Damas Ndumbaro: Marufuku kuvaa jezi ya Mamelodi au Al Ahly kwa Mkapa kwenye michezo ya Simba na Yanga
Nikivaa jezi yangu ya Manchester United nitaulizwa passport ya UK!
 
Imagine washabiki wa Mamelodi wanakuja kuishangilia timu yao, halafu wanajikuta wanaulizwa passport uwanjani kwa sababu ya jezi walizovaa.

Wakirudi kwao lazima tuwekwe kwenye vituko vya dunia.
Halafu anasema ni 'Uzalendo''. Tuna viongozi wa ajabu sana, uzalendo haubambikizwi ni 'itikadi ya mtu kwa taifa lake'
Kuwa mshabiki wa Yanga au Simba si uhaini wa nchi. Timu hizi zimekuwa na upinzani kwa miaka dahari

Upinzani wa Simba na Yanga ndio umezijenga katika ukanda wa A.Mashariki. Zama hizo Simba na Yanga wakicheza A.Mashiriki inazizima, ni kwasababu ya upinzani lakini haina maana ni kukosa Uzalendo.

Sioni tatizo kabisa ! nadhani tatizo wanalikuza tu. Nitavaa jezi yangu ya Man U.
 
Halafu anasema ni 'Uzalendo''. Tuna viongozi wa ajabu sana, uzalendo haubambikizwi ni 'itikadi ya mtu kwa taifa lake'
Kuwa mshabiki wa Yanga au Simba si uhaini wa nchi. Timu hizi zimekuwa na upinzani kwa miaka dahari

Upinzani wa Simba na Yanga ndio umezijenga katika ukanda wa A.Mashariki. Zama hizo Simba na Yanga wakicheza A.Mashiriki inazizima, ni kwasababu ya upinzani lakini haina maana ni kukosa Uzalendo.

Sioni tatizo kabisa ! nadhani tatizo wanalikuza tu. Nitavaa jezi yangu ya Man U.
Huwa tunamuonea sana Idi Amin kwa kumfanya kuwa alikuwa dikteta wa ajabu saana, wakati tuna viongozi wengi ukiwaweka katika mizani ya cross multiplication ya muda, elimu, nafasi, wanavyojimwambafy unajiuliza "huyu angekuwa na mazingira kama ya Idi Amin kweli asingekuwa Idi Amin wetu huyu?"
 
Eti ndio bingwa wa sheria wa simba ila kichwani empty
 
Ukija uwanja wa Taifa ukiwa umevaa jezi ya Mamelodi Sundowns lazima utuoneshe passport ya Afrika Kusini na ukiwa na jezi ya Al Ahly utuoneshe passport ya Misri, nje na hapo Polisi watakuchukua ukapumzike” Damas Ndumbaro, Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Yapi maoni yako?

Kwa kweli Serikali ya CCM haijawahi kuwa na viongozi wa maana zaidi ya Magufuli na Sokoine na kwa mbali Lowassa, huyu mtu inabidi akamatwe atiwe ndani kuongea ujinga wa namna hii.
 
Hakuan sheria inayosema ukiwa mtanzania basi ni lazima u-support Yanga au Simba. Huyo aliyesema hilo ni mpumbavu wa mwisho. Hivyo ni vilabu vya mpira na vina wachezaji kutoka nchi mbalimbali. Wamefikia kwenye udiktekta mpaka wanaamuru watu washangile timu ipi? Watanzania tungukuwa watu tunaojitambua, tungesusia kabisa kwenda mpirani siku hiyo ili liwe somo.
Kuna baadhi ya vitu mpaka unashangaa, utafikiri hii ni vita nchi yako inapigana na nchi jirani ambayo uzalendo ni lazima kwa maslahi ya Taifa
 
Kila nchi ina utaratibu wake. Na utaratibu wa Tanzania ndiyo huo, so ni lazima kuufuata.

Ova
Huu sio utaratibu ni kuingilia maamuzi ya mtu binafsi, na sio kosa kisheria una haki ya kushabikia timu yoyote

Sasa ule ustahamilivu wa 4 R za kiongozi wa nchi ina maana watendaji wake hawauishi??
 
B... Mi hili suala naunga mkono 100% tena tumechelewa sana. Tumekuwa kama wendawazimu kushangilia wageni.
Sawa, utani upo tutaniane (kama mimi ile siku ya Wydad japo najutaga sana) ila sio katika kiwango tulichofikia cha kuujaza uwanja kushangilia wageni.

Watakaokiuka wageuzwe mfano, na iwe serious maana nchi yetu hii utekelezaji sifuri.
Sio kushabikia Tu Hadi kuwapokea. Mpira WA Tanzania umeharibika Sana. Uzuri WAASISI WA uharibifu huo wako kwenye timu yako pendwa.😂😂
 
Ukija uwanja wa Taifa ukiwa umevaa jezi ya Mamelodi Sundowns lazima utuoneshe passport ya Afrika Kusini na ukiwa na jezi ya Al Ahly utuoneshe passport ya Misri, nje na hapo Polisi watakuchukua ukapumzike” Damas Ndumbaro, Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Yapi maoni yako?

Safi sana, Makolo Madunduka ushamba na hasadi umewazidi.
 
Hivi hawa mawaziri huwa wanajiandaa na mahojiano kwa maana nini la kusema? Nikisikia vitu kama hivi naanza kuwa na dharau na elimu ya Tanzania, huyu aliwahi kuwa waziri wa katiba na sheria nchi hii. Hivi Simba na Yanga wakiwa wamejiandaa vizuri kushinda kuvaa kwangu jezi ya Mamelodi au Alhly inaweza kuwa kisingizio cha kufungwa? Michezo ni furaha, utani ndio raha ya mpira wenyewe tusianze kugeuza viwanja vya mipira kuwa airport kuoneshana passport. Mambo ya kijinga kabisa.
 
Hata huku kuna washabiki kibao wa Liverpool, Man sijui Arsenal na wengine je tuoneshe passport za UK au? waziri boya sana, ndio shida ya kuwa na wizara zisizokuwa na kazi unaishia kutoa matamko kama uko nyumbani.
 
Back
Top Bottom