Code alizonipa mzungu zimenisaidia kuona mwanga wa mafanikio yangu na familia yangu hapo baadaye

Code alizonipa mzungu zimenisaidia kuona mwanga wa mafanikio yangu na familia yangu hapo baadaye

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu wana JF wenzangu,

Kwanza nianze kusema kwamba mimi ni miongoni mwa watanzania waliozaliwa katika familia ya maisha ya kati, sio familia tajiri wala masikini.

Pilika pilika za hapa na pale, zilinifanya nihamishie maisha yangu Kaburu ili kuweka mambo fulan sawa. Nikiwa Kaburu nimejikuta nafanya kazi na watu tofauti tofauti kutoka nchi na mabara tofauti.

Mwaka 2014 nikiwa nafanya kazi katika restaurant ya Spar (ambayo hata bongo ipo) kuna sister fulan wa kizungu alitokea kuwa rafiki yangu wa karibu (sio kiuhusiano wa mapenzi). Yule mzungu tulizoeana sana kiasi kwamba tukawa tunapeana uzoefu mbali mbali wa kimaisha, mimi nilikuwa najaribu kumchimba ili kujua ni kwanini watu wengi weupe hasa wazungu ni matajiri ukilinganisha na sisi waafrika weusi, pia na yeye alikuwa akijaribu kudodosa inakuaje waafrika wengi (weusi) ni masikini japo kuna baadhi unakuta wametokea katika familia za watu matajiri.

Sasa katika kumchimba chimba ndo siku 1 akanipa code ya mafanikio yao kimaisha, japo code hii kwa ndugu zangu wabongo ni vigumu sana kuizingatia.

Code hiyo aliyonipa ina vipengele vitano navyo ni 👇

1) MAANDALIZI:
Wenzetu huanza maandalizi ya kumuandalia mtoto maisha toka akiwa tumboni. Yani mke na mume wanapogundua kwamba katika nyumba yao kuna kijacho kinatarajia kuja baada ya mke kushika mimba, huanza maandalizi mapema ya kumtengenezea maisha kwa kuanza kuandaa mazingira ya kumfungulia mtoto ajae account yake ya bank. Hapa katika kumfungulia mtoto account ya bank kuna mawili, kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela katika account hiyo kabla mtoto hajazaliwa, na kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela baada tu ya mtoto kuzaliwa.

Na kwa vile wenzetu wamejiandaa mapema ambapo unakuta baba na mama wote wana kazi, basi account hii huanza kuwekewa pesa na wazazi wote wawili kila mwisho wa mwezi. Zoezi hili huendelea mpaka pale mtoto anapofikisha umri wa miaka 18, japo kuna baadhi wenye pesa zao huendelea mpaka pale mtoto atapokuwa na familia yake nk.

Sasa chukulia baba na mama wawe wanaweka elfu hamsini hamsini kwa kila mwezi, ina maana elfu hamsini hamsini kwa watu wawili ni laki moja, laki 1 kwa miezi 12 (mwaka) ni sawa na milioni 1 na laki 2. Hiyo milioni 1 na laki 2 ukiifanya mara 18 inakuwa milioni ishirini na moja na laki 6 (huu ni mfano tu) maana wao huweka zaidi ya hizo.

2) MALEZI:
Wenzetu pamoja na kwamba watoto wana uhuru wa kuamua jambo, lkn linapokuja swala la malezi huwa makini sana ili kuhakikisha mtoto haendi nje ya matarajio yao, na kuacha kufuata utaratibu wao.

Huu ni utaratibu ambao wameshajiwekea vizazi na vizazi, kwahiyo wazazi hufanya kila wawezalo ili kuhakikisha mtoto wao anakuwa kwenye mazingira bora na yenye kueleweka kwa faida yake na familia yake hapo baadae. Ni vigumu kwa mzungu kwenda kulewa na kurudi nyumban kulala bila kujua mtoto ameshinda wapi, na nani, amekula au hakula, anaumwa au haumwi nk.

3) ELIMU:
Wenzetu hulipa kipaumbele sana swala la elimu, tena huwa wanampa mtoto uhuru wa kuchagua kile anachopenda kusomea. Mfano mtoto anaonesha kupenda kuwa pilot wa ndege, basi wazazi wataelekeza nguvu zaidi katika hilo na ikiwezekana watampeleka katika shule ya kusomea mambo ya ndege bado mapema, waswahili tunasema 'samaki mkunje angali m'bichi', so mpaka atakapokuja kukuwa atakuwa ashafika mbali kwa kile anachojifunza.

4) USIMAMIAJI NA SUPPORT:
Mtoto anapokuwa ashakuwa na tayari ana elimu yake fulan, basi wazazi, ndugu, serikali nk vitamsimamia huyu kupata kazi kutokana na kile alichosomea. Supporter yao huwa ni kubwa na hawapumziki hadi wahakikishe lengo lao limetimia. Na alietafutiwa kazi akianza kazi huwa ni kazi kweli kweli, hakuna muda wa kukaa kwenye vikorido vya ofisi kupiga porojo mbali mbali zisizokuwa na msingi wala faida kwake.

Lakini jambo zuri kwake ni kwamba huanza kazi huku akiwa tayari ana account yake toka utotoni. Accont hiyo tayari ina zaidi ya milioni 20, so atachofanya ni kujazia zingine atazoanza kupokea kwenye mshahara wake.

5) MUENDELEZO:
Mtoto huyu au kijana huyu akishafika hapo alipofika, na yeye hufanya muendelezo kwa kizazi chake, ili kuepusha kuwa kuwa na watoto tegemezi katika familia yao/ zao.

ANGALIZO hapo chini 👇

Sasa basi, wazungu nao kama walivyo binadam wengine, na wao wana mapungufu yao. Nikimaanisha kuwa wapo wazungu ambao hawafuati hizi code kama wenzao, au wapo waliojaribu kufuata ila vizazi vyao vika fail katika hilo na kudumbukia katika umasikini, uteja, ulevi nk. Ila majority 85% ya wazungu wanaishi kwa kufuata huu mfumo wa code na unawanufaisha vizuri bila kwenda kwa shehe, mchungaji, mganga wala mtabiri.

Mimi nilipoowa na mke wangu kuzaa mtoto wa kwanza nilianza kuzifuata hizi code, nilipozaa wa pili pia nimeendelea kuzifuata hizi code tena tukishirikiana na mke wangu ambae na yeye anafanya kazi.

Japo ni changamoto kubwa kufanya mambo mengi kwa pamoja, kama vile kulipa kodi ya nyumba kila mwezi, kuwalipia watoto ada za shule kila mwezi, kununua stock ya chakula kila mwezi, kufanya shopping kila mwezi nk.

Lakini nina amini hii ndio njia bora ya kuwataharishia maisha yaliobora hapo baadae, na elimu hii nimekuwa nikiitoa kwa baadhi ya marafiki zangu, so its up to them eidha kufuata au kutofuata.

Najua kwa ndugu zetu wabongo walio wengi hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwao, lkn kama una uwezo na nafasi ya kufanya hivi just do it now, ili uje kuokoa vizazi na vizazi vyako vitakavyokuja baada yako, sio uendekeze ulevi na kamari.

Asanteni sana.
 
Hajakupa fact moja muhimu. Ili hayo yote yafanyike inatakiwa kuwe na mifumo mizuri kuanzia huduma za jamii, Uchumi mzuri wa kitaifa na uongozi thabiti. Si kweli kwamba wazungu wote wanafuata hizo 'code', mostly likely ni kuwa tayari wanakuta mifumo mizuri ya maisha, kwa hiyo wanaifuata kirahisi. Binadamu wanapenda sana kuvunja sheria, lakini ukizaliwa katika Nchi ambayo kukwepa kodi au kuvunja sheria nyingine ni suala la hatari, huwezi kuthubutu kwenda kinyume.

Kwa hayo yoye, ndiyo maana wazungu wa Ulaya mashariki wapo hoi kulinganisha na wale wa Ulaya magharibi.
 
-Tanzania yetu mzazi anakuambia tena shukuru unalalia godoro, sisi tu.ekua tanalalia ngozi na kula mihogo gmya kuchemshwa. Waafrika tuna mentality mbovu aisee kwani mateso na maisha uliyopitia wakati wewe mzazi unakua ni lazima na watoto wayapitie???
 
Hajakupa fact moja muhimu. Ili hayo yote yafanyike inatakiwa kuwe na mifumo mizuri kuanzia huduma za jamii, Uchumi mzuri wa kitaifa na uongozi thabiti. Si kweli kwamba wazungu wote wanafuata hizo 'code', mostly likely ni kuwa tayari wanakuta mifumo mizuri ya maisha, kwa hiyo wanaifuata kirahisi. Binadamu wanapenda sana kuvunja sheria, lakini ukizaliwa katika Nchi ambayo kukwepa kodi au kuvunja sheria nyingine ni suala la hatari, huwezi kuthubutu kwenda kinyume.

Kwa hayo yoye, ndiyo maana wazungu wa Ulaya mashariki wapo hoi kulinganisha na wale wa Ulaya magharibi.
Hizo ni code za mfumo wa maisha kwa upande wa familia kwa familia mkuu. Na sio swala linalohusiana na serikali. Najua kwamba serikali zina mifumo yao, ila kwa hapa nimeleta zile code zinazohusiana na maisha ya kifamilia kwa raia mmoja mmoja.

Yan swala la wazungu wote kutokufuata huu mfumo pia nimeliongelea japo sio wengi ukilinganisha na wale wanaofuata.

Shukran mkuu kwa kutupa mawili matatu ambayo yametuongezea ufahamu fulan katika hili.
 
-Tanzania yetu mzazi anakuambia tena shukuru unalalia godoro, sisi tu.ekua tanalalia ngozi na kula mihogo gmya kuchemshwa. Waafrika tuna mentality mbovu aisee kwani mateso na maisha uliyopitia wakati wewe mzazi unakua ni lazima na watoto wayapitie???
Japo inachekesha, lkn mengi uliyoandika hapa ni ukweli mtupu.
 
Watz wengi wanazaa watoto waje wawasaidie,Yaan ile wakikuzaa tu ni msaada tosha utafikiri waliombwa na hapo wanazaa watoto hata kumi
Waswahili wanakwambia kila mtoto huja na riziki yake. Kwahiyo anajua akizaa watoto 10 atakuwa na riziki ya watoto kumi hata kama watoto hao hajawapa elimu ya kuwasaidia.

Mawazo mufilisi kabisa haya!
 
Tanzania mtoto akizaliwa analia sana maana kaingiwa kweny balaa wazazi Wana mpango wa kuanza kumtegemea miaka kadhaa na lawama kibao yeye kapewe elimu kama wajibu wa wazazi hana hata mia bank eti aanze Maisha.siku kadhaa anaanza kulaumiwa ajenge kwake huku bongo mtu anazaa watoto wengi kipato chake kwa mwezi kinaisha anashindwa kuweka akiba hata ya elfu 50k sembuse kifungulia account wanawe ...Bongo ukizaliwa katika familia maskini Bora zinazojitambua na Wana uwezo ila kwingine balaa tupu.


Wazazi wa Tanzania wanaona sifa kuja kusema Nimekulelea kwa tabu sana😂😂😂yaani mtoto kwa tabu mpaka anafika kujitegemea kanyooka akili imedumaa matatizo mwanzo mwisho kama kutesa viumbe ..bado anazaa watoto kibao
 
Tanzania mtoto akizaliwa analia sana maana kaingiwa kweny balaa wazazi Wana mpango wa kuanza kumtegemea miaka kadhaa na lawama kibao yeye kapewe elimu kama wajibu wa wazazi hana hata mia bank eti aanze Maisha.siku kadhaa anaanza kulaumiwa ajenge kwake huku bongo mtu anazaa watoto wengi kipato chake kwa mwezi kinaisha anashindwa kuweka akiba hata ya elfu 50k sembuse kifungulia account wanawe ...Bongo ukizaliwa katika familia maskini Bora zinazojitambua na Wana uwezo ila kwingine balaa tupu.


Wazazi wa Tanzania wanaona sifa kuja kusema Nimekulelea kwa tabu sana😂😂😂yaani mtoto kwa tabu mpaka anafika kujitegemea kanyooka akili imedumaa matatizo mwanzo mwisho kama kutesa viumbe ..bado anazaa watoto kibao
Wananichekesha pale unapomshauri swala la kuzaa kwa mpangilio afu anakujibu kuwa kila mtoto huja na riziki yake 😂😂😂
 
Wananichekesha pale unapomshauri swala la kuzaa kwa mpangilio afu anakujibu kuwa kila mtoto huja na riziki yake 😂😂😂
We acha tu yaani ukifuatilia kizazi cha sasa watoto wengi ni tabu Kuna machalii wanagonga mpaka miaka 28 wapo kwao na wamesoma ramani hazisomeki ...kwa kweli kwa miaka hii unaweza kupata tabu kulelea watoto mpaka waje kujitegemea ni mda sana na unaweza ukafa pia
 
Waswahili wanakwambia kila mtoto huja na riziki yake. Kwahiyo anajua akizaa watoto 10 atakuwa na riziki ya watoto kumi hata kama watoto hao hajawapa elimu ya kuwasaidia.

Mawazo mufilisi kabisa haya!
Kwa mrengo wako !!

Hizi codes kwa waTz hawa wasio na ajira na masikini wa vijijini. Wanawezaje kuzifuata ikiwa kula yao, shughuli zao etc ni za bahati nasibu ?!
 
Habari zenu wana JF wenzangu,

Kwanza nianze kusema kwamba mimi ni miongoni mwa watanzania waliozaliwa katika familia ya maisha ya kati, sio familia tajiri wala masikini.

Pilika pilika za hapa na pale, zilinifanya nihamishie maisha yangu Kaburu ili kuweka mambo fulan sawa. Nikiwa Kaburu nimejikuta nafanya kazi na watu tofauti tofauti kutoka nchi na mabara tofauti.

Mwaka 2014 nikiwa nafanya kazi katika restaurant ya Spar (ambayo hata bongo ipo) kuna sister fulan wa kizungu alitokea kuwa rafiki yangu wa karibu (sio kiuhusiano wa mapenzi). Yule mzungu tulizoeana sana kiasi kwamba tukawa tunapeana uzoefu mbali mbali wa kimaisha, mimi nilikuwa najaribu kumchimba ili kujua ni kwanini watu wengi weupe hasa wazungu ni matajiri ukilinganisha na sisi waafrika weusi, pia na yeye alikuwa akijaribu kudodosa inakuaje waafrika wengi (weusi) ni masikini japo kuna baadhi unakuta wametokea katika familia za watu matajiri.

Sasa katika kumchimba chimba ndo siku 1 akanipa code ya mafanikio yao kimaisha, japo code hii kwa ndugu zangu wabongo ni vigumu sana kuizingatia.

Code hiyo aliyonipa ina vipengele vitano navyo ni 👇

1) MAANDALIZI:
Wenzetu huanza maandalizi ya kumuandalia mtoto maisha toka akiwa tumboni. Yani mke na mume wanapogundua kwamba katika nyumba yao kuna kijacho kinatarajia kuja baada ya mke kushika mimba, huanza maandalizi mapema ya kumtengenezea maisha kwa kuanza kuandaa mazingira ya kumfungulia mtoto ajae account yake ya bank. Hapa katika kumfungulia mtoto account ya bank kuna mawili, kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela katika account hiyo kabla mtoto hajazaliwa, na kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela baada tu ya mtoto kuzaliwa.

Na kwa vile wenzetu wamejiandaa mapema ambapo unakuta baba na mama wote wana kazi, basi account hii huanza kuwekewa pesa na wazazi wote wawili kila mwisho wa mwezi. Zoezi hili huendelea mpaka pale mtoto anapofikisha umri wa miaka 18, japo kuna baadhi wenye pesa zao huendelea mpaka pale mtoto atapokuwa na familia yake nk.

Sasa chukulia baba na mama wawe wanaweka elfu hamsini hamsini kwa kila mwezi, ina maana elfu hamsini hamsini kwa watu wawili ni laki moja, laki 1 kwa miezi 12 (mwaka) ni sawa na milioni 1 na laki 2. Hiyo milioni 1 na laki 2 ukiifanya mara 18 inakuwa milioni ishirini na moja na laki 6 (huu ni mfano tu) maana wao huweka zaidi ya hizo.

2) MALEZI:
Wenzetu pamoja na kwamba watoto wana uhuru wa kuamua jambo, lkn linapokuja swala la malezi huwa makini sana ili kuhakikisha mtoto haendi nje ya matarajio yao, na kuacha kufuata utaratibu wao.

Huu ni utaratibu ambao wameshajiwekea vizazi na vizazi, kwahiyo wazazi hufanya kila wawezalo ili kuhakikisha mtoto wao anakuwa kwenye mazingira bora na yenye kueleweka kwa faida yake na familia yake hapo baadae. Ni vigumu kwa mzungu kwenda kulewa na kurudi nyumban kulala bila kujua mtoto ameshinda wapi, na nani, amekula au hakula, anaumwa au haumwi nk.

3) ELIMU:
Wenzetu hulipa kipaumbele sana swala la elimu, tena huwa wanampa mtoto uhuru wa kuchagua kile anachopenda kusomea. Mfano mtoto anaonesha kupenda kuwa pilot wa ndege, basi wazazi wataelekeza nguvu zaidi katika hilo na ikiwezekana watampeleka katika shule ya kusomea mambo ya ndege bado mapema, waswahili tunasema 'samaki mkunje angali m'bichi', so mpaka atakapokuja kukuwa atakuwa ashafika mbali kwa kile anachojifunza.

4) USIMAMIAJI NA SUPPORT:
Mtoto anapokuwa ashakuwa na tayari ana elimu yake fulan, basi wazazi, ndugu, serikali nk vitamsimamia huyu kupata kazi kutokana na kile alichosomea. Supporter yao huwa ni kubwa na hawapumziki hadi wahakikishe lengo lao limetimia. Na alietafutiwa kazi akianza kazi huwa ni kazi kweli kweli, hakuna muda wa kukaa kwenye vikorido vya ofisi kupiga porojo mbali mbali zisizokuwa na msingi wala faida kwake.

Lakini jambo zuri kwake ni kwamba huanza kazi huku akiwa tayari ana account yake toka utotoni. Accont hiyo tayari ina zaidi ya milioni 20, so atachofanya ni kujazia zingine atazoanza kupokea kwenye mshahara wake.

5) MUENDELEZO:
Mtoto huyu au kijana huyu akishafika hapo alipofika, na yeye hufanya muendelezo kwa kizazi chake, ili kuepusha kuwa kuwa na watoto tegemezi katika familia yao/ zao.

ANGALIZO hapo chini 👇

Sasa basi, wazungu nao kama walivyo binadam wengine, na wao wana mapungufu yao. Nikimaanisha kuwa wapo wazungu ambao hawafuati hizi code kama wenzao, au wapo waliojaribu kufuata ila vizazi vyao vika fail katika hilo na kudumbukia katika umasikini, uteja, ulevi nk. Ila majority 85% ya wazungu wanaishi kwa kufuata huu mfumo wa code na unawanufaisha vizuri bila kwenda kwa shehe, mchungaji, mganga wala mtabiri.

Mimi nilipoowa na mke wangu kuzaa mtoto wa kwanza nilianza kuzifuata hizi code, nilipozaa wa pili pia nimeendelea kuzifuata hizi code tena tukishirikiana na mke wangu ambae na yeye anafanya kazi.

Japo ni changamoto kubwa kufanya mambo mengi kwa pamoja, kama vile kulipa kodi ya nyumba kila mwezi, kuwalipia watoto ada za shule kila mwezi, kununua stock ya chakula kila mwezi, kufanya shopping kila mwezi nk.

Lakini nina amini hii ndio njia bora ya kuwataharishia maisha yaliobora hapo baadae, na elimu hii nimekuwa nikiitoa kwa baadhi ya marafiki zangu, so its up to them eidha kufuata au kutofuata.

Najua kwa ndugu zetu wabongo walio wengi hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwao, lkn kama una uwezo na nafasi ya kufanya hivi just do it now, ili uje kuokoa vizazi na vizazi vyako vitakavyokuja baada yako, sio uendekeze ulevi na kamari.

Asanteni sana.
Watanzania 88% wanachojua ni kufanya mapenzi sana na kuzaa watoto wengi bila mipango na wakiona wamewashindwa kinachofuata ni kuwatelekeza au kuwanyanyasa kwa kutowapatia huduma muhimu kwa kisingizio cha maisha magumu na kuilaumu serikali haya uliyoaandika watasoma na kusonya tu ila hawatakuelewa...
 
We acha tu yaani ukifuatilia kizazi cha sasa watoto wengi ni tabu Kuna machalii wanagonga mpaka miaka 28 wapo kwao na wamesoma ramani hazisomeki ...kwa kweli kwa miaka hii unaweza kupata tabu kulelea watoto mpaka waje kujitegemea ni mda sana na unaweza ukafa pia
Yah ni kweli mkuu, hii ni kwa sababu wazazi wengi hawakuwaandalia watoto wao future ya maisha yao.

Kuna wale ambao walikuwa hawajiwezi, hawa inafahamika. Lakini kuna wale ambao walikuwa na uwezo wa kuwalea vizuri na kuwapa elimu nzuri watoto wao, ila walichofanya ni kujenga heshima baa, kubadilisha madem na wengine kuzaa bila mpangilio mzuri.
 
Mimi nipo tofauti kidogo. Mimi siamini katika kuweka akiba ya fedha benki, bali nina amini katika kuwekeza fedha kwenye miradi. Hii faida yake ni kwamba faida inaonekana ila kuweka fedha benki, shilingi inashuka sana thamani.

Babilonian Law of wealth inasema save to invest; don't save to save
 
Hakuna nchi iliyoweza kukontro namba ya watu ikashindwa kuwafanya waishi vizur kijamii au kuongeza uchumi wao. Keep it! Nchi nyingi za KIAFRIKA ya Sahara zimeshindwa hapo tu. Zina idadi ya watu wengi kufananisha na fursa zilizopo. Wazaz wamekomaa kudhan8 watoto wakikua watawasaidia.
Mfumo huu tutauweza na jitihada za kuwafikisha watu wanapokwenda zitfanikiwa kias iwapo kampeni y kupanga watoto itawezekana. Tunza hii hoja
 
Watz wengi wanazaa watoto waje wawasaidie,Yaan ile wakikuzaa tu ni msaada tosha utafikiri waliombwa na hapo wanazaa watoto hata kumi
Such a very negative critisism that u have done though it is true..u have failed to realize that some life orientation for africans are so closedly attached to our culture especially in kids raising so in turn they r really not mistakes
 
Yah ni kweli mkuu, hii ni kwa sababu wazazi wengi hawakuwaandalia watoto wao future ya maisha yao.

Kuna wale ambao walikuwa hawajiwezi, hawa inafahamika. Lakini kuna wale ambao walikuwa na uwezo wa kuwalea vizuri na kuwapa elimu nzuri watoto wao, ila walichofanya ni kujenga heshima baa, kubadilisha madem na wengine kuzaa bila mpangilio mzuri.
Father wangu mdogo ana watoto wanne pesa anayo ana maduka kama matano nyumba kubwa tatu ,FUSO ziko mbili yule mwanae wa kwanza akiwa early 20's alimshamkabidhi Fuso moja na yeye sio mkubwa sema ni wakiume wa kwanza maana ana wa kiume wawili na wanawake wawili..mtoto wake wa kwanza aliolewa na jamaa ambaye nae ana uwezo kidogo wa pili ndo huyo kamkabidhi Fuso mpaka anafika miaka 24 tayar Fuso ishamlipa akaoa ,mwanae anafuata baada ya huyo pia ni wakiume nae kakabidhiwa Duka la jumla sema yeye alisoma hapo IFm sasa ivi duka lishakuwa mbali nae kashaoa.. wa mwisho ni wa kike ndo yupo nae home ila washakuja jamaa kadhaa kutaka kumuoa .

Mzee hana shida wala wanae hawana shida njia ishawanyookea kitambo hawanaga stress ,kingine ni mtu wa dini ila aliktaa kabisa kuoa mke mwingine alisema inaweza kuleta ugomvi
 
Such a very negative critisism that u have done though it is true..u have failed to realize that some life orientation for africans are so closedly attached to our culture especially in kids raising so in turn they r really not mistakes
Those cultural ideas in some ways are too mythical stances. Why the proffesionals we have failing to influence change to African minds!?.
 
Back
Top Bottom