#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

Status
Not open for further replies.
Miongoni mwa familia hii kubwa ya virus iitwayo "Coronaviridae" ni aina saba tu za "coronavirus" zimebainika kusababisha madhara ya kiafya kwa binadamu.

Aina nne za coronavirus zimebainika kusababisha madhara ya wastani yananayofanana na mafua lakini aina tatu zinaonekana kusababisha madhara makubwa kwenye mfumo wa upumuaji na kinga wa binadamu "Severe and acute respiratory syndrome SARS Cov,The Middle east respiratory syndrome(MERS Cov), na sasa SARS Cov-2 ambayo ndiyo aina ya virusi vinavyosababisha ugonjwa uitwao kitaalamu COVID-19.

SARS Cov-2 ni binadamu wa Coronavirus wanaosababisa madhara katika upumuaji na kinga (SARS) virusi hivi vimeangaliwa na kuonekana kufanana jini zao kwa asilimia 79.Ingawa vinafanana bado siyo vya aina ileile moja na udhihirikaji wa magonjwa ya virusi hivi unatofautiana.
 
Hii habari ingenoga Sana Kama huyu aliebandika hii habari angeliweza kutafautisha baina ya herufi "R" na "L"..

Ukweli imepata tabu Sana kuisoma na kuifahamu hii habari.
 
Najiuliza kwa sababu ati hapa kwetu maabara iko Dar tu nchi nzima. Hivi hizo sample zinatumwa kwa WhatsApp? Kama sio zitasafirishwa ngapi na mara ngapi?

Kama kweli sisi ni dona kantri (donner country) na tunapaswa kutembea vifua mbele...basi tuoneshane katika vita dhidi ya kirusi corona.

Pitia link hii uone gharama - ila nikiri kuwa sijiu chochote ktk suala la corona.

Medicare is paying $36 for the CDC coronavirus test
 
Kwenye hili janga wako wanaifaidika haswa wauza majeneza wachimba makaburi Maabara Wapika ubwabwa misibani nk.
 
Umeutaja uzalendo, hongera sana, ila ngoja waje wenye povu lao wenye 'allergy' na hilo neno!
 
Mara nyingi mtu akiugua ugonjwa fulani na akafanikiwa kupona huwa inakuwa ngumu sana kuugua tena huo ugonjwa. Je, chanjo ya Corona ni kuugua Corona?
 
Viral infections nyingi hazina kinga wala dawa.

Ukiungua COVID19 na ukapona haimaanishi ndio umejenga kinga ya milele, ukipona na ukarudi mtaani ukaendelea na tabia za kutokujikinga utaukwaa tena na tena tenaa.

Ni kama mafua tuu, ukiyapata na ukapona haimaanishi hautayapata tena.


Unforgetable
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom