Dar es salaam limegeuka jiji la makelele, Serikali imelala?

Dar es salaam limegeuka jiji la makelele, Serikali imelala?

Bodaboda wanafunga honi za Harrier Lexus, yaani ni shida

Pia boda zimekua nyingi sana dar, hivi baada ya 5years hali itakuaje kwa wingi wao
20241223_235120.jpg
 
Wenzako wenye hela wamesogea Mbweni.

Hata iliyokuwa mitaa ya kishua Dar zama hizo, watoto wanaweza cheza mpira barabarani siku hizi dała dała zinakatiza.

Ukitaka amani sogea nje, akina sisi tusio na uwezo wa kununua Mbweni, utaratibu ni Kibaha.
Usafiri ukiboreshwa miundombinu ikiwa safi hata unaweza ukaishi Ikwiriri na kazi ukafanyia Dar !
 
Siku hizi ukitembea katika jiji la Dar es salaam, hali imekuwa si hali ni makelele mtindo mmoja. Hakuna utulivu kabisa.

Ukienda masokoni kila mwenye kibanda chake ana spika na rerding inayoita biashara yake non-stop kuanzia asubuhi saa mbili hadi usiku au jioni mida ya kufunga kazi.

Wakati huohuo kuna magari yanapita mabarabarani yanapiga muziki kwa sauti kubwa ajabu eti yanapromote makampuni fulanifulani. Wakati mwingine yanaweka kambi masokoni au sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na kufungulia maspika yake ya muziki. Yaani ni makelele tupu mijini.

Kwa sasa ukiwa jijini Dar es salaam, unafanya mishe zako hakuna utulivu, huwezi kuconcentrate.

Ukiacha hilo, utakutana na bodaboda nao wamefunga mziki mzito, wanapiga singeli mtindo mmoja.

Hapo sijazungumzia Bar zinazofungulia muziki non stop katika makazi ya watu.

Noise pollution Dar ni kubwa mno imesababisha watu waumwe vichwa, uwezo wa kusikia kupungua, msongo wa mawazo, Quality of life imeshuka mno na sababu mojawapo ni Makelele mtindo mmoja.

Serikali haina budi kufanya yafuatayo.

1. Kuzuia kila mwenye biashara yake masokoni kuwa na kimtambo cha kupiga kelele kuita wateja. Hivi vispeaker vinafanya maisha ya ufanyaji shughuli masokoni kuwa headache

2. Serikali ipige marufuku kwa bodaboda kufunga speaker kwenye mabodaboda yao, kwanza haya mamiziki wanayofungulia ni hatari kwa usalama barabarani.

3. Serikali ithibiti haya matangazo ya magari ambayo huzunguuka mitaani huku wamefungulia muzik kwa staili ya Disco.

4. Miziki kwenye mabar iangaliwe upya, limit ya kiwango cha sauti (decibels) kiwekwe ili kupunguzia wananchi adha.
Umesahau na wanaohubiri dini, hii yote ni kutokana na kuwa na rc mshamba.
 
Usiisahau misikiti na makanisa.
Waguse kote Ila sio hapo mkuu, msikiti ni achana ya dakika mbili, mara tano Kwa siku.
Which means is not a problem.

Kanisa ni sehem takatifu, Taifa letu linahitaji maombi, ili kutoka katika hatua tuliopo.

Bila hayo maombi hata Amani hii isingekuwepo
 
Ushaambiwa jiji la biashara then unalalamika kelele.
Hamia Mtwara/Lindi ambako kumetulia.
Dar ina wakazi 6M, wewe lonely ndo hupendi kelele.
Dar ni Jiji la biashara kuliko majiji kama Dubai na Tokyo?
Mbona huko hakuna hivyo vispika na makelele?

Kuna mdau huko juu amesema hali hiyo ya makelele na kupenda makelele ni dalili ya ujima na umasikini,nakubaliana nae kwa asilimia mia moja.
 
Waguse kote Ila sio hapo mkuu, msikiti ni achana ya dakika mbili, mara tano Kwa siku.
Which means is not a problem.

Kanisa ni sehem takatifu, Taifa letu linahitaji maombi, ili kutoka katika hatua tuliopo.

Bila hayo maombi hata Amani hii isingekuwepo
Mkuu hujakaa karibu na ile misikiti ya "swalaa, swalaa, kitanda chako ndiyo kaburi, shuka ndiyo sanda yako, swalaa swalaaa" wanakupigia makelele saa nzima sala ya alfajiri, bila kujali una imani gani?

Maombi hayatambuliki kwa wote katika secular state. Maombi yenu ombeni kanisani kwenu msiwapigie kelele wengine wasioamini kama nyie.
 
Waguse kote Ila sio hapo mkuu, msikiti ni achana ya dakika mbili, mara tano Kwa siku.
Which means is not a problem.

Kanisa ni sehem takatifu, Taifa letu linahitaji maombi, ili kutoka katika hatua tuliopo.

Bila hayo maombi hata Amani hii isingekuwepo
Hata Congo, Yemen, Palestina na Sudan wanaomba sana.
Halafu hamuwezi kuomba bila kelele??
 
Siku hizi ukitembea katika jiji la Dar es salaam, hali imekuwa si hali ni makelele mtindo mmoja. Hakuna utulivu kabisa.

Ukienda masokoni kila mwenye kibanda chake ana spika na rerding inayoita biashara yake non-stop kuanzia asubuhi saa mbili hadi usiku au jioni mida ya kufunga kazi.

Wakati huohuo kuna magari yanapita mabarabarani yanapiga muziki kwa sauti kubwa ajabu eti yanapromote makampuni fulanifulani. Wakati mwingine yanaweka kambi masokoni au sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na kufungulia maspika yake ya muziki. Yaani ni makelele tupu mijini.

Kwa sasa ukiwa jijini Dar es salaam, unafanya mishe zako hakuna utulivu, huwezi kuconcentrate.

Ukiacha hilo, utakutana na bodaboda nao wamefunga mziki mzito, wanapiga singeli mtindo mmoja.

Hapo sijazungumzia Bar zinazofungulia muziki non stop katika makazi ya watu.

Noise pollution Dar ni kubwa mno imesababisha watu waumwe vichwa, uwezo wa kusikia kupungua, msongo wa mawazo, Quality of life imeshuka mno na sababu mojawapo ni Makelele mtindo mmoja.

Serikali haina budi kufanya yafuatayo.

1. Kuzuia kila mwenye biashara yake masokoni kuwa na kimtambo cha kupiga kelele kuita wateja. Hivi vispeaker vinafanya maisha ya ufanyaji shughuli masokoni kuwa headache

2. Serikali ipige marufuku kwa bodaboda kufunga speaker kwenye mabodaboda yao, kwanza haya mamiziki wanayofungulia ni hatari kwa usalama barabarani.

3. Serikali ithibiti haya matangazo ya magari ambayo huzunguuka mitaani huku wamefungulia muzik kwa staili ya Disco.

4. Miziki kwenye mabar iangaliwe upya, limit ya kiwango cha sauti (decibels) kiwekwe ili kupunguzia wananchi adha.
Na bado! Saa100 Hana ustaarabu na umakini kwenye uongozi!
Tunaandika Jf Kila kukicha,ni malalamiko ila serikali haisomi na haifuatilii.
 
Back
Top Bottom