Tetesi: Congo DRC na Burundi wanadaiwa wapo mbioni kuivamia Rwanda

Mimi naomba yasitokee maana Jeshi la Rwanda kwa gadhabu na hasira zitarusha mabomu hadi Tanzania na Uganda.
Kuichokoza Tanzania kwenye upande huo ni sawa na kucheza na moto au nyoka aina ya Koboko ndani ya chumba chako.

Tuombe yasitokee kwakuwa tunapenda kuwaona wakibaki kwenye nchi yao waishi maisha yao.
 
Hiyo ilikuwa ahadi ya Tshikedi wakati wa kampeni kuwa akishinda atawamaliza M23!
Hivyo huo sio uvumi ; it’s just a matter of time.
Congo ni wazembe hawako serious na usalama wa nchi yao.
 
Majasusi wake wanalala mitaa ya Mzizima wanafanya wanachotaka(operation) wanaondoka unnoticed, unasemaje?

Tushukuru Mungu Tanzania hatuna changamoto za Kiusalama mambo yangekushangaza.
Ni prediction zako hakuna kitu kama hicho.Majasusi wapo si wa Rwanda hata Nchi marafiki na sisi hivyo hivyo wapo Majasusi wa Tanzania Rwanda na sio Rwanda tu kwenye inchi nyingine zinazohatarisha maslahi yetu, Kwa hiyo sio kitu cha ajabu.Majasusi wa Urusi wapo Marekani na wa Marekani wako Urusi ni vitu vya kawaida Sana katika ulimwengu wa Ujasusi.Kama alivyo mwenyewe PK Kuwa jasusi wa Nchi za Magharibi East and Central Africa ni mambo ya kawaida achaneni na story za vijiweni.
 
Hii ni Trend so inakuja Africa after UKRAINE THEN PALESTINA AND NOW AFRICA then watarudi tena Ulaya au wataenda ASIA .... so mdogo mdogo kunachafuka kila kona... Ili Mambo Yao YATIMIE. kuhusu Uchumi.... Hao Hao wanatakaowapa PESA NA SILAHA Burundi /Congo ndio watakaowaoa PESA na SILAHA RWANDA
 
Majasusi wake wanalala mitaa ya Mzizima wanafanya wanachotaka(operation) wanaondoka unnoticed, unasemaje?

Tushukuru Mungu Tanzania hatuna changamoto za Kiusalama mambo yangekushangaza.
Hadithi za kwenye vijiwe vya kahawa hizi mkuu. Kama ni 'unnoticed' wewe umezipata wapi hizo habari?
Na majasusi wa nchi moja kuwepo nchi nyingine ni kitu cha kawaida sana!

Halafu sentensi yako ya kwanza na ya pili zinakinzana.
 
Mnawapa kichwa Santa hao wanyarwanda,lakini PK mwenyewe anaujua ukweli Kuna Mahali Africa Mashariki huwezi kosea kuwachokoza, PK Hawezi jaribu kukosea hata kurusha jiwe Tz.
Ila ni kama sisi pia tumeparanganyika sana kiasi kwamba mtu akijipanga anaweza akatupiga vibaya hovyo maana kwa sasa ni kama tuko busy na kula keki ya taifa tu hatujui pia tuna maadui wa nje ila adui yetu mkubwa tunamuona ni vyama vya upinzani tu na wakosoaji wa serikali ya ccm.

Nadhani PK alituondolea Mtikila kilaini sana kwahiyo hatuwezi kumbeza moja kwa moja
 
Hao DRC na Burundi hawajashauriwa vizuri, wanatakiwa waunde kikundi Cha uasi kinachipigana na Rwanda, wakipe nguvu, Ila sio majeshi ya serikali kabisa, wao wajifanye hawahusiki,

Kwa hio waivamie Rwanda kwa vikosi vyote angani na aridhini lakini wakiwa wamevaa nguo za waasi.
 
Rwanda ni Kama ina laana, watusi wametawala miaka 30 baada ya kuwaondoa wahutu. Mwaka huu 2024 kuna dalili ya wahutu kurudi tena
Hahahaha, wale watoto washakua wakubwa muda wao wa kurudi nyumbani umefika
 
Kagame ni tatizo katika ukanda wote huu wa Maziwa Makuu. Akikaa pembeni amanin itatamalaki!
 
Majasusi wake wanalala mitaa ya Mzizima wanafanya wanachotaka(operation) wanaondoka unnoticed, unasemaje?

Tushukuru Mungu Tanzania hatuna changamoto za Kiusalama mambo yangekushangaza.
Mkikaa kwenye pool table mnajidanganyaga Sana. Huyu PK sio kwamba mjanja Ila watu wake ndio wasariti na hawana shukrani, na kiburi hicho aliwaponza miaka ya 2013-2014, tukamwanzishia operation kimbunga, haikulenga chochote zaidi ya wanyarwanda. Mengine tuachie sisi. Pk several times tumemkalisha sirini sio mpaka uambiwe. Mungu ibariki Tz na Vyombo vyake vya Ulinzi na Usalama na Amiri Jeshi wake Mkuu.
 
Rwanda iondolewe EAC, kwanza Kagame ameshaacha kuhudhuria vikao vya marais.
Hajiamini, alimwambia JK atampiga asipotarajia na panapouma, Jk akatuma vijana jamaa kalala kamwagiwa maji anaamka anakuta chumba yake imejaa vijana wa Mwamnyange na Othman. Kapigwe biti kuwa acha utoto fala wewe tutakuja kukupasua afu hao wakasepa , toka hapo hakuwahi Leta dharau kwa Mama Tanzania[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Mkuu Kwa nje ndivyo ilivyo lakini ni tofauti na Hali ilivyo huko ndani.Misheni ya Mtikila kitengo ilijua.Nakubaliana na wewe Kuwa hatuwezi kumbeza PK.Pk ana maadui wengi Kwa sasa nafikiri kuliko Marais wote wa Africa ni Lazima hawe makini hivyo alivyo 24hrs sawa na sisi tulivyokuwa wakati wa Baba wa Taifa na sera za ujamaa.NB:Wanaoshughulika na Wapinzani Kuna desk lake lakini vitengo vingi.Usiwe na wasiwasi Tuko vizuri.
 
Kama israel na marekani na ulaya magharibi wote wameshindwa pale gaza eneo sawa na kisiwa cha ukerewe. Wataweza hao warundi na wakongo kuivamia nchi yenye ukubwa wa mikoa mitatu ya tanzania? Kwa uchumi gani walionao sasa
Mangi, Tabora ni 76,151 sq km. Rwanda ni 26,338 sq km... Get your facts right
 
Ameen ameen ameen.

Kumbe tuwaaimini aisee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…