Dah! Urusi wameachia hiki kifaa kikachukuliwa kizembe sana, hii hasara sasa

Hizo ni propaganda, usiulize ni nani, ni vipi, ni lini, ili iweje?

Jamaa huyu anashangaza sana - sensational news 24X7
Hapo wazee wa Magharibi wanajibebea tu kwenda kukisoma kwa undani zaidi

Si ujifanya vinara wa technolojia na uwezo wa kufa mtu sasa kwa nini wanakwenda kuvizia kifaa. ambacho hakitakuwa na umuhimi wowote kwao ndio maana Warusi hawakuangahika kwenda kukifuata baada ya ndege kuanguka - mdio maana walikiacha peupe bila ya kuki-retrive wakati walikuwa na helicopters za kwenda kukifuata - NATO wali hilo hawalifikirii kabisa as far as they are concern wanajifariji kwamba finally wame come across a treasure trove!!
 
Mkuu unajua MIG na SUKOI ni Russian made ila hata Ukraine anamiliki na Poland pia 😅😅😅😅 acha kujitekenya

Umenikumbusha kitu mkuu, kuna waandishi wa habari wa kujitegemea ambao wapo front line waliwahi kusema uharibifu wa ndege, helicopters unao unao onyeshwa kwenye mitandao ya kijamii actually belongs to Ukraine Army na kwa kuwa Ukraine na Russia wana military flying machines zinazo fanana wanatumia propaganda zao kudanganya watu, picha nyingine na video zilichukuliwa 2014/15!!
 
Hako ni ka External fuel tank na tena ni empty, sasa la nini kama internal tanks zipo full
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Siko upande wa mtu yoyote lakin external fuel tanks hazikai hapo. Mostly zinakuwa attached under airframe au under wings not on the tips of the wings.

Hili nalo ukalitazame
 
Lazima wasande awamu hii na watafute suluhisho la mezani 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220913-161751.png
    150.8 KB · Views: 5
Mkuu sio kuwa wamekiachia kizembe, wamechapika hadi kuchakaa!!"yanini kujifia, kwani ni vita ya familia yako, kuwa unawatetea?
 
Tupunguze ukari wa maneno!
Mimi Sina upande ktk huu mgogoro lakini tusubiri tuone hatima ya haya ndani ya masaa kadhaa!
Nina Jamaa yangu yupo Frontline Kama doctor upande wa Ukraine, anasema Tangia Tarehe 09/09 mpaka Leo Jeshi la Ukraine limepoteza Mamluki zaidi ya 4000 na majeruhi 13,000 na zaidi. Ila hali ni ngumu ni Kama wanajitoa mhanga.
 
Wakuu siwaoni
Sikirimimimasikini
Bwana Utam
Na co🤣🤣🤣
 
Siko upande wa mtu yoyote lakin external fuel tanks hazikai hapo. Mostly zinakuwa attached under airframe au under wings not on the tips of the wings.

Hili nalo ukalitazame
Asante Sana Mkuu. Labda wewe atakuelewa.
 
Ukraine wakikamata au kuua askari wa Russia basi lazima wapige picha na kusambaza mitandao,Kuna baadhi ya picha mpaka zinakiuka maadili ila zinaletwa na askari wa Ukraine!
Ila Ukraine anavimba tu,lakini hasara halisi itajulikana vita ikiisha!
Mvamizi hawezi vamia kwako akafanya ukatili kisha akaweka kwenye social media. Atashambuliwa sana na jamii. Ni sawa na mtu aje kwako aue anyang'anye halafu apost kwenye social media.
 
Eti una dokta upande wa ukraine, hivi ninyi wahaya akina kalokola mtaacha lini sifa?
 
Mhhh! Kwani Mrussi aliambiwa kuna mtu anataka kuichukua Urussi?? Wanajeshi wa Urussi wanapigania Urussi gani iliyoko huko ndani ya nchi ya Ukraine?
 
Ni nani amekuambia ana upande?.
 
Mvamizi hawezi vamia kwako akafanya ukatili kisha akaweka kwenye social media. Atashambuliwa sana na jamii. Ni sawa na mtu aje kwako aue anyang'anye halafu apost kwenye social media.
Ndio maana nasema,Ukraine anakula kichapo Cha kimya kimya!
 
Mkuu, Hawajaenda kuvizia bali wamekipata kwa jasho baada ya kutungua ndege ya Adui-Mrussi.
Mkuu ni kwa vipi unasema hakitakuwa na umuhimu wowote kwao (NATO) wakati Mrussi mwenyewe alijua umuhimu wake ndo maana kakiweka kwenye ndege yake?
Warussi hawakuhangaika kwenda kukifuata kwani wangepita wapi na kwa kifaa gani? Isingewezekana kabisa hata kama wanatamania. Hawakuwa na muda wa kukiharibu kifaa hicho - wao walijali kujiokoa nafsi zao kwa kutimua mbio. Wanafahamu zaidi yako kwamba wangelijipeleka na helicopters kukifuatakama ulivyosema; na zenyewe including marubani wake zingetunguliwa na hivyo kuongeza hasara ya mali na watu.
Vita/mapambano ni pamoja na kumsoma adui:- mbinu zake, vifaa alivyonavyo na uwezo wa kuvitumia, morali wa wapiganaji wake......Kwa hiyo upatikanaji wa kifaa hicho ni Mujarab sana kwa NATO.
 
Hiyo ndio tafsiri ya vita. Vita sio nzuri hata kidogo. Huyo jamaa yako angekupa na Takwimu za Urussi (Madaktari huweza kuwasiliana hata kama ni upande mwingine) ili kupata uhalisia zaidi. Zingatia kwamba Kitendo cha askari wa Urussi kutupa silaha na kukimbia ni ishara wazi na ushahidi kwamba wamezidiwa mno i.e. wameona Vifo ni vingi sana na majeruhi ni wengi mno. Kwa hiyo wamelazimika (sio hiari) kujiokoa kwa kukimbia hata bila viatu na hilo ni agizo la amiri jeshi mkuu wa Urussi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…