China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

Kipilipili tafadhali naomba namba yako nataka nikuulizie

mkuu unaweza kuuliza hapa ili na wengine wafaidike. Au kama ni ishu binafsi naomba njoo PM, nimesitisha kutoa namba yangu kwa sababu baadhi yetu sio wastaarabu na mimi lengo langu hapa si kufanya biashara ila kusaidia TAARIFA tu.
 
Siko la asali sina details za soko lake hapa China.

Natoa wito kwa wengine wanaotaka ku export bidhaa zao nje ya nchi wanitumie majina ya vitu hivyo kisha nitavituma kwa wahusika

mkuu NAKUHAKIKISHIA demand ya asali ni kubwa sana kwa china, japokuwa utahitajika kuingiza bidhaa zenye ubora na packaging nzuri. sina details kuhusu jinsi ya kuingiza lakini kama unaweza kupata mchina bongo mkafanya patnership/joint venture naamini itakusaidia sana kuingiza kwa urahisi na kupata faida nzuri.
 
Mkuu vipi machine au printa za kusafisha picha. Ambazo ni refarbished zinapatikana mji gani. Thanx in advance

mkuu hizi zipo Guanzhou kuna eneo linaitwa "Dashato" unaweza ukapata japokuwa nashauri ununue mpya kwa sababu bei zake si ghali sana tena kama utaamua kwenda kuzinunulia mji wa Shenzhen ambako ni jirani tu na Guanzhou
 
kipilipili, hongera sana, makala yako ni nzuri sana, ila hebu zungumza kidogo na opportunities za ku-export. website zipi mtu anaweza kutembelea akapata taarifa hizo?

mkuu, uzoefu wangu hasa ni wa kutoa bidhaa huku kuja Tanzania. Hili nitalifanyia kazi kisha ntaleta mrejesho In Sha Allah. nimewahi kuona baadhi ya watu wakileta mizigo china lakini wengi wamekua wakisema sheria na taratibu za uingizaji bidhaa huku zinabana ukilinganisha na nyumbani
 

nashukuru mkuu, naomba akisharudi mwambie akupe mrejesho na utuwekee hapa ili wengine wafaidike na tuendelee kusaidia na wengine. information is power na wengi tunakosa fursa za kupiga hatua mbele kwa kukosa taarifa sahihi.
 
nahitaj kujua gharama za kutuma mzgo toka China how much per kg?

mkuu ningejua unataka kusafirisha mzigo gani pengine ningekuwa kwenye nafasi nzuri ya kukushauri zaidi. mfano, kama unasafirisha bidhaa nzito au zenye upana mkubwa basi Meli ni bora zaidi kuliko ndege na ni cheap na hutapata hasara. kama bidhaa unayosafirisha ni nyepesi na size ndogo na unaihitaji kwa haraka basi usafiri wa ndege ni mzuri.
baada ya majibu hayo niseme tu vipimo vya KG hutumika sana unaposafirisha kwa ndege na yapo makampuni yanayisafirisha kwa dola kuanzia 8/kg na kuendelea kutegemana na terms na conditions. wengi ninaojua wanaosafirisha kwa bei hiyo itakulazimu ufanye clearence mwenyewe airpot. japokuwa yapo pia mengine ambayo yanafanya clearence ingawa bei yao iko juu kidogo.
 
Kipilipili...kuna soko la bidhaa ghafi nalihitaji kutoka china hasa viwanda vya biochemical...wapi naweza kupata directory yao
 
Ndugu Pilipili
tunashukuru sana kwa jambo hili ambalo unalifanya.
naomba kujuwa hali ya usalama katika hiyo miji, yaani kama kuna wizi wa mara kwa mara, uporaji na mengine kama hayo
 
looking ur a good clearing agent

Nipo. Tuna kamouni ilkyosajiwa kwa kazi hiyo. Tuna uzoefu wa kutosha. Kama jamaa alivyosema hapo mwanzo ni kazi iliyo na usiri ndani yake. Ni-pm.
 
I
Hatuna haja ya kusema wanabana. Hivyo ndivyo inavyotakiwa. Wachina wanatengeneza bidhaa zao wenyewe, wakiruhusu bidhaa za nje ziingie ovyo ovyo bidhaa za zitakosa soko ndani ya nchi yao wenyewe. Haiwezekani waruhusu magari na mitambo ya japan wakati wanajua kuwa wanayo ya kwao. Potelea mbali kama hayana ubora sana. Ndio maana China imebaniwa au kukataa kujiunga na WTO. Hapa kwetu tunaruhusu kila kitu mpaka sementi inayozalishwa na viwanda vyetu. Haya ukwepaji kodi kibao
 



Kwa wale ambao watapenda kupata access za huduma mbalimbali mbalimbali kutoka nje ya nchi hasa China wasisite kutumia hii android mobile App. Inaitwa Grab Overseas Market.

Ina resources kibao (nyingi bado kukamilika) kama vile suppliers, manaufacture, na other services. Pia wadau wa watanzania wanaweza kuweka products au services zao ili waweze kuiza nje ya nchi hasa China.


Niliahidi kuja na simple solution kwaajili ya kuwasaidia watanzania, nadhani mwanzo ndiyo huu.

Maoni yanakaribishwa.

Pamoja
 
Kipilipili...kuna soko la bidhaa ghafi nalihitaji kutoka china hasa viwanda vya biochemical...wapi naweza kupata directory yao


Kwa wale ambao watapenda kupata access za huduma mbalimbali mbalimbali kutoka nje ya nchi hasa China wasisite kutumia hii android mobile App. Inaitwa Grab Overseas Market.

Ina resources kibao (nyingi bado kukamilika) kama vile suppliers, manaufacture, na other services. Pia wadau wa watanzania wanaweza kuweka products au services zao ili waweze kuiza nje ya nchi hasa China.


Niliahidi kuja na simple solution kwaajili ya kuwasaidia watanzania, nadhani mwanzo ndiyo huu.

Maoni yanakaribishwa.

Pamoja
 
Ndugu Pilipili
tunashukuru sana kwa jambo hili ambalo unalifanya.
naomba kujuwa hali ya usalama katika hiyo miji, yaani kama kuna wizi wa mara kwa mara, uporaji na mengine kama hayo

hali ya usalama kiujumla inaridhisha tena sana. wenzetu wameweka ulinzi wa kila aina kila mahala.camera kila mahala kuanzia kwenye mabasi,taxi,mitaani na kwenye majengo. lakini wadokozi hawakosekani mahala popote duniani. unachotakiwa tu ni kutumi common sense tu kuangalia usalama wako binafsi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…