Code alizonipa mzungu zimenisaidia kuona mwanga wa mafanikio yangu na familia yangu hapo baadaye

Code alizonipa mzungu zimenisaidia kuona mwanga wa mafanikio yangu na familia yangu hapo baadaye

Tusizunguke sana.Serikali zinazojitambua na kutumia kodi za wananchi vizuri ndio chanzo cha maisha mazuri.
Serikalia inaanzia na wewe nyumban kwako.
Naomba nikupe mfano hai hapo chini 👇
Mimi nilikuwa na mjomba wangu ambae alikuwa anafanya kazi serikalini miaka ya 90, alikuwa na cheo kikubwa kwahiyo na mshahara wake ulikuwa mkubwa ukilinganisha na wenzake wa chini yake.

Mjomba huyu wakati baada ya wenzake aliowazidi mshahara walikuwa wanajitahidi kuwasomesha watoto wao na kuwaandalia misingi bora ya maisha, yeye alikuwa anajenga heshima baa. Hakuna baada ambayo walikuwa hawamjui kuanzia magomeni, kinondoni, ilala nk. madem ndio usiseme, mke alipigana mwisho akaamua kutulia alee wanae.

Alibahatika kuzaa watoto watatu, wa kiume wawili na wa kike mmoja. Wote hakuwapa elimu inayostahili. Alikuwa akitoka asubuhi kwenda kazini anarudi saa 7 au 8 ya usiku akiwa bwii, hajui kama kuna mtoto alienda shule au hakwenda, alijisomea au hakujisomea, anaumwa au haumwi nk.

Sasa hivi kazi imesha, hana nyumba, hana kiwanja, hana chochote kama kumbu kumbu kwa kazi aliyofanya ujanani. Watoto wa kiume wamekosa muongozo wa elimu sasa mkubwa ni teja, mdogo anapiga debe. Bint kaolewa na muuza mitumba fulan ambae ndio hujitahidi kuhudumia na familia ya baba wa mke.

Je hapo tuilaumu serikali? Watoto? Baba (mjomba)? Au nani?
 
Mimi nipo tofauti kidogo. Mimi siamini katika kuweka akiba ya fedha benki, bali nina amini katika kuwekeza fedha kwenye miradi. Hii faida yake ni kwamba faida inaonekana ila kuweka fedha benki, shilingi inashuka sana thamani.

Babilonian Law of wealth inasema save to invest; don't save to save
Nilikusudia kusema hivyo pia, na ubora wa njia hiyo ni kwamba kama ulifungua biashara ndogo kwa akili ya future ya mwanao utakuwa na mida wa kutosha kuisoma, kuelewa wewe binafsi, kuyajua na kuua shughulikia mapungufu ya biashara hiyo kisha unarudi kum shape mtoto wako ili aendane na mahitaji ya kiusimamizi ya biashara hiyo, Huko mbeleni yeye mwenyewe anaweza kuja kubadili mode ya biashara hiyo lakini akiwa tayari anaelewa basic and what does it meant for, atakuwa na Road map ya kumpeleka anakotakiwa kwenda, mfano wa Mr dudumizi wa kuweka angalao 100,000 kwa mwezi kwenye pig account ya mtoto imenyooka sana, imagine, kwa hesabu zake mwenyewe anaonyesha kuwa kwa miaka 18 ya uwekezaji huo mtoto atakuwa na around 21,000,000 sawa, si kiasi kidogo hata chembe, ila hela hiyo hiyo inatosha kabisa kumwaribu mwanao hadi ujutie good faith saving yako ya 18 years, na kwa age hiyo mtoto kupoteza mwelekeo ni jambo la sekunde tu kama hukumnyoosha vya kutosha.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwa mrengo wako !!

Hizi codes kwa waTz hawa wasio na ajira na masikini wa vijijini. Wanawezaje kuzifuata ikiwa kula yao, shughuli zao etc ni za bahati nasibu ?!
Mkuu nimeshauri kwa wale wenye uwezo wa kufanya hivyo.

Maana kuna mtu ana mshahara au uwezo wa kuiandalia familia yake kesho iliyokuwa bora, lkn unakuta mtu huyo anautumia mshahara huo katika mambo ya kijinga kama vile ulevi wa kutupa, kamari, vimada nk.
 
Watanzania 88% wanachojua ni kufanya mapenzi sana na kuzaa watoto wengi bila mipango na wakiona wamewashindwa kinachofuata ni kuwatelekeza au kuwanyanyasa kwa kutowapatia huduma muhimu kwa kisingizio cha maisha magumu na kuilaumu serikali haya uliyoaandika watasoma na kusonya tu ila hawatakuelewa...
😂😂😂😂 kweli mkuu, baadhi yao nimeshawaona kupitia comment zao.
 
Serikalia inaanzia na wewe nyumban kwako.
Naomba nikupe mfano hai hapo chini 👇
Mimi nilikuwa na mjomba wangu ambae alikuwa anafanya kazi serikalini miaka ya 90, alikuwa na cheo kikubwa kwahiyo na mshahara wake ulikuwa mkubwa ukilinganisha na wenzake wa chini yake.

Mjomba huyu wakati baada ya wenzake aliowazidi mshahara walikuwa wanajitahidi kuwasomesha watoto wao na kuwaandalia misingi bora ya maisha, yeye alikuwa anajenga heshima baa. Hakuna baada ambayo walikuwa hawamjui kuanzia magomeni, kinondoni, ilala nk. madem ndio usiseme, mke alipigana mwisho akaamua kutulia alee wanae.

Alibahatika kuzaa watoto watatu, wa kiume wawili na wa kike mmoja. Wote hakuwapa elimu inayostahili. Alikuwa akitoka asubuhi kwenda kazini anarudi saa 7 au 8 ya usiku akiwa bwii, hajui kama kuna mtoto alienda shule au hakwenda, alijisomea au hakujisomea, anaumwa au haumwi nk.

Sasa hivi kazi imesha, hana nyumba, hana kiwanja, hana chochote kama kumbu kumbu kwa kazi aliyofanya ujanani. Watoto wa kiume wamekosa muongozo wa elimu sasa mkubwa ni teja, mdogo anapiga debe. Bint kaolewa na muuza mitumba fulan ambae ndio hujitahidi kuhudumia na familia ya baba wa mke.

Je hapo tuilaumu serikali? Watoto? Baba (mjomba)? Au nani?
Very painful kaka.
Hii ya kulaum serikali ni excuse tunatumia wengi ila it really doesnt resolve anything.
You are the one responsible for your own life and those under your care.

Japo serikal ingetimiza wajibu wake ingekua bora zaid
 
Mimi nipo tofauti kidogo. Mimi siamini katika kuweka akiba ya fedha benki, bali nina amini katika kuwekeza fedha kwenye miradi. Hii faida yake ni kwamba faida inaonekana ila kuweka fedha benki, shilingi inashuka sana thamani.

Babilonian Law of wealth inasema save to invest; don't save to save
Ya ni kweli mkuu, ila sometimes miradi nayo hufilisika na kukuacha mtupu.

Kufanya biashara kunahitaji moyo na uzoefu, sio kukurupuka tu.

Btw: fanya kile ambacho moyo wako unakushauri mkuu, kikubwa kiwe na njia nzuri kwa vizazi vyako vijavyo.
 
Watanzania 88% wanachojua ni kufanya mapenzi sana na kuzaa watoto wengi bila mipango na wakiona wamewashindwa kinachofuata ni kuwatelekeza au kuwanyanyasa kwa kutowapatia huduma muhimu kwa kisingizio cha maisha magumu na kuilaumu serikali haya uliyoaandika watasoma na kusonya tu ila hawatakuelewa...
Kuzaa watoto wengi au wachache sio kipimo cha uduni wala ubora wa mtu.wala sio kipimo cha umasikini as long as unaweza kumudu mahitaji yao
 
-Tanzania yetu mzazi anakuambia tena shukuru unalalia godoro, sisi tu.ekua tanalalia ngozi na kula mihogo gmya kuchemshwa. Waafrika tuna mentality mbovu aisee kwani mateso na maisha uliyopitia wakati wewe mzazi unakua ni lazima na watoto wayapitie???
Usilaumu sana wazazi,inawezekana walichokupa,ndio walichokuwa nacho,
Maisha ya kibongo ni magumu sana,baba Mwalimu,mama polisi,mshahara haufiki 700K,unafikiri wataweza kukuandalia hayo yote?
Cha muhimu,ukifanikiwa kutoboa,for hook or crook,legal or illegal,weka bima ya maisha,wekeza kwa ajiri ya uzao wako,wapo wazazi wanafanya hii,unaoa,au kuolewa,Mzazi anakukabidhi nyumba hata kama haijaisha,uishi,au umalizie uishi,ufsnyie biashara maisha yaende,
Huku kwetu tuna Siasa za hovyo,mifuko ya hifadhi ya jamii,na bima ya afya ilibidi iwe kimbilio la maskini na wananchi,lakini serikali hii ya kijambazi imefilisi mifuko yote
 
Mkuu haya mambo ndio unaita code? Kweli mkuu kujua haya ndo ulisubiri kuambiwa na mzungu?

Mbona ni obvious kabisa haya
Kuyajua haya sio tatizo, tatizo ni aina ya upangiliaji wake ndio tunaita code.
 
Wananichekesha pale unapomshauri swala la kuzaa kwa mpangilio afu anakujibu kuwa kila mtoto huja na riziki yake 😂😂😂
Muhusika : Wewe kwenu wa ngapi

Mimi : wa 4

Muhusika : wazazi wako wangeamua kuzaa watoto watatu, wewe ungezaliwa

Mimi : Hapana lakini zama zimebadilika, mahitaji ya kulea mtoto kipindi nazaliwa na sasa ni tofauti

Muhusika : hujayajua maisha wewe, unadhani wazazi wako wangefikiria gharama wangekuzaa au unadhani enzi hizo hazikuwepo. Kwanza acha uoga wa maisha, wewe zaa tu maana hakuna mtoto atakaekufa kwa njaa akishazaliwa au asikue.
Mimi hapa nazaa hadi wote waliopo kiunoni waishe maana kila mmoja Mungu humpa ridhki yake na kwanza naweza kuzaa watoto watatu na wote wakanisahau ila yule wa tano ambaye sijamzaa ndio fungu langu

Mimi : 😷😷😷
 
Very painful kaka.
Hii ya kulaum serikali ni excuse tunatumia wengi ila it really doesnt resolve anything.
You are the one responsible for your own life and those under your care.

Japo serikal ingetimiza wajibu wake ingekua bora zaid
We can't change our government system, before we change ourselves.

Government itasimama kwa upande wa taifa, na sisi tutasimama kwa upande wa familia.
 
Kwa tz iyo code haitawezekana ata kwa mikwaju kutokan na mfumo mbovuvwa kuzaa bila ya mpangilio wenzetu wanzaa kwa mpango ndio maana izo code kwao inakua ni rahic kutekelezeka
 
Sijui Kama nnayo ongea wengine wamegusa lakin huyu Mzungu kakuficha pia baadhi ya mambo ..badala ya kuchangia account why msiweke Bima?Bima za maisha ,za elimu n.k?...kingine wazungu wanajali Sana quality ya elimu ...kumsomesha mtoto sio kumpeleka Kayumba...
 
Waswahili wanakwambia kila mtoto huja na riziki yake. Kwahiyo anajua akizaa watoto 10 atakuwa na riziki ya watoto kumi hata kama watoto hao hajawapa elimu ya kuwasaidia.

Mawazo mufilisi kabisa haya!

Idea mbaya sana mkuu imejaa kichwani mwa watz wengi hii inachangia jamii kuendelea kuwa na tegemezi wengi na lindi la umaskini
 
Habari zenu wana JF wenzangu,

Kwanza nianze kusema kwamba mimi ni miongoni mwa watanzania waliozaliwa katika familia ya maisha ya kati, sio familia tajiri wala masikini.

Pilika pilika za hapa na pale, zilinifanya nihamishie maisha yangu Kaburu ili kuweka mambo fulan sawa. Nikiwa Kaburu nimejikuta nafanya kazi na watu tofauti tofauti kutoka nchi na mabara tofauti.

Mwaka 2014 nikiwa nafanya kazi katika restaurant ya Spar (ambayo hata bongo ipo) kuna sister fulan wa kizungu alitokea kuwa rafiki yangu wa karibu (sio kiuhusiano wa mapenzi). Yule mzungu tulizoeana sana kiasi kwamba tukawa tunapeana uzoefu mbali mbali wa kimaisha, mimi nilikuwa najaribu kumchimba ili kujua ni kwanini watu wengi weupe hasa wazungu ni matajiri ukilinganisha na sisi waafrika weusi, pia na yeye alikuwa akijaribu kudodosa inakuaje waafrika wengi (weusi) ni masikini japo kuna baadhi unakuta wametokea katika familia za watu matajiri.

Sasa katika kumchimba chimba ndo siku 1 akanipa code ya mafanikio yao kimaisha, japo code hii kwa ndugu zangu wabongo ni vigumu sana kuizingatia.

Code hiyo aliyonipa ina vipengele vitano navyo ni 👇

1) MAANDALIZI:
Wenzetu huanza maandalizi ya kumuandalia mtoto maisha toka akiwa tumboni. Yani mke na mume wanapogundua kwamba katika nyumba yao kuna kijacho kinatarajia kuja baada ya mke kushika mimba, huanza maandalizi mapema ya kumtengenezea maisha kwa kuanza kuandaa mazingira ya kumfungulia mtoto ajae account yake ya bank. Hapa katika kumfungulia mtoto account ya bank kuna mawili, kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela katika account hiyo kabla mtoto hajazaliwa, na kuna wale ambao hufungua na kuanza kuweka hela baada tu ya mtoto kuzaliwa.

Na kwa vile wenzetu wamejiandaa mapema ambapo unakuta baba na mama wote wana kazi, basi account hii huanza kuwekewa pesa na wazazi wote wawili kila mwisho wa mwezi. Zoezi hili huendelea mpaka pale mtoto anapofikisha umri wa miaka 18, japo kuna baadhi wenye pesa zao huendelea mpaka pale mtoto atapokuwa na familia yake nk.

Sasa chukulia baba na mama wawe wanaweka elfu hamsini hamsini kwa kila mwezi, ina maana elfu hamsini hamsini kwa watu wawili ni laki moja, laki 1 kwa miezi 12 (mwaka) ni sawa na milioni 1 na laki 2. Hiyo milioni 1 na laki 2 ukiifanya mara 18 inakuwa milioni ishirini na moja na laki 6 (huu ni mfano tu) maana wao huweka zaidi ya hizo.

2) MALEZI:
Wenzetu pamoja na kwamba watoto wana uhuru wa kuamua jambo, lkn linapokuja swala la malezi huwa makini sana ili kuhakikisha mtoto haendi nje ya matarajio yao, na kuacha kufuata utaratibu wao.

Huu ni utaratibu ambao wameshajiwekea vizazi na vizazi, kwahiyo wazazi hufanya kila wawezalo ili kuhakikisha mtoto wao anakuwa kwenye mazingira bora na yenye kueleweka kwa faida yake na familia yake hapo baadae. Ni vigumu kwa mzungu kwenda kulewa na kurudi nyumban kulala bila kujua mtoto ameshinda wapi, na nani, amekula au hakula, anaumwa au haumwi nk.

3) ELIMU:
Wenzetu hulipa kipaumbele sana swala la elimu, tena huwa wanampa mtoto uhuru wa kuchagua kile anachopenda kusomea. Mfano mtoto anaonesha kupenda kuwa pilot wa ndege, basi wazazi wataelekeza nguvu zaidi katika hilo na ikiwezekana watampeleka katika shule ya kusomea mambo ya ndege bado mapema, waswahili tunasema 'samaki mkunje angali m'bichi', so mpaka atakapokuja kukuwa atakuwa ashafika mbali kwa kile anachojifunza.

4) USIMAMIAJI NA SUPPORT:
Mtoto anapokuwa ashakuwa na tayari ana elimu yake fulan, basi wazazi, ndugu, serikali nk vitamsimamia huyu kupata kazi kutokana na kile alichosomea. Supporter yao huwa ni kubwa na hawapumziki hadi wahakikishe lengo lao limetimia. Na alietafutiwa kazi akianza kazi huwa ni kazi kweli kweli, hakuna muda wa kukaa kwenye vikorido vya ofisi kupiga porojo mbali mbali zisizokuwa na msingi wala faida kwake.

Lakini jambo zuri kwake ni kwamba huanza kazi huku akiwa tayari ana account yake toka utotoni. Accont hiyo tayari ina zaidi ya milioni 20, so atachofanya ni kujazia zingine atazoanza kupokea kwenye mshahara wake.

5) MUENDELEZO:
Mtoto huyu au kijana huyu akishafika hapo alipofika, na yeye hufanya muendelezo kwa kizazi chake, ili kuepusha kuwa kuwa na watoto tegemezi katika familia yao/ zao.

ANGALIZO hapo chini 👇

Sasa basi, wazungu nao kama walivyo binadam wengine, na wao wana mapungufu yao. Nikimaanisha kuwa wapo wazungu ambao hawafuati hizi code kama wenzao, au wapo waliojaribu kufuata ila vizazi vyao vika fail katika hilo na kudumbukia katika umasikini, uteja, ulevi nk. Ila majority 85% ya wazungu wanaishi kwa kufuata huu mfumo wa code na unawanufaisha vizuri bila kwenda kwa shehe, mchungaji, mganga wala mtabiri.

Mimi nilipoowa na mke wangu kuzaa mtoto wa kwanza nilianza kuzifuata hizi code, nilipozaa wa pili pia nimeendelea kuzifuata hizi code tena tukishirikiana na mke wangu ambae na yeye anafanya kazi.

Japo ni changamoto kubwa kufanya mambo mengi kwa pamoja, kama vile kulipa kodi ya nyumba kila mwezi, kuwalipia watoto ada za shule kila mwezi, kununua stock ya chakula kila mwezi, kufanya shopping kila mwezi nk.

Lakini nina amini hii ndio njia bora ya kuwataharishia maisha yaliobora hapo baadae, na elimu hii nimekuwa nikiitoa kwa baadhi ya marafiki zangu, so its up to them eidha kufuata au kutofuata.

Najua kwa ndugu zetu wabongo walio wengi hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwao, lkn kama una uwezo na nafasi ya kufanya hivi just do it now, ili uje kuokoa vizazi na vizazi vyako vitakavyokuja baada yako, sio uendekeze ulevi na kamari.

Asanteni sana.
Hongera sana kwa kupata code za kulea watoto
Ila ukumbuke pia yafuatayo ambayo hajakuambia;
1. Mtoto wa Kizungu mzazi wake hawezi kumchapa na ukimchapa anakuitia Police (Anapiga 911)
2. ,Mtoto akifikisha miaka 18 anarusiwa kuwa na Girl friend/boy friend, kuvuta sigara na hata kunywa pombe
3. Mtoto wa kizungu ana andaliwa kujitegemea yeye na mke/mume wake pekee hakuna mambo ya extended family; na maanisha Mzazi akizeeeka anapelekwa nyumba ya wazee, na hakuna ndugu sijui mjomba nk kusumbua kuomba chochote nk
4. mtoto akishafikisha miaka 18 huna madaraka naye tena zaidi ya kumlipia ada huku akijivinjari na boy/girl friend wake nyumbani kwako

Ninachomaanisha ni kuwa
1. wanamambo mazuri hasa utaratibu wa Elimu yao wa kutambua Vipaji na kuviendeleza
Na kusomesha masomo machache ili mtu ayaelewe vizuri sio huku kwetu katoto ka darasa la nne kamebeba bagi zima la vitabu na madaftari
2. Utaratibu wa kumfungulia account mtoto pia ni mzuri kwani wakati anafika Sekondari walau una ada ya kumsomesha nk
3. Elimu yao humjengea mtoto Kujiamini na sio nidhamu ya woga kama Elimu ya huku kwetu, ambapo unaweza kukuta Mtu ana elimu ya juu kabisa ila anashindwa kusimamia ukweli kwa sabau ya woga

ILA kwa upande wa malezi KWA UJUMLA kuna namna wana BORONGA hivyo usi copy paste!!
 
Back
Top Bottom