#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

Status
Not open for further replies.
Usipaniki. Serikali imejipanga na inatosheka na kituo cha Mlonganzila. Sample zitasambazwa kwa drones mara moja maana sisi ni matajiri na dona countiri.
 
Ingawa hadi sasa Corona imesababisha vifo zaidi kwa wazee na wagonjwa wenye magonjwa mengine, wagonjwa wenye upungufu wa kinga mwilini wawe chanjo na maambukizi ya COVID-19.

Katika Mkutano wa Virusi na Magonjwa Nyemelezi wa Machi 10, Dr. John Brooks wa CDC alitahadharisha kuwa maambukizi ya COVID-19 yanategemewa kuwa makubwa zaidi kwa wagonjwa wenye maradhi ya UKIMWI na CD4 chache au wale walio na VVU wengi ingawa wanapata dawa za kufubaza makali.

Ingawa haifahamiki kabisa kitakachotokea pindi watu wenye maradhi ya UKIMWI watakapopata maambukizi ya Corona, ni vyema sisi kama Taifa lenye maambukizi makubwa ya VVU tukachukua tahadhari zaidi.

Hadi mwaka 2018, Tanzania ilikuwa na wagonjwa wenye VVU zaidi ya milioni moja na laki sita (1,600,000), hivyo utagundua ni watu wangapi wako katika hatari za huu ugonjwa.
 
Wakati nilipokuwa nasoma maswala ya "health and safety" ambayo yanashabihiana ki mbinu na haya maswala mazima ya korona nilifundishwa zipo njia 5 zinazotofautiana ki vipaumbele katika kukabiliana na Hatari yoyote. ni kama ifuatavyo.

1. Elimination – Physically remove the hazard
2. Substitution – Replace the hazard
3. Engineering controls – Isolate people from the hazard
4. Administrative controls – Change the way people work
5. Personal protective equipment– Protect the worker with PPE

Inadhaniwa na wataalamu kuwa njia namba moja ya completely elimination ndiyo effective na njia ya mwisho ya kuwapa watu vitendea kazi vya kukabiliana na hatari ndiyo least effective.

Nilifundishwa Njia Namba moja ambayo ni ya kwanza katika kukabiliana na Hatari (hazard) na kukontrol athari zitokanazo na hatari (risk) ni Elimination – Physically remove the hazard. Ondoa kabisa kitu hatarishi. Mfano priority ya kwanza ni kuondoa Korona Kabisa.

Lakini pale inapokuwa haiwezekani kuondoa kitu hatari basi tunaenda hatua ya pili ambayo ni substitute. Kama tunaweza kupata kitu cha kuwa mbadala wa korona kisicho na madhara basi inakuwa vizuri

Inaposhindika kupata mbadala basi hatuaa ya 3 ni isolate people from the Hazard - hapa kama tunazungumzia korona maana yake ili kuwalinda watu wetu tulitakiwa ku isolate jamii yetu na vyanzo vyote ambavyo vingeweza kuleta korona kwetu. Hapa tumezuia watu wetu kwenda nje lakini hatujazuia wageni hasa kutoka nchi zenye maambukizi ya juu.

ikishindikana hapa tunaenda hatua ya 4 ambayo ni admistrative control, kujaribu kufundisha watu njia za kubadili mienendo hatarishi kama kuzuia mikusanyiko, kufundisha watu jinsi ya kufanya usafi kujikinga n.k

Hatua ya mwisho ni kuwapa watu vifaa vya kujikinga. kama mask, dawa za kunawia n.k

mimi ki mtizamo wangu sisi watanzania tunaanzia namba 5 kurudi namba moja na hilo ni tatizo kubwa. We are not guided by proffesionalism.

Yaani ni sawa na unasikia nyoka nyoka kwa jirani badala ya kumtafuta nyoka kumuua (elimination) au kuleta mdudu anayeweza kula nyoka kama paka (substitution) au kuhakikisha unafunga njia zote ambazo nyoka angeweza kupitia kuingia kwako (isolation) eti unahangaika kwanza na kuwagawia wanafamilia fimbo, viatu n.k eti ili kila mmoja aweze kupambana na nyoka akikutana naye, au unaanza kuwafundisha jinsi ya kupambana na nyoka. Hebu tupime wenyewe ni ipi njia sahihi ya kupambana na nyoka kwa vipaumbele?.
 
Mpaka sasa, Serikali haijafanikiwa kuwapa mafunzo watu mbalimbali juu ya kujikinga na virusi vya corona.

Jana nilikuwa Mwanza. Sehemu ya kuongilia, kwenye mlango kuna metal detector box ambapo mtu hupita. Vitu ulivyo navyo, kama simu, vitabu, saa, n.k.; kama ilivyo airport unaweka kwenye chombo ambacho kinasukumizwa na walinzi ili uvichukue upande wa pili. Walinzi wamevaa gloves.

Cha kushangaza, wanaoingia wote ni lazima vitu vyao vipite ndani ya zile containers. Maana yake ni kwamba kama kuna yeyote ana maambukizi, na vitu vyake vipo contaminated, na wale wengine wote watakuwa contaminated kupitia vyombo ambamo wanatumbukiza simu zao na vifaa vingine.

Mimi niliwakatalia. Bahati nzuri walinzi wale hawakuwa wabishi. Waliniruhusu lakini wengine waliendelea kama yalivyo mazoea.

Inaonesha bado maandalizi yetu ni hafifu.
 
Iwe amri abiria wanawe kabla na baada ya kupanda daladala au mwendokasi.

inchaji.
 
Kuhusu Corona, Kwanza COVID 19 Maana yake ni Corona Virus Disease ambao umebainika au kugundulika mnamo 2019 huko Wuhan China kwa wala mapopo. Hivi virus ni jamii ya virus ambavyo siku zote vikimuingia binadamu athari zake ni mafua.

Na zaidi sana hupatikana kwenye wanyama niliowataja. Kila binadamu huugua mafua lakini wanaoathirika zaidi ni wazungu ambao kwanza kinga zao zilishapata mtikisiko hasa watu wazima sana na sio vijana ingawa pia wanaweza kuupata.

Na pia wadudu hawa huenea kwa haraka maeneo yenye baridi na wale wapenda kula vitu vya baridi kama ice cream na barafu.

Idadi ya wanaoupata ugonjwa huu ni kubwa kulinganisha na wanaokufa kwa maana kwamba kinga ya mwili inasaidia ikiwa boosted hasa kwa kula matunda au vitamen C,

Kwa sisi waafrika tumelichukulia suala hili kama la kutisha sana baada ya kuona wenzetu wengi idadi yao wanaupata lakini cha msingi mafua ni kitu cha kawaida ambacho unaweza kuyatibu kwa njia za kuwa msafi kila wakati.

Pia nilikuwa sielewi sanitizers sasa nimeelewa na pia kuhusu masks ni kwa ajili ya waliathirika ili wasiwambukize wengine lakini wewe ambaye ni mzima kuna njia tatu mdudu anaweza kukupata macho, mdomo na pua je kila baada ya nusu saa waweza kubadilisha mask yako? (inavyoshauriwa) na unapoivua ni nani anakuvua maana hutakiwi kuivua mwenyewe.

Hali kadhalika na gloves unapoivaa hutakiwi kushika simu etc je wewe unafahamu jinsi unavyotakiwa kuivua na pia una habari helmet inaweza kuwa chanzo cha hao wadudu kusambaa?.

Kuna mengi niilikuwa siyafamahamu wewe unaweza kuongezea pia.
 
Wapendwa na JamiiForums,

Kila mmoja wetu anatambua inchi yetu na dunia kwa ujumla tupo kwenye taharuki ya ugonjwa wa corona.

Ombi langu kwa serikali yetu, kwanini isilete hvyo vipimo vya Corona hadi kwenye maduka ya watu binafsi ili pale mtu anapojihis ana dalili hzo aende duka analolitaka yeye nakupima kama ataonekana ana dalili hzo, hatua za matibabu zifanyike.

Ombi jingne: Vipimo hivyo vya corona viruhusiwe kuuzwa kama bidhaa nyingne ili kwa watu wenye nafasi zao waweze kununua kwa matumizi yao!.

Kinga ni bora kuliko tiba. Tujilinde.

[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Call your doctor: If you think you have been exposed to COVID-19 and develop a fever and symptoms, such as cough or difficulty breathing, call your healthcare provider for medical advice.

Watch for symptoms
Reported illnesses have ranged from mild symptoms to severe illness and death for confirmed coronavirus disease 2019 (COVID-19) cases.
The following symptoms may appear 2-14 days after exposure.*
  • Fever
  • Cough
  • Shortness of breath
*This is based on what has been seen previously as the incubation period of MERS-CoV viruses.

Kwa kuwa hakuna vipimo maalum watu au washukiwa wenye dalili hizo huwekwa karantini kwa siku 2-14 kumtizamia kama atakuwa na dalili kali hizo hapo juu.
 
Kuna dalili za wenye madaraka ya dunia kujaribu kuzuia mikusanyiko ya ibada. Tahadhari ambayo ningependa kuitoa mapema ni hii, corona virus ni pigo plague, Biblia inasema linapotokea pigo juu ya uso wa nchi, kusanyiko takatifu lije mbele za Bwana Mungu na kumuomba rehema, naye anatazuia na kukomesha pigo hilo.

2Mambo ya nyakati 7:13 Ninapofunga mbingu ili mvua isinyeshe+ nami ninapoamuru panzi waile nchi+ nami nikileta tauni katikati ya watu wangu,+ 14 na watu wangu+ ambao jina langu limeitwa+ juu yao wajinyenyekeze+ na kusali+ na kuutafuta uso wangu+ na wageuke kutoka katika njia zao mbaya,+ basi mimi nitasikia nikiwa mbinguni+ na kusamehe dhambi yao,+ nami nitaiponya nchi yao.

Kwa hiyo nawaonya mapema viongozi wetu wasije jaribiwa na misukumo na hofu zilizokumba dunia, watasababisha watu wengi kufa maana hakuna namna ya kuzuia corona zaidi ya maombi yanayofanywa kwenye ibada
 
Mkuu unahitaji kujifunza sana juu ya Agano jipya
 
Imani katika dini inaleta tumaini katika jamii. Sayansi na technolojia inaleta ukweli na maendeleo katika jamii

Hivo basi akli ya mwanadamu ni muhimu kuweka vipaumbele kulinga na hali halisi

Kwa sasa mkusanyiko wa Aina yeyote ni hatari hata ungekua wa malaika wenyewe
 
VIVIANET, Mimi naamini mapigo ya kipindi cha siku za mwisho bado. Ukitaka kujua hayo mapigo yatakuwaje nenda kasome kitabu cha Ufunuo wa Yohana sura ya 16: 1-18
Mapigo haya ukianza na:-
(i) jipu baya bovu juu ya wale wenye chapa ya mnyama
(ii) Bahari kuwa kama damu ya mfu
(iii) Mito na chemichemi za maji zikawa damu
(iv) Jua litawaunguza wanadamu kama moto N.K

Hizi ni rasha rasha kama za mvua tu ni kwamba mambo huko mbeleni yatakuwa magumu sana tujitahidi kumutafuta Mwenyezi Mungu aturehemu.
 
Mamlaka za kiserikali zinapochukua tafadhari na hatua za kulinda watu ili wasiangamie ama Kwa magonjwa ama kitu kingine chochote, mamlaka hiyo inakuwa inafanya kazi ya Mungu moja Kwa moja, Kwa maana Mungu hapendi mtu yeyote afe kabla hajamjua Yeye Kwanza

Kwa maana hiyo, Pindi mamlaka za kidunia zijapofanya kazi zake Kwa haki, kulinda watu wote kujaribu kuzui kile ambacho Mungu hapendi, huitwa ni mamlaka zinazofanya kazi karibu na Sheria za Mungu

Kuzuia mikusanyiko iwe ni ya kidini haiwezi ikawa sababu ya kuwafanya wenye Imani hizo wasiwe na ushirika wa Mungu wao

Kwa mfano Wakristo, wao wenyewe ndio kanisa (yaani, jengo la Ibada sio sehemu pekee ambapo Mungu wao aweza kuwapo) Bali mahali popote watakapokusanyika ima ni watu wawili au watatu, basi Kati Yao Mungu wao yupo

Kwa hiyo hoja yako hiyo ni nzuri Ila sio hitimisho la ukomo wa uweza wa Mungu Kwa wamuombao
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom