China kuisaidia Tanzania ujenzi wa SGR na mradi wa umeme Mto Rufiji

Fedha mtaani zikiwa vizuri serikali itafaidi sana. Serikali iangalie namna ya kuwafanya wananchi wake wawe matajiri. JPM hatojuta akifanya hili.
 
😀 😀 😀 😀 ama hujamwelewa mwenye nchi yake. Dona kantri isiyoweza kuongeza mishahara ya watumishi wake.
Isiyoweza Kutoa ajira, inayowafanya wananchi wake waishi kama mashetani. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwa kilio kikuu hapo baadae... Mchina ana roho mbaya haijawahi tokea.... Wanaofanya kazi na Wachina wanajua haya
Ila China wanaweza kutuvusha toka uchumi wa kati hadi dona katre
 
Weee hilo mzee hataki, anataka tulimie meno ili tuishi kama mashetani.
Tukilimia meno hatutakuwa na uwezo wa kupanda ndege wala SGR haitakuwa na kazi na hilo analielewa maana Rais si mjinga. Tuombe Mungu hii miaka mitano alifanye hili. Tupunguze kumkashifu na kumponda pia.
 
Natamani Tanzania tungekuwa tunarekodi na kuachia tapes za Marais wetu pale wanapostaafu kama wanavyofanya Marekani. Ningependa sana kusikiliza mazungumzo ya Nyerere, Magu na Mwinyi (Baba) na viongozi wa nchi nyingine.
 
Kwa kilio kikuu hapo baadae... Mchina ana roho mbaya haijawahi tokea... Wanaofanya kazi na wachina wajua haya

Huko Zambia sijui wamefanyaje! 😀 Yaani, ni kama mtu upo huna msaada halafu ndugu wanakugombania wakusaidie ila kumbe kila mmoja ana malengo na maslahi yake. Mwingine anataka uwe kibarua wake, mwingine ukae na wanaye, mara umlindie nyumba n.k.
 
Hii ni dalili kuwa hakuna hela ya kukamilisha hiyo miradi na sasa tunalazimika kutafuta fedha kutoka chanzo vingine wakiwemo wachina, watu ambao sio wema kabisa.Hiyo SGR itakuwa ni mali ya wachina pale tutaposhindwa kulipa deni na hiki ndio wachina wanachokitafuta.
 
Wachina twende nao kwa umakini mkubwa sidhani kama wana dini hawa!
China pia atafaidika na reli ya mpya ya SGR kwa kuwa inaunganisha China na vyanzo mbali mbali vya malighafi kutoka Congo, Rwanda, Burundi na Tanzania yenyewe na pia itatoa fursa kwa bidhaa nyingi za China kufika kwenye masoko kwa urahisi na kwa gharama nafuu. Mradi wa SGSR ni muhimu pia kwa uchumi wa China. Kikwete alishasema ukitaka KULIWA kubali na wewe ULIWE.
 
Chagua who is the best Beberu Mzungu Vs Mchina and discuss.
 
Tanzania nchi ya ajabu sana china kuna soko la makaa ya mawe lakini hapo kwenye simu sidhani kama waliongelea 🙄
 
China Imecheza na "gape".

Biashara/siasa duniani ni sawa na biashara ya daladala...ukisusia root fulani wenzio wanaichangamkia.
Afrika ni sawa na mrembo fulani wa uhakika, jamaa mmoja akijifanya ana hasira halafu akasusa, muda huo huo wengine haraka sana wanaziba pengo.
 
Wachina twende nao kwa umakini mkubwa sidhani kama wana dini hawa!
Wenye dini ndio waliotuuza utumwani, walitukata mikono walifanya mauaji ya halaiki na waanzilishi wa vita zote kubwa duniani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…