DOKEZO Clinic ya Marie Stopes Mwanza inatoa huduma za utoaji mimba (abortion)

DOKEZO Clinic ya Marie Stopes Mwanza inatoa huduma za utoaji mimba (abortion)

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Si njaa zake ndo zinamfanya aendelee kuwa kwenye hiyo taasisi Kama alivyobainisha si ndio ?

Swali, hiyo taasisi ikifungiwa ama kunyang'anywa leseni si atapoteza kazi ???

Mambo mengine unaachana nayo tu ! Hi dunia imejaa kila ushetani ! Watu wanafanya mpaka biashara za viungo vya binadamu sembuse abortion ??

Ukiona Jambo fulani halikufai kimaadili au kulingana na Sheria za nchi achana nalo ! Hii dunia haina huruma na mtu, watu wanaangalia pesa tu !
Mkuu acha apoteze kazi jamii ipone,siamini kama hajui hilo,maana hata kazi yenyewe inaonekana haifurahii tena kutokana na kulazimika kufanya kitu ambacho anajua wazi ni kosa.

Tunajua kwamba wanaotoa mimba hapo ni watu walioamua wenyewe lakini kufanywa na taasisi ambayo imeaminiwa Kitaifa kutoa huduma na watumishi wake kukiuka viapo vya maadili haikubaliki,likiachwa hili litaibuka lingine watoto watatekwa huko mitaani wataenda kunyofolewa viungo hapohapo halafu tutasema tena hayatuhusu huku watu wakipotea.

Lazima pawepo wa kujitoa mhanga,Leo hii Nyeyere angelambishwa asali na wakoloni tusingekuwa hapa,kuna watu walikufa Ili wengine tupone,ndivyo dunia ilivyo,uovu hautakoma na wema hautakoma pia.
 
Wewemdo unajua leo. Hiyoni taasis ya kimarekani ambayo lengo lake kuu ni kuadvocate depopulation duniani. Wanatunia kigezo cha family planning ili kuhalalisha agenda yao. Wapo duniani kote na wala hawana gharama kubwa sometimes wana ngo zao zinafanya abortion bure kabisa
Umekosea kidogo, Marie stopes SIO taasisi ya Kimarekani, ni taasisi ambayo makao makuu yake ni London, Uingereza, na funding yao wanapata kutoka Uingereza, wala sio Marekani.
 
Mkuu acha apoteze kazi jamii ipone,siamini kama hajui hilo,maana hata kazi yenyewe inaonekana haifurahii tena kutokana na kulazimika kufanya kitu ambacho anajua wazi ni kosa.

Tunajua kwamba wanaotoa mimba hapo ni watu walioamua wenyewe lakini kufanywa na taasisi ambayo imeaminiwa Kitaifa kutoa huduma na watumishi wake kukiuka viapo vya maadili haikubaliki,likiachwa hili litaibuka lingine watoto watatekwa huko mitaani wataenda kunyofolewa viungo hapohapo halafu tutasema tena hayatuhusu huku watu wakipotea.

Lazima pawepo wa kujitoa mhanga,Leo hii Nyeyere angelambishwa asali na wakoloni tusingekuwa hapa,kuna watu walikufa Ili wengine tupone,ndivyo dunia ilivyo,uovu hautakoma na wema hautakoma pia.
Well said.
 
Clinic ya Marie Stopes iliyoko jijini Mwanza wanajihusisha na vitendo vya utoaji mimba. Mimba zinatolewa sana pale, hasa za wanafunzi wa vyuo vikuu. Mchezo unaofanyika ni kwamba wanawake wanaohitaji hiyo huduma hufika hapo na huulizia huduma ya abortion, au kwa kujifanya mimba imeharibika.

Kinachofuata, mhusika anafanyiwa huduma inaitwa "dilatation and curateage", ambayo kimsingi ni kutanua njia ya shingo ya kizazi, kisha kuharibu mimba kwa kusafisha kizazi.

Sasa, the way wana record hiyo ili kuficha huo uozo ni wana record kama vile mtu alikuja na "miscarriage" tayari au "incomplete abortion" halafu kuwa wao wakasafisha tu kizazi kuondoa mabaki yaliyobaki kwenye kizazi, lakini ukweli ni kwamba wanakua wameharibu mimba na kufanya abortion ila kwenye rekodi zao wanaonyesha kama vile ni incomplete abortion.

Kuna uwezekano pia timu ya usimamizi wa huduma za afya ya halmashauri na hata ya mkoa inajua kabisa mchezo unaoendelea lakini wananyamazishwa kwa bahasha, maana hizi habari ziliwahi kuripotiwa kwao lakini hakukua na hatua zozote ziulizofuata.

Pia, hawa watu kuanzia wakati wa usahili kama unataka kuajiriwa pale kama daktari au muuguzi, wanakuuliza kabisa wewe mtazamo wako kuhusu utoaji mimba ukoje, na wanakupa scenario kuwa ikitokea wakati unatimiza majukumu yako halafu akaja mteja ambae anataka kutoa mimba je utachukua hatua gani? Ukitoa majibu ambayo yanaonyesha kama vile unapinga mambo ya abortion, wanakuchinjia baharini hupati hiyo kazi.

Tukumbuke kuwa kwa nchi yetu, utoaji wa mimba (abortion) ni kinyume cha sheria za nchi.

Nimeona nifichue hili jamani nimechoka vitendo hivi kila siku nashiriki utoaji mimba ila ni kwa sababu ya njaa tu, nimeona nije kutoa ripoti huku, Wizara ya Afya Tanzania fuatilieni hili mchukue hatua.

Nendeni pale kagueni records zao muone walivyo na "incomplete abortion" kibao ambazo wanazifanyia dilatation and curatage, hizo zote ni mimba ambazo zimetolewa hakuna cha incomplete abortion wala nini.

Fanyeni uchunguzi kwa makini, mtagundua kitu, ila msiende kichwa kichwa.

Asante.
Hahaha...eti "umeona ufichue", uko ulimwengu wa ngapi ndugu? kipi kisichojulikana kuhusu Marie Stopes?
 
Hivi mfano umempa mwanafunzi mimba
Kipi Nafuu?
Uende jela miaka 30 kumpa mimba mwanafunzi
Au umepeleke akaflashiwe mimba kesi iishe[emoji848]

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa nini uwe na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi in the first place? Unafanya mapenzi na mwanafunzi, tena kavu kavu, sasa kwa nini usiozee tu jela?
 
Back
Top Bottom