASA hata kidogo na best part ni kwamba NASA nayo ni ya Marekani
Space x huwezi kuifananisha na CNSA maana mafanikio na vitu ilivyofanya CNSA space X hajafanya hata robo. Ndio maana nimekuuliza zaido ya kufanya majaribio na kurusha satelites na kuunda reusable rockets space x kafamya nini cha ajabu zaidi?
Unajua kwanini kwa wamarekani space x ilionekana big deal?
Ni kwa sababu baada ya kuground space shuttle program, ambayo ilikuwa ya Nasa, marekani alianza kutegemea nchi kama russia, india na umoja wa ulaya kurusja satelites. Ndio maana space x akaja kuwaondolea aibu hiyo.
Turudi kwenue CNSA,
Nasa ni mkongwe historia inambeba ila kwa kipimdi kifupi mambo aliyoyafanya CNSA ni makubwa mno hata collabo la shirika la anga la ulaya hawayafikii hata robo.
China kwa sasa naweza kusema ndiye mshindani wa moja kwa moja wa US kwenye anga.
Halafu sometimes budget si hoja. Hivi unajua chombo cha India alichokipeleka mwezini budget yake nzima haifikio hata budget ya movie ya kimarekank ya interstellar? Ni kama nusu ya budget ya hiyo movie.
 
Huawei yuko sokoni ametoa Mate60
Watu hawataki kutoa hela zao kununua vitu kwa mashakamashaka

Kwa nini ununue Huawei expensive isiyo na Google services legally wakati Xiaomi, Oppo au Vivo zenye Google services zipo
Yani unanunua simu expensive then unaanza kuhangaika kukesha mitandaoni "How to get Google services in Huawei phones [emoji1][emoji1]"
Dunia haina huo muda, Ni wachache wapo tayari kuhimili usumbufu huo otherwise inawafaa Wachina tu
 
Huelewi the technical part ya vitu.
Narudia kuna virtual boxes zinaweza kuund amazingira ya kurun kitu. Harmony Os ina apps zake ambazo pia zina run kwenye harmony OS na wala si za android. Previously ilikuwa ina run apps zake kama kawa na za añdroid kupitia inbuilt emulator, sijui toleo la hivi karibuni kama linaendelea kurun android apps au inarun za harmony OS tu.
Badla ya kubishana na mimi hebu basi chukua muda usome virtual boxes au emulators zinavyifanya kazi uelewe kuwa unaweza tengeneza mazingira ya kurun kitu kingine cha OS fulan kwenye Os fulan kupitia emulators.
Mfano chief mkwawa alikuwa anasema anacheza games za symbian kupitia emulators kwenye android. So ina maana ana install games za symbian na kuzicheza kwenye android, hili haliifanyi android kuwa symbian
Haelewi huyu ,hata android apps unaweza kifungua na kuzitumia kwenye windows kupitia blue stacks
 
Hahaha hiyo Mate 60 Pro ambayo imemtegemea Mchina inawafaa Wachina sio ulimwengu
Dunia bado inahitaji Google services na haina muda wa kusubiri app developers waanze kutengeneza app kwa ajili ya HarmonyOS pia
Hizo Petal Search, Petal Maps nk zinawafaa Wachina. Dunia inataka Google search, Google maps, nk
Naona unabadili beat tu haya bwana dunia inabadilika sifikiri hata wao marekani na ulaya wanapenda ushindani China anaowapa ila shida hawana namna ndio imekwisha tokea.

Na ubaya wa mtu wanaye dili naye sasa amekwisha wahi kuwa superpower duniani kwa maelfu ya miaka na kuanguka na kuwa superpower tena na kuanguka inshort anajua mbinu zote za kuwa juu.

China nafikiri ndio taifa pekee superpower la kale kwa maelfu ya miaka iliyopita lipo hai mpaka sasa na ni superpower so mbinu zote za kuwa wakubwa wanazijua.

Na ubaya zaidi wana hasira za kwa nini walitawaliwa kitu ambacho sisi waafrika tumekosa kuwa na hasira ya kwa nini tulifanywa watumwa na kutawaliwa
 
Watu hawataki kutoa hela zao kununua vitu kwa mashakamashaka

Kwa nini ununue Huawei expensive isiyo na Google services legally wakati Xiaomi, Oppo au Vivo zenye Google services zipo
Yani unanunua simu expensive then unaanza kuhangaika kukesha mitandaoni "How to get Google services in Huawei phones [emoji1][emoji1]"
Dunia haina huo muda, Ni wachache wapo tayari kuhimili usumbufu huo otherwise inawafaa Wachina tu
Lakini imeuza kiasi kwamba ameshindwa kumeet demand. Hapa anataka kupeleka production nyingine ifanyike hong kong. Demand ya simu ya mate pro na mate pro 60 imezidi uwezo wake wa uzalishaji.
 
Back
Top Bottom